TUKUTUKU
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 11,765
- 4,033
Anachinjwa kama wanyama wengine!Samahani kidogo wadau, hivi KITIMOTO anachinjwa au anauawa?
Anachinjwa kama wanyama wengine!Samahani kidogo wadau, hivi KITIMOTO anachinjwa au anauawa?
Yeyote anaweza chinja tu kwetu sisi wakristo hatuna shida hata kama kanyongwa sisi twala. You know what we do initially chakula ni cha mpishi baada ya mimi kupewa na kibadili na kuwa chakula cha Mungu wa Israeli, Ibrahim, Isaka, n.k. Ukiamin tu hata kama kina sumu ya kufisha hakitakudhuru. Hivyo mimi nawashauri wakristo whatever atakayechinja kikubwa ni wewe kumshirikisha Mungu wako ili akipe baraka na nguvu ili kikupe afya. Tuachane na urgument za kidini hili halitatusaidia zaidi utakuta wachinjaji wanakula bila kufuata kanuni za afya na mwisho wanakufa na hypertension. Tuwe wavumilivu kama kristo alivyovumilia mpaka kufa msalabani.
Hili ndilo jibu haswaa!!
mkuu nadhani umenielewa. Tangu kuasisiwa kwa udini na jk sasa hivi watu wamefikia kuhoji kila jambo la kijamii linalofanywa na upande mmoja kwa kwa nini na wengine hawahusishwi? Ndo maana nimeuliza wanasheria, wanajamii na watu wa mifugo. Vinginevyo ningeuliza tu kwa ni waislamu ndo wachinjaji? Au ningesema nachukia nyama inayochinjwa na waislamu!
Sasa kama mahusiano yalikuwa mazuri kiasi cha kuita jirani yako akuchinjie kuku au mbuzi ili mle pamoja imekuwaje huu udini wa kubaguana,kuchomeana nyumba za ibada na kashfa? Nani kayaleta hayo ghafla namna hii? Ndugu wanapogombana haraka sana wanamtafuta mchochezi wao na kumu eliminate.Waislam na Wakristo ni ndugu toka zamani wakiishi kwa kushirikiana (hata kuchinja kuku)hivyo ni vema sasa hivi wakamjua ni nani anayewagombanisha?kwa sababu mwanao yu mahututi na mwenye usafiri jirani yako mmegombana kwa udini jee yule aliyechochea udini huo mtamuona?Wakristo walikuwa wanafuata utaratibu huu kwa namna ileile ya kuishi vizuri na wenzao waislamu si unajua tena wakristo hawana hiyana. Vile vitu ambavyo wanakula na wenzao hawakupenda kuwakwaza waliwapelekea waislamu iliwachinje na ili waweze kula wote. Lakini Nguruwe huwa wanachinja wenyewe kwani wenzetu kidinihuwa hawali.
kwao ni haramu kula mnyama aliyechinjwa na mkristo...cha kushangaza wakristo wenyewe hawana tatizo kula mnyama aliyechinjwa kwa kuelekezwa kibla...kuna kitu cha kujifunza hapa...Hakuna sehemu kwe kolani kwamba mkristu akichinja basi mslam asile.
Mwana mpotevu kwe baibo hakuchinjiwa ng'ombe na mslam.
kwa hiyo ndo unataka kusema,Viongozi wa dini wachinje kitimoto pia au?Samahani kidogo wadau, hivi KITIMOTO anachinjwa au anauawa?
Tunakula nyati, anachinjwa? Ili uweze kumchinja inabidi umpige risasi ndipo uwahi kumchinja na wakati mwingine unamkuta amekufa. Nguruwe inabidi umpoteze fahamu ili uweze kumchinja. Chakula kikiandaliwa na mwislamu kuna taratibu inabidi zifuatwe za uchinjaji na mtu yeyote anakula. Mkristo anapochinja kuna utaratibu anaufuata na mtu yeyote anaruhusiwa kula, ila mkristo kabla ya kula kitu anatakiwa abariki chakula pale najisi yeyote inatoka hata kwa mwislam akibariki anakuwa hana tatizo, ila tatizo ni mafundisho ya viongozi wa dini wanashindwa kutoa elimu ya kutosha kwa waumini wao na baadhi yao ni tatizo wanahubiri chuki na bora viongozi wetu wa dini wakawa na elimu za dini na zakijamii kuliko kuwa na kiongozi shule ndogo anaongoza watu wenye uelewa mkubwa halafu anafanya mambo ya kuwagawa wa Tz.
Anachinjwa Mkuu au nyundo akianguka na kulegea kisu kinamalizia! Na kule kwetu huwa kazi hiyo tunawapa ndugu zetu ktk Adam kwa sababu wanapenda kuchicha, na ili Tusiwakwaze, na ni kama nguruwe wa shughuli tuwe pamoja! Manake huwa swali lao la kwanza kabla ya kula, "Kachinja nani?"Samahani kidogo wadau, hivi KITIMOTO anachinjwa au anauawa?
Wacha zako hizo za kuleta!Toa ushahidi wa ayat ndani ya Qurani inayo zuia Mkristo asichinje!Si useme tu kuwa mna uchu wa nyama kwa sana!uislamu ni dini yenye utaratibu kwa kila jambo. Hivyo kwa dini ambazo hazina utaratibu, mtatusamehe. Simply hatuli nyama zilizo chinjwa na wasio kua waislamu kwa sababu kwetu nyama hizo ni vibudu kwa kua zimechinjwa bila kuomba idhini ya muumba.
....usungilo....Si kweli kuwa kwa waislamu anayeruhusiwa kuchinja ni shehe tu. Ninachofahamu kila muislamu mwanaume anayefahamu utaratibu wa kuchinjia kuchinja. Nikweli kuchinja kunaambatana na maombi/sala kwa ajili ya yule mnyama anayechinjwa. Katika uislamu kuna hata exception kuwa inapotokea kwenye mazingira ambayo hakuna muislamu mwanaume anayejua taratibu za kuchinja lakini kuna mwanamke anayefahamu taratibu za kuchinja basi anaweza kufanya hivyo. Hili ni suala la kiimani zaidi kwani mapokeo yanasema hivyo. Ulichouliza kinaweza ku-apply kweli kwenye jamii isiyokuwa na waislamu ambako bado watu wanachinja kwa utaratibu waliojiwekea. So kutegemea padri, askofu au mchungaji kuchinja mnyama kisha hiyo nyama akiliwa na waumini wa dini nyingine kwa mtazamo wangu nadhani itakuwa ngumu na hasa kwa nchi kama Tz ambayo nijuavyo si ya kidini kama zilivyo zingine ambazo hata katiba inaeleza wazi kuwa nchi husika inafata imani ya dini fulani.