Hivi ni lazima wadada mvae shela na kushika maua mkononi?

katichi

JF-Expert Member
Nov 26, 2016
2,011
1,177
Habari za jioni wakuu? Shalom!

Rejea kichwa hapo juu, kwa Hakika hakuna kijana anaejielewa anayependa kuingia katika taasisi nyeti ya ndoa kwa njia isiyoeleweka namanisha isiyo rasmi yaani bila kupata baraka za kanisa na wazazi.

Siku za karibuni tumeshuhudia sherehe za kufunga ndoa zikiwa za kufuru unaweza kuta harusi moja inagharimu Tsh. 45 milioni huku bibi harusi akirukaruka na shela lake na kupamba mitandao ya kijamii ili mashoga wajue rasmi kuwa ameshapata mwenza .

Jambo la kushangaza bajeti nzima ya harusi inategemea michango ya kuomba unaweza kuta Bwana harusi na familia yake wanachangia Tsh. 4 millioni kati ya Tsh 45 millioni zinazohitajika.

Binafsi kufanya harusi kwa michango ya kuomba naona kama roho yangu haiafiki natamani mfano nikitaka kuuoa namchukua mwanawali akiwa amevaa nguo zake nzuri sio shela tunaenda zetu kanisani tunafungishwa ndoa iliyopata kibali cha Mungu wa mbinguni baadaye tunaondoka zetu tunaenda kuishi pamoja.

Sasa swali langu, je Mdada unaweza kubali kuingia ndoani bila shela wala 'party' za kuwalingishia mashoga lakini tunaenda kanisani kama kawaida bila kujisikia mnyonge?

NB
Binafsi sipendi mambo ya kusumbua watu kuchangishana.

Naomba kuwasilisha!
 
Na pia unaweza kujichanga ukafanya simple party kwa 2m na sherehe ikabamba vilivyo ukaacha historia.

Maisha ni kuchagua.

Wewe fanya yako ya 2M ibambe mwingine atafanya ya 300M ili ibambe.
 
Baba na mama yangu walioana na sherehe yao walichangiwa. Na wao wenyewe wanachangia waliowachangia.

Na mimi nilipokuwa mkubwa nikaanza kuchangia marafiki zangu na wao wakaja kunichangia. Na naendelea kuwachangia wengine. Process inaendelea kwa namna hiyo.

Kuchanga inakuwa ngumu endapo wazazi wako hawakuoana au walioana kienyeji na wewe binafsi hauna mpango wa kuoa harusi. Huwezi kuona umuhimu wa kuchanga.
 
Uko vizuri mkuu kwa ubanaji matumizi
Mkuu ni kweli lakini wengi wao wanatehemea michango ya kuomba hii imekaaje? Kipi bora kuomba omba au kufanya kawaida tu bila kutegemea michango ya watu kuomba omba kwataka moyo.
 
Mimi naenda kuoa ila nitwapromise nitarudi kwa ajili ya sherehe then hawanioni tena
 
Iko njema ila hayo maamuzi magumu huwa huleta mtafaruku mda ukipita.
Mmmmh mtafaruku upi mkuu au watu kununa kisa hawakula wali ?

Kwanza watu kipindi hiki cha Magu wagumu sana kuchangia harusi ninamfano halisi kabisa rafiki angu kaangukia pua watu hawajatoa fedha kabaki kulia lia.
 
Mkuu ni kweli lakini wengi wao wanatehemea michango ya kuomba hii imekaaje? Kipi bora kuomba omba au kufanya kawaida tu bila kutegemea michango ya watu kuomba omba kwataka moyo.
ni kweli kabisa mkuu
 
Uko vizuri mkuu kwa ubanaji matumizi
Mi namuunga mkono sipendiii hiyo michango michango, kwanza sherehe nyingi za sasa hivi zimekosa staraa unakuta watu wazima wamevaa vivazi vya ajabuajabu wanacheza hovyo hovyo bila mpangilio hawajui km mle kuna wazazi, istoshe mijitu inabeba hadi watoto wadogo wengine wabebwa mgongoni MTU anacheza singeli Yuko na mtoto mgongoni mtu kavaa gauni fupi miguu imekomaa km anacheza Mpira wa miguu, ziwa limeshakuwa ndala lipo nje lote akichezaaa looo acheni wanawake wenzanguu haileti picha nzuri kwenye jamii,,,,

Sasa unakuta ma bibi harusi wengine wimbo wowote utakaopigwa kakurupuka huyoo anachezaa hovyoo na mabwana harusi wengine ikipigwa twanga pepeta mwanaume anakata nyongaa utafikiri yupo kwenye mashindano ya BSS,,,,,,,,

Ikitokea nikaolewa sitofanya sherehee kuuubwa ya kukufuru Bali watakuja marafiki wachache ndugu wapande zote mbili kasherehe kangu na kawaida very simple....

Mkumbuke sherehe ni ya Siku moja tuuu ila ndoa ni ya maisha kufa na kuzikana mkiwa ndani mwenu hawatawaona wala kusikia shida zenu na raha zenu hata ukiwaringishia hao mashoga ni Siku moja tuuu
 
Mi namuunga mkono sipendiii hiyo michango michango, kwanza sherehe nyingi za sasa hivi zimekosa staraa unakuta watu wazima wamevaa vivazi vya ajabuajabu wanacheza hovyo hovyo bila mpangilio hawajui km mle kuna wazazi, istoshe mijitu inabeba hadi watoto wadogo wengine wabebwa mgongoni MTU anacheza singeli Yuko na mtoto mgongoni mtu kavaa gauni fupi miguu imekomaa km anacheza Mpira wa miguu, ziwa limeshakuwa ndala lipo nje lote akichezaaa looo acheni wanawake wenzanguu haileti picha nzuri kwenye jamii,,,,

Sasa unakuta ma bibi harusi wengine wimbo wowote utakaopigwa kakurupuka huyoo anachezaa hovyoo na mabwana harusi wengine ikipigwa twanga pepeta mwanaume anakata nyongaa utafikiri yupo kwenye mashindano ya BSS,,,,,,,,

Ikitokea nikaolewa sitofanya sherehee kuuubwa ya kukufuru Bali watakuja marafiki wachache ndugu wapande zote mbili kasherehe kangu na kawaida very simple....

Mkumbuke sherehe ni ya Siku moja tuuu ila ndoa ni ya maisha kufa na kuzikana mkiwa ndani mwenu hawatawaona wala kusikia shida zenu na raha zenu hata ukiwaringishia hao mashoga ni Siku moja tuuu
Dadaangu kumbe uko vizuri hivi
 
Inawezekana sana,tena unakuwa na amani na watu wote, hata wakikuletea kadi zao una uamzi wakuchanga au usichange na hakuna wakukuuliza. Tusilazimishe vitu vinavyopaswa kufanyika kirahisi vituumize kwa kuwafurahisha wengine
 
Msimamo wako au wenu. Wewe na mwenza wako ndio utakaoamua gharama za harusi. Unaweza sema wewe utapangilia harusi gharama ndogo ila mwenza wako akataka harusi kubwa ya kuacha gumzo. Ukilazimisha ndogo bila muafaka na mwenza wako utatia doa kwenye maisha ya ndoani.

Wadada wengi wanapenda kuringishia picha za harusi mitandaoni,potelea mbali bwana harusi asiwepo pichani ila yeye na shela yake ya gharama lazima picha zimwagwe kwa wingi kupata sifa mitandaoni
 
Back
Top Bottom