Hivi ni harali kwa mbunge kuongea na simu bungeni huku kikao kikiendelea

Ptz

JF-Expert Member
Aug 23, 2011
541
384
Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sana vikao vya bunge letu la Tanzania live kwa kupitia tv. Nimeshuhudia baadhi ya wabunge na mawaziri wakiongea na simu bungeni huku kikao cha bunge likiendelea, ni mara kadhaa nimemshuhudia Mkuchika akiongea na simu na gazeti la mwanachi lilishamtoa kwenye front page picha yake huku akiongea na simu.

Leo hii nimemshudia Davide Kafulia (mbunge Kigoma Kusini) akiongea na simu huku mzee Cheyo akitoa mchango wake, zaidi ya yote punde baada ya mzee Cheyo(Mbunge wa Bariadi) kumalizia mchango wake, kuna Mbunge wa Mbalali mh Kilufi akichangia kuna mbunge mmoja alikuwa kaketi kushoto kwake ghafla msg iliingia kwenye simu yake, niliisikia msg kwa ringtone ya Nokia, mbunge huyo alichukua simu na kuisoma msg na mara tu baada ya kusoma alionesha tabasamu zito (Source TBC leo saa 11 hadi moja jioni). Kwangu mimi nauita upumbavu. Nimekuwa pia nikifuatilia bunge la Kenya na Uganda, sijawahiona upumbavu huu.

Ni bunge hili hili kuna mbunge mmoja alishathubutu kughushi hati na saini ya waziri mkuu Mizengo Pinda na kuachwa bila hatua yoyote ile. Je, ni harali kwa tabia kufanywa na hawa watu tunawaita waheshimiwa kuzitumia simu zao wakati wa kikao kikiendelea katika jengo tunaloliita tukufu kwani hata huku uraiani kuna vikao tumekuwa tukivifanya ni kulazimika kuzizima au kutoingia na simu kabisa,

Kwa mifano ya mabunge ya wenzetu niliyoitaja mfano bunge la Kenya naona kwa Yule spika"sir Kenneth Marende, naibu wake "sir Farah Macalin" upumbavu ninaouona huukwa bunge letu Tanzania si rahisi kuuvumilia kwa bunge la Kenya, nilishashudia waziri akitolewa nje na kupigwa Ban ya vikao vitatu kwa kutojibu swali ipasavyo kwa ushahidi nilionao Bunge la Kenya ni Bunge la Kenya kweli "It's a really Kenyans Parliament" ni vigumu kumjua hata mpinzani au mtawala ni ninani! Nawasilisha.
 
Haya tumeyataka wenyewe kama hatutaki mambo ya ovyo basi ikatae ccm kwa kuichagua CDM
 
Wabunge na viongozi wetu wamejaa mzaha katika utendaji wao. Mtu makini anayetambua umuhimu wake bungeni hawezi kutumia simu. Ni aibu yao na yetu wapiga kura tunaoshindwa kuwawajibisha wabunge wetu. Upuuzi unaofanyika Tanzania katika uongozi haupo mahali popote DUNIANI. Hapa hawara anahongwa cheo na wote tunaishia kuchangia kwa kodi zetu. Mhalifu anapata uteuzi wa Raisi. Ni ajabu na kweli.
 
nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sana vikao vya bunge letu la tanzania live kwa kupitia tv. Nimeshuhudia baadhi ya wabunge na mawaziri wakiongea na simu bungeni huku kikao cha bunge likiendelea, ni mara kadhaa nimemshuhudia mkuchika akiongea na simu na gazeti la mwanachi lilishamtoa kwenye front page picha yake huku akiongea na simu.

Leo hii nimemshudia davide kafulia (mbunge kigoma kusini) akiongea na simu huku mzee cheyo akitoa mchango wake, zaidi ya yote punde baada ya mzee cheyo(mbunge wa bariadi) kumalizia mchango wake, kuna mbunge wa mbalali mh kilufi akichangia kuna mbunge mmoja alikuwa kaketi kushoto kwake ghafla msg iliingia kwenye simu yake, niliisikia msg kwa ringtone ya nokia, mbunge huyo alichukua simu na kuisoma msg na mara tu baada ya kusoma alionesha tabasamu zito (source tbc leo saa 11 hadi moja jioni). Kwangu mimi nauita upumbavu. Nimekuwa pia nikifuatilia bunge la kenya na uganda, sijawahiona upumbavu huu.

Ni bunge hili hili kuna mbunge mmoja alishathubutu kughushi hati na saini ya waziri mkuu mizengo pinda na kuachwa bila hatua yoyote ile. Je, ni harali kwa tabia kufanywa na hawa watu tunawaita waheshimiwa kuzitumia simu zao wakati wa kikao kikiendelea katika jengo tunaloliita tukufu kwani hata huku uraiani kuna vikao tumekuwa tukivifanya ni kulazimika kuzizima au kutoingia na simu kabisa,

kwa mifano ya mabunge ya wenzetu niliyoitaja mfano bunge la kenya naona kwa yule spika"sir kenneth marende, naibu wake "sir farah macalin" upumbavu ninaouona huukwa bunge letu tanzania si rahisi kuuvumilia kwa bunge la kenya, nilishashudia waziri akitolewa nje na kupigwa ban ya vikao vitatu kwa kutojibu swali ipasavyo kwa ushahidi nilionao bunge la kenya ni bunge la kenya kweli "it's a really kenyans parliament" ni vigumu kumjua hata mpinzani au mtawala ni ninani! Nawasilisha.

halali
 
Haya tumeyataka wenyewe kama hatutaki mambo ya ovyo basi ikatae ccm kwa kuichagua CDM

naona hujaelewa vizuri hoja ya mtoa mada. Amefafanua vizuri na kutoa mfano hata wa David kafulila( ni CCM?!). Hapa hakuna hoja ya CCM wala CDM.
 
Hapa mi sioni cha ajabu, hata wasipoongea na cm huwa wanapiga stori wenyewe kwa wenyewe huku hoja ikiendelea. na stori zinanoga hadi mtu anahama kiti chake anasogea kwa mwingine. wengine wanapiga usingizi tu kule mjengoni kipengele muhimu ni wakati wa kuandika majina kwa ajili ya sitting allowance,
 
Back
Top Bottom