Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Je umeshawahi kujiuliza ni kwa nini wanawake ndiyo wanao lalamika sana kuhusu ugumu au matatizo ya ndoa kuliko wanaume? Inawezekana ni kwa sababu wanawake ni wakosoaji na wanaotaka zaidi kwenye uhusiano kuliko wanaume, wakati wanaume ni wagumu kutoa?
Hakuna anayeweza kusema hasa ni kwa nini wanawake ndiyo wanaolalamika na pengine hata kuomba talaka katika ndoa ukilinganisha na wanaume. Lakini kwa kuangalia sababu kuu ambayo mara nyingi ndizo zenye kutajwa sana kama chanzo cha kuvunjika kwa ndoa tunaweza kupata "ati-ati" ya jambo lenyewe.
Kabla ya ndoa wanandoa huwa na ndoto tamutamu ambazo siyo rahisi katika ndoa. Kwa kuwa tuna hizi ndoto tamu kuhusu ndoa tunapokuja ingia kwenye ndoa na kugundua kwamba tulichokifikiri hakipo ndipo tunapoanza kuvunjika moyo na kujiuliza kwamba ndoa ina maana. Kwa kawaida tunachotarajia kukipata kabla ya ndoa, tunapoingia kwenye ndoa hatukipati na hili huvuruga kila kitu.
Inaonekana kama matarajio ya wanaume huwa siyo makubwa sana kama yale ya wanawake kabla ya ndoa. Huenda hili huchangia katika kufanya wanaume wasishangazwe sana na kile wanachopambana nacho baada ya ndoa. Inawezekana pia ni kwa sababu wanaume wameshika "mpini" kwenye masuala mengi ya kiuhusiano wakati wanawake wameshika kwenye "makali".
Kwenye ndoa tatizo la fedha hukera sana. Kila ndoa ina tatizo linalo husiana na fedha au kipato. Ama hakuna fedha za kutosha au kuna fedha nyingi zinazo sababisha kisirani cha aina moja au nyingine. Kama ilivyo kwa matarajio suala la fedha au kipato pia lina sura ileile ya mwanamke kushika "makali" na mwanamume kushika "mpini". Mwanamke hajaweza kumiliki au kumilikishwa kipato na hili humfanya kuwa mwathirika wa migogoro yote ya kifedha au kipato katika ndoa.
Inabidi wanandoa kujua kwamba ndoa yao haiunganishwi kwa fedha na wala kuwa au kutokuwa na fedha hakuna maana ya kuwa ya furaha au kukosa furaha. Wanachotakiwa kukijua wanandoa ni kwamba wao wameoana ili kuunda familia kwa njia ambayo kipato hakitakuwa na nafasi ya kuwaathiri. Inabidi wajue kwamba hawakuoa wala kuolewa na kipato bali wapenzi wao na kuwepo kwa fedha hakuwezi kubadili mpenzi kuwa "mbaya" au "mzuri". Kushindwa kuelewa tofauti iliyopo kati ya upendo na kipato kunaweza kuwa chanzo cha mgogoro katika ndoa yoyote.
Mwanaume anaweza kudhani kuacha shilingi laki moja nyumbani kila siku kunatosha kuimarisha uhusiano. Ndiyo maana wanaume wengi huwa wanasema "nampa kila kitu lakini wapi…." Hiyo "kila kitu" kwao ina maana ya fedha na siyo kauli na kusikiliza au kujali. Katika hali kama hii mwanamke ndiye anayeshika kwenye "makali" wakati mwanaume ameshika kwenye "mpini".
Matatizo ya ndugu au wazazi kuingilia ndoa ni suala lingine linalotajwa sana katika kuvunjika kwa ndoa nyingi. Bila shaka wengi wetu tunajua kwamba mila na desturi zetu (ni potofu, hata hivyo) ndoa inakuwa ni ya ndugu na wazazi pia, siyo wanandoa peke yao. Lakini kwa bahati mbaya sana katika ndoa nyingi ndugu wa mwanaume ndiyo ambao huingilia ndoa kwa kuwasakama wake katika ndoa hizo wanaume wengi hujikuta wakiwaunga mkono wazazi au ndugu zao dhidi ya wake zao.
Hakuna anayeweza kusema hasa ni kwa nini wanawake ndiyo wanaolalamika na pengine hata kuomba talaka katika ndoa ukilinganisha na wanaume. Lakini kwa kuangalia sababu kuu ambayo mara nyingi ndizo zenye kutajwa sana kama chanzo cha kuvunjika kwa ndoa tunaweza kupata "ati-ati" ya jambo lenyewe.
Kabla ya ndoa wanandoa huwa na ndoto tamutamu ambazo siyo rahisi katika ndoa. Kwa kuwa tuna hizi ndoto tamu kuhusu ndoa tunapokuja ingia kwenye ndoa na kugundua kwamba tulichokifikiri hakipo ndipo tunapoanza kuvunjika moyo na kujiuliza kwamba ndoa ina maana. Kwa kawaida tunachotarajia kukipata kabla ya ndoa, tunapoingia kwenye ndoa hatukipati na hili huvuruga kila kitu.
Inaonekana kama matarajio ya wanaume huwa siyo makubwa sana kama yale ya wanawake kabla ya ndoa. Huenda hili huchangia katika kufanya wanaume wasishangazwe sana na kile wanachopambana nacho baada ya ndoa. Inawezekana pia ni kwa sababu wanaume wameshika "mpini" kwenye masuala mengi ya kiuhusiano wakati wanawake wameshika kwenye "makali".
Kwenye ndoa tatizo la fedha hukera sana. Kila ndoa ina tatizo linalo husiana na fedha au kipato. Ama hakuna fedha za kutosha au kuna fedha nyingi zinazo sababisha kisirani cha aina moja au nyingine. Kama ilivyo kwa matarajio suala la fedha au kipato pia lina sura ileile ya mwanamke kushika "makali" na mwanamume kushika "mpini". Mwanamke hajaweza kumiliki au kumilikishwa kipato na hili humfanya kuwa mwathirika wa migogoro yote ya kifedha au kipato katika ndoa.
Inabidi wanandoa kujua kwamba ndoa yao haiunganishwi kwa fedha na wala kuwa au kutokuwa na fedha hakuna maana ya kuwa ya furaha au kukosa furaha. Wanachotakiwa kukijua wanandoa ni kwamba wao wameoana ili kuunda familia kwa njia ambayo kipato hakitakuwa na nafasi ya kuwaathiri. Inabidi wajue kwamba hawakuoa wala kuolewa na kipato bali wapenzi wao na kuwepo kwa fedha hakuwezi kubadili mpenzi kuwa "mbaya" au "mzuri". Kushindwa kuelewa tofauti iliyopo kati ya upendo na kipato kunaweza kuwa chanzo cha mgogoro katika ndoa yoyote.
Mwanaume anaweza kudhani kuacha shilingi laki moja nyumbani kila siku kunatosha kuimarisha uhusiano. Ndiyo maana wanaume wengi huwa wanasema "nampa kila kitu lakini wapi…." Hiyo "kila kitu" kwao ina maana ya fedha na siyo kauli na kusikiliza au kujali. Katika hali kama hii mwanamke ndiye anayeshika kwenye "makali" wakati mwanaume ameshika kwenye "mpini".
Matatizo ya ndugu au wazazi kuingilia ndoa ni suala lingine linalotajwa sana katika kuvunjika kwa ndoa nyingi. Bila shaka wengi wetu tunajua kwamba mila na desturi zetu (ni potofu, hata hivyo) ndoa inakuwa ni ya ndugu na wazazi pia, siyo wanandoa peke yao. Lakini kwa bahati mbaya sana katika ndoa nyingi ndugu wa mwanaume ndiyo ambao huingilia ndoa kwa kuwasakama wake katika ndoa hizo wanaume wengi hujikuta wakiwaunga mkono wazazi au ndugu zao dhidi ya wake zao.