Hiyo ni nyumba ya kawaida tu na unatakiwa upige hesabu ya nyumba mbili za kawaida tu, tofauti ni hiyo flow ya zege inayotenganisha nyumba ya juu na chini.
Piga hesabu ya kufunika hiyo flow ya juu kwa gharama ya nondo, saruji, kokoto na mchanga.
Majengo kama hayo hujengwa na wahandisi walio na leseni, sio mafundi wa mtaani hivyo unaweza kupiga hesabu hasa ya kumlipa kuanzia kwenye mashimo makubwa ya msingi hadi kufunika sakafu ya juu na baada ya hapo unaweza kuajiri mafundi wa kawaida kumalizia japo sina hakika kama mhandisi anaweza kuchukua tenda ndogo.
Kuna mhandisi wa umeme utatakiwa kumpa zabuni ila ukikomaa vizuri unaweza kusave mil.100 japo inaweza isiishe kabisa lakini ikahamia na kuanza maisha yako huku ukiimalizia taratibu.
Majengo kama hayo yanakuwa na gharama kubwa endapo utakuwa unanunua vifaa vya ujenzi kwenye hardware za mitaani, ila kama utaamua kununua saruji kutoka kuwandani, nondo kiwandani, mabati/vigae kiwandani, vioo na frame zake kiwandani huku tofali ukazitengrneza mwenyewe gharama itapungua kuliko kununua kwa mawakala wa kati.