Hivi ndivyo tunavyodanganyana kuhusu Ligi Kuu yetu (NBC PL)

BIG Africa

Member
Oct 15, 2022
84
116
"LIGI yetu inaeendelea"."Ligi yetu imepiga hatua".Hizi ni baadhi ya kauli za watu ambao wamekuwa wakijitokeza na kusema hivyo.

Binafsi sidhani.Kwani maendeleo ya ligi kuu huwa yanatazamwa kwa kuangalia vigezo vipi katika timu?.Jibu ni jepesi tu.

Ni viwanja bora vya timu,malipo mazuri ya wachezaji na benchi la ufundi ambayo hutokana na uwekezaji mzuri ndani ya klabu na kadhalika.Sasa tujiulize swali.

Timu zetu zina miundombinu bora ya soka?.Jibu ni hapana.Inashangaza kuona hata timu kubwa kama Simba na Yanga na zenyewe hazina viwanja vyao vya mechi,achana na viwanja vya mazoezi.

Azam FC na Kagera Sugar tu ndiyo timu zenye viwanja vyenye hadhi ya Ligi Kuu.Uwanja wa Benjamin Mkapa sio wa Simba wala Yanga.Ni wa serikali.

Nchi hii mambo mengi sana kwenye soka bado hayajakaa sawa tofauti na watu wanavyodanganyana.

Nilichokuja kugundua ni kwamba watu wengi wanaitazama Ligi Kuu yetu kwa kuangalia timu tatu tu.Simba,Yanga,na Azam FC.Basi.Bado kuna pengo kubwa sana kati ya timu zetu ndogo na timu zetu kubwa.
 
Upo sahihi Mkuu!
Ni kitu vitu viwili tu ambavyo mimi naona tumepiga hatua:
Kwanza hakuna malalamiko ya wachezaji kutolipwa mishahara kama zamani.

Pili mechi zetu Sasa zinarushwa live.
 
Hatua ni hatua tu hata km ni moja kwa sababu zifuatazo:-
1.Kumeongezeka uwekezaji wa fedha. Leo hii kila timu ya ligi kuu inapata kiasi cha takribani mil.500 kwa mwaka. Changanya na zawadi ya bingwa mil 500 na zawadi zingine.Huu si uwekezaji mdogo.

2. Kuboreshwa kwa baadhi ya viwanja. Leo hii viwanja vya Kaitaba,Namungo,Azam Complex,na Dodoma vimewekwa taa na pitch za bandia. Hili si hatua ya kubeza.

3. Kuongezeka kwa wadhamini km sport pesa,NBC n.k

4. Kuongezeka kwa idadi ya timu toka 2 hadi 4 kwenye mashindano ya kimataifa.

Kwa level za nchi zetu ukilinganisha na wenzetu wanaotuzunguka,sisi tumepiga hatua.
 
Unajua maana ya Kuendelea au kupiga hatua ??

Unafukaje huko bila kupiga hatua?

Punguza kuwa 100percentist , punguza userious ktk maisha!!..
 
Nakushauri ukipata muda siku hebu angalia azam tv 3 mchana huwa wanarusha marudio ya games za zamani hivyo viwanja uvione.

Sina imani kama timu za simba na yanga kama kuna siku zinatakuwa na uwanja wake recently, maana mkapa stadium ni mtaji wa watu ule.
 
Kaangalie ligi ya Ghana au Nigeria kuanzja viwanja na malipo ya wachezaji ndio utajua kwa kiasi gani tumepiga hatua,Nigeria mchezaji anayelipwa zaidi analipwa shilling Millioni 6 dau ambalo wachezaji wetu walilipwa 2006, kacheki sasa na hivyo viwanja Ghana au nigeria vinavyochezewa ligi kuu utacheka ni vipara tulu, heri yetu sisi tunaojaribu kuvifungia fungua vile vibovu
 
Kagera sugar wamejenga lini uwanja? Ila nakubaliana na wewe ligi yetu sio kubwa sanasana wanapaishwa na mafanikio ya Simba kimataifa
 
Kuna timu kubwa huko Ulaya hazina viwanja zinatumia viwanja vya Manispaa na zishashinda hadi UEFA champions league halafu unashangaa Simba na Yanga kukosa viwanja?
 
Nami nimeshangaa kua kagera ana uwanja mzuri haha upo wapi??unaitwaje??ameshacheza mechi yeyote??
Ule uwanja wa kaitaba unaotumiwa na kagera sugar ni wa manispaa ya Bukoba...sio wa kagera wala CCM ndo maana ulijengwa vile...


Ila kagera sugar wana uwanja wao wa mazoezi huko kiwandani kwao misenyi
 
"LIGI yetu inaeendelea"."Ligi yetu imepiga hatua".Hizi ni baadhi ya kauli za watu ambao wamekuwa wakijitokeza na kusema hivyo.

Binafsi sidhani.Kwani maendeleo ya ligi kuu huwa yanatazamwa kwa kuangalia vigezo vipi katika timu?.Jibu ni jepesi tu.

Ni viwanja bora vya timu,malipo mazuri ya wachezaji na benchi la ufundi ambayo hutokana na uwekezaji mzuri ndani ya klabu na kadhalika.Sasa tujiulize swali.

Timu zetu zina miundombinu bora ya soka?.Jibu ni hapana.Inashangaza kuona hata timu kubwa kama Simba na Yanga na zenyewe hazina viwanja vyao vya mechi,achana na viwanja vya mazoezi.

Azam FC na Kagera Sugar tu ndiyo timu zenye viwanja vyenye hadhi ya Ligi Kuu.Uwanja wa Benjamin Mkapa sio wa Simba wala Yanga.Ni wa serikali.

Nchi hii mambo mengi sana kwenye soka bado hayajakaa sawa tofauti na watu wanavyodanganyana.

Nilichokuja kugundua ni kwamba watu wengi wanaitazama Ligi Kuu yetu kwa kuangalia timu tatu tu.Simba,Yanga,na Azam FC.Basi.Bado kuna pengo kubwa sana kati ya timu zetu ndogo na timu zetu kubwa.
Kaitaba sio Uwanja unaomilikiwa na Kagera Sugar
 
Back
Top Bottom