mamushkabrain
New Member
- Jun 16, 2010
- 2
- 0
Hodi hodi naingia, mara ya kwanza nachangia
roho yangu yafurahia , jamii forum kunukia
ila naumia kwa mada hii nachangia.
tunawaita wasomi, na macho yetu yapo kwao
tunajisisifu nao, kumbe tunajidanganya
si vyema nikizunguka, ngoja yangu hoja niitoe
Raisi kawatembelea, kutaka yao kura
kaenda wapamba vichwa, nao wajione bora
wakasahau shida zao, kumtwika ende nazo
juzi juzi katugomea, mishahara kuongozewa
na haha hao wasomi, ajirani waelekea
wasahau serikalini , ndipo vilio vilipo
wangeamua kulia, vilio vyao kusikika
wao wajitia kucheka, raisi kushangilia
lini Tanzania tutapata sauti?
vijana ndio nyie , macho mwayafunga
mnasahau ya mjomba, nyimbo awaimbia?
ingewapasa kusema, yale yote mlonayo
kwani ujio wake hamkuujua,mseme kawavamia?
mngeyaandika yakwenu, nanyi nafuu kujipatia
nyie si ndo viongozi , baadae kutuongoza?
kwa nini mwajinyamazia, nafasi mmepatiwa
ongeeni kwa niaba, jamii kuiokoa
ni kura kajawaomba, si hali kuwajulia
mkadanganyika na hilo, kura mkampatia
ni lipi alolitenda, kwa wenzenu walomaliza
ajira katuahidi, na maisha bora
yapo wapi hayo yote, kam asi utapelei
nawashangaa sana vijana, vigelegele mwamwagia
mmesahau ahadi, zote alowaambia
na mengi yakuyaandika, basi tu staki wachosha
ila jukwaani nitasimama
mengi nipate taamka
wana JF mpoooooooo?
roho yangu yafurahia , jamii forum kunukia
ila naumia kwa mada hii nachangia.
tunawaita wasomi, na macho yetu yapo kwao
tunajisisifu nao, kumbe tunajidanganya
si vyema nikizunguka, ngoja yangu hoja niitoe
Raisi kawatembelea, kutaka yao kura
kaenda wapamba vichwa, nao wajione bora
wakasahau shida zao, kumtwika ende nazo
juzi juzi katugomea, mishahara kuongozewa
na haha hao wasomi, ajirani waelekea
wasahau serikalini , ndipo vilio vilipo
wangeamua kulia, vilio vyao kusikika
wao wajitia kucheka, raisi kushangilia
lini Tanzania tutapata sauti?
vijana ndio nyie , macho mwayafunga
mnasahau ya mjomba, nyimbo awaimbia?
ingewapasa kusema, yale yote mlonayo
kwani ujio wake hamkuujua,mseme kawavamia?
mngeyaandika yakwenu, nanyi nafuu kujipatia
nyie si ndo viongozi , baadae kutuongoza?
kwa nini mwajinyamazia, nafasi mmepatiwa
ongeeni kwa niaba, jamii kuiokoa
ni kura kajawaomba, si hali kuwajulia
mkadanganyika na hilo, kura mkampatia
ni lipi alolitenda, kwa wenzenu walomaliza
ajira katuahidi, na maisha bora
yapo wapi hayo yote, kam asi utapelei
nawashangaa sana vijana, vigelegele mwamwagia
mmesahau ahadi, zote alowaambia
na mengi yakuyaandika, basi tu staki wachosha
ila jukwaani nitasimama
mengi nipate taamka
wana JF mpoooooooo?