Binafsi nimekuwa najiuli, hivi kwa nini serikali, na wachambuzi wengi walikuwa kinyume na hatua ya wabunge wa cdm kususia hotuba ya rais pale bungeni. Tena, hata hatua yao ya kutoka wakati wa marekebisho ya kifisadi ya kanuni za bunge. Lakini hakuna mchambuzi yoyote aliyekemea kitendo cha wabunge wa ccm kupiga kelele na kuwazomea wenzao wa cdm. Hata kama wabunge wa chadema hawakufanya ustarabu na kwamba walikosa uungwana kama wanavyosema ccm na wachambuzi wengine wenye mawazo kama wao, swali langu, je wao walikuwa wastaarabu na wavumilivu kwa kupiga kelele na kuwazomea watu wanaotoka kimya kimya tena kwa heshima zote.
Lakini kilichoniacha hoi zaidi ni pale na rais kukosa subira na kuanza kupiga vijembe na kujigamba mwisho wa hotuba yake ya pale bungeni. Hata hivyo, majigambo hayo hatukuyaona kwenye hotuba ya mwisho wa mwezi. Aliposema wazi kabisa kuwa bila ya viongozi wa cdm kutoa ushirikiano yeye na serikali hawawezi. Hili wana jf mnalionaje?
Lakini kilichoniacha hoi zaidi ni pale na rais kukosa subira na kuanza kupiga vijembe na kujigamba mwisho wa hotuba yake ya pale bungeni. Hata hivyo, majigambo hayo hatukuyaona kwenye hotuba ya mwisho wa mwezi. Aliposema wazi kabisa kuwa bila ya viongozi wa cdm kutoa ushirikiano yeye na serikali hawawezi. Hili wana jf mnalionaje?