Hivi Nyuki Wanahitaji Kujengewa Chuo Kikuu na Serikali?

Hivi Nyuki Wanahitaji Kujengewa Chuo Kikuu na Serikali?

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
79,088
Reaction score
84,978
Serikali inajenga Chuo Kikuu cha Nyuki mkoani Singida, lengo ni kutoa elimu ya sayansi ya masuala ya nyuki ambayo itasaidia watu, pia lengo lingine ni kumuenzi Liti Kidanka “Malkia wa Nyuki” aliyepambana vita na Wakoloni wa Ujerumani kwa kutumia nyuki.

Screenshot 2025-05-09 201202.png
 
Katavi kuna chuo cha SUA, Mizengo Pinda Campus kinafanya tafiti na kusomesha kozi za Ufigaji nyuki.

To my side: Nyuki ni Mdudu Mkubwa sana kwenye dunia hii. Ila kujua faida zake mpaka umfuatilie na kuelezwa.
 
Serikali inajenga Chuo Kikuu cha Nyuki mkoani Singida, lengo ni kutoa elimu ya sayansi ya masuala ya nyuki ambayo itasaidia watu, pia lengo lingine ni kumuenzi Liti Kidanka “Malkia wa Nyuki” aliyepambana vita na Wakoloni wa Ujerumani kwa kutumia nyuki.

View attachment 3329038
Umeuliza swali bovu sana.Ningekuwa nimelewa kindi au mtukuru,ningehitimisha kwamba wewe ni mpumbavu sana kumbe siyo.
NB;Hivi kwa nini tunafundishwa kuhusu pollination/uchavushaji wakati nyuki tunaishi nao kila sehemu.
 
BICHWA KOMWE sasa niende Singida "nikachukue" DIPLOMA YA KUVUNA ASALI.

Nitaambatana na BINTI SINGIDA binti kiziwi na yeye akaongeze ujuzi, aachane na ile CERTIFICATE IN SECRETARIAL STUDIES.

Tukitoka hapo tunaenda VETA kujifunza kuunda MIZINGA ya kufugia nyuki kwa kutumia mbao za mninga na ngozi ya pundra.

Cc: Lamomy Nyani Ngabu Lucas Mwashambwa Mbaga Jr secretarybird cocastic DR Mambo Jambo
Tutaenda wote bibie maana ukienda mwenyewe akina mkumbo watakukula.
 
Kweli vita haichagui silaha, serikali ambayo haiamini uchawi inamuenzi na kujivunia ndg ccm LITI ambae alikua anatumia sayansi ya giza, maajabu ya dunia hayapo 7 tena, bali sasa kuna ya nane, ya tisa, na kumi, yanapatikana tanzania.
 
Mwanasayansi Nguli duniani Albert Einstein alipata kusema hivi kuhusu nyuki “If the bee disappears from the surface of the earth, man would have no more than four years to live.” ningekua na muda ningekueleza jinsi gani nyuki ni Uchumi unaojitegemea,Ni Tiba kamili,ni Chakula kamili,Ni utalii,ni Elimu, mchavushaji wa mazao karibia ya 80℅,Ni mlinzi shidi ya wanyama vamizi kama Tembo nk

Kuna Siku nitaweka Uzi hapa kuhusu uchumi wa Nyuki upate maarifa.
 
Uhuni Mtupu Wa CCM
wakati mwingine muwe mnawapa ccm maua yao, si kila kitu wanachofanya ni uhuni. Umewahi kusafiri kwenda singida? Angalia kando ya barabara ukiwa mkoani singida utaona asali kwa wingi ikiuzwa. Mmekariri singida ni alizeti na vitunguu tu, kuna bidhaa zingine zipo, kuna viazi vitamu, uwele, mtama, karanga na mazao mengine mengi tu. Kuna kijiji cha nyuki ndani ya manispaa ya singida, hivyo basi kujengwa chuo cha nyuki huko ni muafaka, nyuki wapo kwa wingi sana wanazurura kwa makundi yao wakitafuta pa kutua watengeneze asali
 
wakati mwingine muwe mnawapa ccm maua yao, si kila kitu wanachofanya ni uhuni. Umewahi kusafiri kwenda singida? Angalia kando ya barabara ukiwa mkoani singida utaona asali kwa wingi ikiuzwa. Mmekariri singida ni alizeti na vitunguu tu, kuna bidhaa zingine zipo, kuna viazi vitamu, uwele, mtama, karanga na mazao mengine mengi tu. Kuna kijiji cha nyuki ndani ya manispaa ya singida, hivyo basi kujengwa chuo cha nyuki huko ni muafaka, nyuki wapo kwa wingi sana wanazurura kwa makundi yao wakitafuta pa kutua watengeneze asali
Uliyoyataja Yapo Sehemi Nyingi Sana Tanzania
Tabora , Rukwa, Katavi
 
Nadhani hicho chuo kinabidi kiwe na mtaala wa sio tu maswala ya nyuki na mazao yake lakini pia na mazoo ya misitu ikiwemo tiba zake. Kuna vingi hatujui kama wanajamii juu ya mazao ya misitu.
 
Sijasoma habari yote lakini kama ni Singida bilashaka itakua ni pamoja na "drone" ndege nyuki, "wadudu" ndege nyuki asilia na "Ungo ama UFO" ndege invisible.
 
Nadhani hicho chuo kinabidi kiwe na mtaala wa sio tu maswala ya nyuki na mazao yake lakini pia na mazoo ya misitu ikiwemo tiba zake. Kuna vingi hatujui kama wanajamii juu ya mazao ya misitu.
Songida Kuna misitu?
 
Back
Top Bottom