Rais wa CWT ndugu Mkoba amekuwa ni bigwa wa maneno zaidi kuliko vitendo. Inavyoonekana ndg, huyu amekuwa akilichukulia suala hili kama sehemu mojawapo ya kitega uchumi chake, kwan uzoefu unaonyesha mara tu anapotangaza mgogoro na serikali, huitwa na kupozwa kwa kitu kidogo na hatimaye huahirisha mgomo na kuwaacha walimu na wapenda mabadiliko ya elimu njia panda wasijue la kufanya. Kwa mgogoro huu alioutangaza anatushawishi vipi tumuamini kama siyo mbinu yake ya kuitisha serikali ili mwisho anufaike kwa kupata kitu kidogo na kuwaacha tena walimu solemba?