Hivi ni kweli rais Magufuli ndio karuhusu 'machinga'?

Chapa Nalo Jr

JF-Expert Member
Dec 8, 2010
7,515
6,489
Kwa wakazi wa DSM, na pengine hata miji mingine hapa Tz mtakubaliana nami kuwa hali ya usafi na mpangilio wa matumizi wa maeneo mijini umekuwa shang'ala bhang'ala.

Kwa sasa machinga wanapanga biashara kila eneo lililowazi, wamebana upana wa barabara kwani mali zao zinaingia mpaka barabarani na hivyo waenda kwa miguu sehemu zingine wana share barabara na magari. Sehemu za kupita watu kwa miguu zimechukuliwa na machinga. Vituo vya daladala hamna pa kukaa au kusimama ili kusubiri abiria.

Pembezoni mwa barabara mpya za mabasi ya mwendo kazi nako ni aibu tupu. Wauza machungwa, madafu, maembe, mahindi ya kuchoma, vimshikaki vya 50, waliomwaga nyanya chini na viungo mbalimbali wameachwa wakizichafua hizo barabara na kuondoka.

Mbaya sasa hata yale maeneo ya karibu na Ikulu wameshasogea na usikute muda si mrefu watakuwa wamepanga bidhaa zao lango la ikulu.

Naamini mpangalio katika mji ni muhimu kama vile ilivyo muhimu kupanga vema vitu nyumbani kwako.

Hawa machinga wakiachwa hivyo mpaka wakaji-establish ktk maeneo tajwa hapo juu, basi siku utakapoamua kuwatoa hakika litazuka balaa kubwa.

Kuna maneno yanapita pita huko tukiuliza kuwa eti ni amri ya JPM kuwa eti machinga waachwe wafanye watakavyo. Na tetesi zingine ni kuwa eti iliamuliwa hivyo ili UKUTA ukose waungaji mkono. Sijui sijui sijui. Lakini kwa vyovyote ni bomu kubwa hakika kwa huu mwenendo wa machinga.

Ni rai yangu kama ni kweli hizi vurugu za machinga ni ruksa ya JPM basi namuomba asome angalau maoni yangu haya labda anaweza kuamua vinginevyo kwa heshima ya miji yetu. Mgeni akija kwako aone kweli ni mtu uliestarabika. Uchafu ukizidi utakaribisha machizi kuona ni halali kunya popote. Yaani una ugeni muhimu jijini halafu jiji lote linanuka mavi. Hapana hapana hapana aisee!!!!
 
Hakika sasa hali ya usafi katika jiji imekuwa mbaya sana, lakini watembea kwa miguu ndio tunapata shida ,hatari kubwa inatukabili kukwepa kukanyaga bidhaa huku madereva wa daladala wakikimbizana kuwahi abiria pasipo kujali tupitao pembezoni,tunaomba mamlaka husika zitafakari kwa kina jinsi ya kuondoa HATARI hii
 
Ukipita kariakoo saaasa hivi ni kero kubwa. Hasa mitaa ya Gerezani terminal mpaka msimbazi. Sio siri wamachinga wengi wachafu. Wanachafua jiji kwa takataka mpaka kelele. Ni aibu kwa jiji kama la dar kuwe na foleni hadi ya watembea kwa mguu. Service road sio zenu nyie wamachinga. Period
 
Kumbe UKUTA ulimyumbisha jamaa hivi?
Mi nilikuwa naiuliza, kuna kipindi wamachinga walikuwa wanatimuliwa maeneo haya:
1.K/Koo gerezani kwenye kituo cha magari ya mwendokasi
2. Ubungo darajani hadi mataa, wakahamishiwa barabara ya kuingia stand mawasiliano.
3. Mbezi luis barabara ya stand ya zamani (kushoto) unapoekekea stand mpya.
Baada ya muda nikaona business as usual.

Sijui atalegeza mangapi kwa hofu ya UKUTA?
Ipo siku atatangaza ajira mpya na kuwapandishia wafanyakazi madaraja na mishahara yao UKUTA ukipamba moto tena.
 
Hili ni jukunu la jiji ambalo lipo chini ya UKAWA
Kumbuka jiji halina chombo cha dola kuweza kudhibiti kusanyiko kubwa la machinga. Sasa kama mwenye mamlaka na vyombo vya dola ameruhusu hilo basi uongozi wa jiji utaishia kukataza tuu lakini uwezo wa kuwaondoa wabishi hawana.
 
Kumbe UKUTA ulimyumbisha jamaa hivi?
Mi nilikuwa naiuliza, kuna kipindi wamachinga walikuwa wanatimuliwa maeneo haya:
1.K/Koo gerezani kwenye kituo cha magari ya mwendokasi
2. Ubungo darajani hadi mataa, wakahamishiwa barabara ya kuingia stand mawasiliano.
3. Mbezi luis barabara ya stand ya zamani (kushoto) unapoekekea stand mpya.
Baada ya muda nikaona business as usual.

Sijui atalegeza mangapi kwa hofu ya UKUTA?
Ipo siku atatangaza ajira mpya na kuwapandishia wafanyakazi madaraja na mishahara yao UKUTA ukipamba moto tena.
Ujumbe huu uwafikie wahusika. Hofu ya Siasa za UKUTA zisiharibu mandhari ya jiji
 
Nakumbuka maeneo ya Ubungo darajani riverside palikuwa kweupe unatembea bila tatizo lakini baada ya machinga kule Mwanza kuruhusiwa kufanya biashara zao barabarani na huku ikaanza kurudi biashara. kwa sasa pale darajani kupita nishida. biashara+pikipiki > mtembea ka miguu kupita ni shida. na huwa wanaweka mawe ambayo wakiondoka huyaacha hapo darajani.
 
Arusha ndio imekuwa balaa! Geneva of Africa imefunikwa na machinga kila barabara. Najiuliza: Mwenye duka anayetakiwa atoe risiti ya mashine ili kodi iende serikalini ana machinga kibao mbele ya duka lake wanaozuia wateja wasiingie dukani. Tena machinga hao wanauza mali zile zile anazouza mwenye duka lakini machinga hatoi risiti. Kwa mtindo huu si lazima mapato ya serikali yatashuka sana? Hivi ni kweli huo ndio msimamo wa serikali kwamba machinga wanaruhusiwa kuweka biashara zao.popote? Naomba viongozi wa serikali wajibu ili tujue ukweli
 
Hii ni aibu kubwa!! Huwezi kukusanya kodi kwenye hali holela kihivi!! Sijajua lengo ni nini? Labda Makondo atakuja kutusimulia
 
Acha ubinafsi wwe maadamu u kula kulala acha vijana wapate riziki ikifika jion wamechoka na Kazi na hela ya kula wanayo hivo hawatupigi roba kuliko wakikaa vijiweni Bila shughuli.Kila sehemu duniani kuna machinga waliotengewa maeneo maalamu wafanye biashara,huku tumeshindwa kuwawekea miundo mbinu viwanja vya wazi open market vishauzwa vyote.Usifiche aibu yako Kwa mgeni I hali unakufa njaa acha waje ili waone tofauti yao na third world,cha msingi ni kuwarasimisha na kuwatoza kozi labda 500 Kwa siku na kuwawekea Sheria ya usafi ,pia watafutie maeneo jirani na stand wajengewe wapangishwe ili jiji lipate mapato na wao wapate riziki.Mfano Ile stand ya Gerezani ukijenga frem ndani na nje zinatoka Jumla ya frem 2000 Kwa hela ndogo laki Mbili Kwa mwezi hapo jiji litapata zaid ya milioni 400 Kwa mwezi,Kwa mwaka ni bilioni 5 kwa gerezani tu ujaja mnazi mmoja yote pembeni mwa ukuta,kivukoni kuanzia azam marine had ferry,ukuta wa shule ya uhuru ,kidogo chekundu, nk panadizainiwa vizuri kimvuto.jiji litapata zaid ya bilioni moja na nusu kwa mweziambayo itaongeza mapato ya jiji.Hapo utakuwa umesaidia vijana kupata sehemu ya kufanya biashara na jiji kupata mapato.Tuwatumie machinga Kwa faida.
 
Acha ubinafsi wwe maadamu u kula kulala acha vijana wapate riziki ikifika jion wamechoka na Kazi na hela ya kula wanayo hivo hawatupigi roba kuliko wakikaa vijiweni Bila shughuli.Kila sehemu duniani kuna machinga waliotengewa maeneo maalamu wafanye biashara,huku tumeshindwa kuwawekea miundo mbinu viwanja vya wazi open market vishauzwa vyote.Usifiche aibu yako Kwa mgeni I hali unakufa njaa acha waje ili waone tofauti yao na third world,cha msingi ni kuwarasimisha na kuwatoza kozi labda 500 Kwa siku na kuwawekea Sheria ya usafi ,pia watafutie maeneo jirani na stand wajengewe wapangishwe ili jiji lipate mapato na wao wapate riziki.Mfano Ile stand ya Gerezani ukijenga frem ndani na nje zinatoka Jumla ya frem 2000 Kwa hela ndogo laki Mbili Kwa mwezi hapo jiji litapata zaid ya milioni 400 Kwa mwezi,Kwa mwaka ni bilioni 5 kwa gerezani tu ujaja mnazi mmoja yote pembeni mwa ukuta,kivukoni kuanzia azam marine had ferry,ukuta wa shule ya uhuru ,kidogo chekundu, nk panadizainiwa vizuri kimvuto.jiji litapata zaid ya bilioni moja na nusu kwa mweziambayo itaongeza mapato ya jiji.Hapo utakuwa umesaidia vijana kupata sehemu ya kufanya biashara na jiji kupata mapato.Tuwatumie machinga Kwa faida.
Kila kitu ndugu kinakuwa na utaratibu wake na ndio hapo ustaarabu unakoanzia!! Na pia lazima kuwe na planing!! Mfanyabiashara mdogo hategemewi kuwa mdogo forever!! Pia kuna kiasi cha income watu wanaruhusiwa kutokulipa kodi!! Ila kwa ustawi wa taifa lolote lazima kila anaejipatia kipato lazima achangie maendeleo ya Taifa lake, Hata iwe ni kidogo kiasi gani! Kwa hayo machache ningependa kusema kama taifa hatujapungukiwa maeneo kiasi cha kuwabananisha wafanya biashara kila mahali kulingana na mawazo yako!! Mheshimiwa rais anasemaga watafutie maeneo rafiki! Ila sijaona kiongozi yoyote anahangaika kuwatafutia maeneo? Tatizo liko wapi? Kupanga siku zote ni kuchagua, Kwa nini tusichukue baadhi ya maeneo katikati ya mji na hawa vijana wakapewa hilo eneo @" Ila kwa kulipia Kodi kiasi fulani ili serekali nayo ipate mapato!! Hii dhana ya kutukaba mtaani haina mashiko!! Unakuta mtu na kimeza chake cha karanga amezuia njia ya waenda kwa miguu, Ukipita barabarani unagongwa na daladala na bodoboda hii sio sawa!!
 
Kumbe UKUTA ulimyumbisha jamaa hivi?
Mi nilikuwa naiuliza, kuna kipindi wamachinga walikuwa wanatimuliwa maeneo haya:
1.K/Koo gerezani kwenye kituo cha magari ya mwendokasi
2. Ubungo darajani hadi mataa, wakahamishiwa barabara ya kuingia stand mawasiliano.
3. Mbezi luis barabara ya stand ya zamani (kushoto) unapoekekea stand mpya.
Baada ya muda nikaona business as usual.

Sijui atalegeza mangapi kwa hofu ya UKUTA?
Ipo siku atatangaza ajira mpya na kuwapandishia wafanyakazi madaraja na mishahara yao UKUTA ukipamba moto tena.

Kwani kurejesha machinga na Bodaboda si sera ya UKAWA
Nyie Bavocha aisee haya hamjitambui,mnaburuzwa tuuu,na mnaugonjwa mbaya sana wa kupoteza kumbukumbu,na ndio sifa kubwa ya Nyumbu
 
Makonda alitaka kuwaondoa machinga lakini mara tukaona kimya mpaka leo. Makonda alijenga hoja kuwa hao machinga wametafsiri vibaya kauli ya rais. Sasa sijui alionywa au vipi
 
Acha ubinafsi wwe maadamu u kula kulala acha vijana wapate riziki ikifika jion wamechoka na Kazi na hela ya kula wanayo hivo hawatupigi roba kuliko wakikaa vijiweni Bila shughuli.Kila sehemu duniani kuna machinga waliotengewa maeneo maalamu wafanye biashara,huku tumeshindwa kuwawekea miundo mbinu viwanja vya wazi open market vishauzwa vyote.Usifiche aibu yako Kwa mgeni I hali unakufa njaa acha waje ili waone tofauti yao na third world,cha msingi ni kuwarasimisha na kuwatoza kozi labda 500 Kwa siku na kuwawekea Sheria ya usafi ,pia watafutie maeneo jirani na stand wajengewe wapangishwe ili jiji lipate mapato na wao wapate riziki.Mfano Ile stand ya Gerezani ukijenga frem ndani na nje zinatoka Jumla ya frem 2000 Kwa hela ndogo laki Mbili Kwa mwezi hapo jiji litapata zaid ya milioni 400 Kwa mwezi,Kwa mwaka ni bilioni 5 kwa gerezani tu ujaja mnazi mmoja yote pembeni mwa ukuta,kivukoni kuanzia azam marine had ferry,ukuta wa shule ya uhuru ,kidogo chekundu, nk panadizainiwa vizuri kimvuto.jiji litapata zaid ya bilioni moja na nusu kwa mweziambayo itaongeza mapato ya jiji.Hapo utakuwa umesaidia vijana kupata sehemu ya kufanya biashara na jiji kupata mapato.Tuwatumie machinga Kwa faida.
Kuna siku hao machinga wataziba njia yako kwa kupanga bidhaa zao au ile njia upitayo kwenda kutafuta riziki ndipo utajua kuwa mpangalio ktk mji ni muhimu au sio muhimu/ubinfsi kama ulivyosema.
 
Kwani kurejesha machinga na Bodaboda si sera ya UKAWA
Nyie Bavocha aisee haya hamjitambui,mnaburuzwa tuuu,na mnaugonjwa mbaya sana wa kupoteza kumbukumbu,na ndio sifa kubwa ya Nyumbu
Kwa hiyo CCM inatekeleza sera za UKAWA baada ya kujengewa UKUTA. Hata hivyo jifunze kufikirio nje ya box. Sio kila anayeipibinga CCM ni Bavicha. Fisi mzee we.
 
Ok. Kuna uzi umeanzishwa huko kuwa Makonda ameamua kuwaondoa. Lakini ni je ana baraka za MKUU aliyewaruhusu machinga kujiachia watavyo!!?
 
Back
Top Bottom