Hivi sheria ya rushwa ina macho kuangalia nani katoa rushwa?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,486
30,166
Nianze mada yangu kwa kunukuu Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 18, ambayo inasema hivi "Kila mwanachi atakuwa huru kutoa mawazo yake na maoni hayo hayapaswi kuingiliwa na chombo kingine chochote" mwisho wa kunukuu.

Pili niseme kila mwananchi yuko huru kuihoji serikali yetu kwa kuwa sisi wananchi ndiyo WAAJIRI wa serikali iliyopo madarakani.

Sasa nije kwenye mada yangu ya leo, ni kuwa Rais wetu amekuwa akisisitiza kuwa serikali yake imapiga vita ya rushwa na vita hiyo haitamwangalia mtu aliyetoa rushwa hiyo.

Sasa cha ajabu ni kuwa kauli hiyo ya Rais haionyeshi uhalisia wake kwa kuwa sisi wananchi tunaona kuwa sheria hiyo inawahusu watu wengine peke yake na siyo wateule wa Rais, kwa kuwa ukiwa mteule wa Rais ni RUKSA kutoa rushwa!

Nitaeleza ni kwanini nasema wateule wa Rais ni RUKSA kutoa rushwa.

Wabunge wa upinzani Godbless Lema na Joshua Nassari walitoa picha za video zinazoonyesha namna mkuu wa wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, namna alivyohonga madiwani wa Chadema ambao walidaiwa kuwa wamehamia CCM kutokana na kuunga mkono utendaji mkono wa Rais!

Wakati kashfa hiyo ikiwa "mbichi" watanzania walishikwa na bumbuwazi pale mkuu huyo wa wilaya akipandishwa cheo na mamlaka ya uteizi na kuwa mkuu wa mkoa wa Manyara!

Sasa inaonekana wazi kuwa sheria ya rushwa ina "macho" na inaangalia nani kufanya, kama aliyefanya ni mteule wa Rais, RUKSA kufanya na ndicho kilichotokea kwa DC Mnyeti pamoja na kukiri kwake kuwa kweli alitoa rushwa na akaongea kuonyesha kiburi cha madaraka kuwa kama na wao Chadema wanataka kuhonga Ruksa iwahonga madiwani wa CCM!

Sasa kwa watu waliolewa madaraka yao kama CCM hivi sasa dawa yao ni moja tu kuwakataa katika chaguzi ndogo za udiwani zilakazofanyika November 26 mwaka huu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tukumbuke kuwa katika moja ya hotuba zake Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa unapopewa madaraka ni lazima ujichunge katika utendaji wako, akafananisha na kuwa kuna Waziri dogo wa kule Uingereza alituhumiwa kwa "kutembea" nje....

Pale alipoandika barua ya kujiuzuru kwa Waziri Mkuu, hata barua hiyo haikujibiwa badala yake Waziri Mkuu kutokana na kukasirika kwake wala hakumjibu badala yake akateua mtu kuziba nafasi yake.

Hapa TZ kinachofanyika ni vice versa, anayetuhumiwa kwa rushwa ndiye anapata Promotion ya kuwa RC!
 
Huyu ni mpindishaji mkubwa wa sheria za nchi. Kumbuka rushwa aliyowapa Wabunge wa MACCM ya milioni 10 kila mmoja. Huyu ni mvunjaji wa sheria nchini ukiangalia vyeti na jina fake la Bashite, rushwa ya mnyeti, ukwapuzi wa bilioni 16 za wahanga wa tetemeko, kujichotea pesa hazina kama vile anatoa mfukoni mwake, kumfukuza kazi Nape. Ni janga la Taifa huyu jamaa kama anafanya yote haya kabla ya 2020 subiri baada ya wizi wa kura wa kutisha 2020 kwa kutumia mtutu wa bunduki na kitengo chake cha wizi wa kura. Nchi itakuwa katika hali mbaya sana.

Nianze mada yangu kwa kunukuu Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 18, ambayo inasema hivi "Kila mwanachi atakuwa huru kutoa mawazo yake na maoni hayo hayapaswi kuingiliwa na chombo kingine chochote" mwisho wa kunukuu.

Pili niseme kila mwananchi yuko huru kuihoji serikali yetu kwa kuwa sisi wananchi ndiyo WAAJIRI wa serikali iliyopo madarakani.

Sasa nije kwenye mada yangu ya leo, ni kuwa Rais wetu amekuwa akisisitiza kuwa serikali yake imapiga vita ya rushwa na vita hiyo haitamwangalia mtu aliyetoa rushwa hiyo.

Sasa cha ajabu ni kuwa kauli hiyo ya Rais haionyeshi uhalisia wake kwa kuwa sisi wananchi tunaona kuwa sheria hiyo inawahusu watu wengine peke yake na siyo wateule wa Rais, kwa kuwa ukiwa mteule wa Rais ni RUKSA kutoa rushwa!

Nitaeleza ni kwanini nasema wateule wa Rais ni RUKSA kutoa rushwa.

Wabunge wa upinzani Godbless Lema na Joshua Nassari walitoa picha za video zinazoonyesha namna mkuu wa wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, namna alivyohonga madiwani wa Chadema ambao walidaiwa kuwa wamehamia CCM kutokana na kuunga mkono utendaji mkono wa Rais!

Wakati kashfa hiyo ikiwa "mbichi" watanzania walishikwa na bumbuwazi pale mkuu huyo wa wilaya akipandishwa cheo na mamlaka ya uteizi na kuwa mkuu wa mkoa wa Manyara!

Sasa inaonekana wazi kuwa sheria ya rushwa ina "macho" na inaangalia nani kufanya, kama aliyefanya ni mteule wa Rais, RUKSA kufanya na ndicho kilichotokea kwa DC Mnyeti pamoja na kukiri kwake kuwa kweli alitoa rushwa na akaongea kuonyesha kiburi cha madaraka kuwa kama na wao Chadema wanataka kuhonga Ruksa iwahonga madiwani wa CCM!

Sasa kwa watu waliolewa madaraka yao kama CCM hivi sasa dawa yao ni moja tu kuwakataa katika chaguzi ndogo za udiwani zilakazofanyika November 26 mwaka huu.
 
Naona mleta mada umejigeuza mahakama ya kutafsiri sheria na kuhukumu unaowahisi wamekula rushwa.
 
Naona mleta mada umejigeuza mahakama ya kutafsiri sheria na kuhukumu unaowahisi wamekula rushwa.
Nimesema kuwa huyo mteule wa Rais Alexander Mnyeti ametuhumiwa kutoa rushwa.

Sasa kwa utaratibu wa kawaida wa serikali inayoongoza kwa utawala bora ilibidi jamaa Mnyeti akae pembeni kwanza "pending" investigation, lakini badala yake tunashuhudia anapandishwa cheo!
 
Huyu ni mpindishaji mkubwa wa sheria za nchi. Kumbuka rushwa aliyowapa Wabunge wa MACCM ya milioni 10 kila mmoja. Huyu ni mvunjaji wa sheria nchini ukiangalia vyeti na jina fake la Bashite, rushwa ya mnyeti, ukwapuzi wa bilioni 16 za wahanga wa tetemeko, kujichotea pesa hazina kama vile anatoa mfukoni mwake, kumfukuza kazi Nape. Ni janga la Taifa huyu jamaa kama anafanya yote haya kabla ya 2020 subiri baada ya wizi wa kura wa kutisha 2020 kwa kutumia mtutu wa bunduki na kitengo chake cha wizi wa kura. Nchi itakuwa katika hali mbaya sana.
Umesema kweli tupu mkuu BAK

Hizi ni raaha rasha tu, baada ya uchaguzi wa 2020 tutashuhudia vitu vya ajabu sana ambavyo Taifa letu halijawahi kupitia tokea lipate Uhuru wake!

Tumwonbe Mungu wetu atunusuru na hali hiyo inayokuja......
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nimesema kuwa huyo mteule wa Rais Alexander Mnyeti ametuhumiwa kutoa rushwa.

Sasa kwa utaratibu wa kawaida wa serikali inayoongoza kwa utawala bora ilibidi jamaa Mnyeti akae pembeni kwanza "pending" investigation, lakini badala yake tunashuhudia anapandishwa cheo!
.
Mkuu, tuhuma zisizo za kiutumishi au zisizohusiana na maadili ya utumishi hazimzuii mtumishi kupanda cheo au kupata promotion. Vilevile kiuhalisia Mnyeti katika utumishi wake hana tuhuma. Hii ni kwa sababu hajatuhumiwa na chombo au mamlaka yeyote ile inayotambulika (mfano kamati ya maadili ya utumishi). Hata huko wanakodai wamepeleka "tuhuma" zao, yaani TAKUKURU, bado hakutoshi kuibua tuhuma halali. Kilichopelekwa TAKUKURU ni taarifa tu. Na TAKUKURU wakiamua kuchukua hatua zaidi basi hizo hazitakuwa "tuhuma", bali hatua za kisheria.

Tusipende sana kuhukumu mapema pasipo kuzingatia matakwa ya kisheria yakoje. Kuanza kupiga kelele kuwa Mnyeti au fulani ana tuhuma inapelekea kuingilia mamlaka ya Raisi. Maana watu wanapiga kelele ili kumuonesha Raisi kuwa uteuzi wake una walakini na/au haufai.

Kuna namna ya kupinga teuzi zinazofanywa na Raisi kisheria, kelele tu hazisaidii na ni ulimbukeni. Kumbuka tuhuma sio kosa. Na Raisi anayo mamlaka aliyopewa kikatiba ya kufanya uteuzi wa mtu aliyekidhi vigezo.
 
Back
Top Bottom