Hivi namba ya simu ni jambo la siri?

Makamee

JF-Expert Member
Nov 29, 2013
2,029
1,191
Nijuavyo mimi lengo la simu ni mawasiano,Inakuaje kwamba namba ya simu ionekane ni kitu cha siri sana kiasi kwamba watu wengi hukataa kuweka wazi au kupewa mtu mwengine bila ridhaa yake?
Kwani tatizo ni nini?
 
Kimsingi namba ya simu hasa za wale public figures zinatakiwa ziwe wazi na zitambulike na kila mtu ili pengine kuweza kupata taarifa kwa haraka toka kwa watu wao.
Mf:RPC,DC,Mganga mkuu wilaya/mkoa n.k
 
Nijuavyo mimi lengo la simu ni mawasiano,Inakuaje kwamba namba ya simu ionekane ni kitu cha siri sana kiasi kwamba watu wengi hukataa kuweka wazi au kupewa mtu mwengine bila ridhaa yake?
Kwani tatizo ni nini?

Kwa Tuliooa/olewa Namba Zetu Ni Siri Kwa Sababu Ya Usalama Wetu Kwenye Ndoa.
 
Mkuu Makamee , salama kwanza? umenyimwa namba nini mkuu?? hahaaa, natania tu ....

Sio kitu cha siri ila ni kitu BINAFSI......Tofautisha BINAFSI na SIRI. Ukiifanya namba yako ya simu iwe ya PUBLIC utajuta. watu wana tabia tofaut, wengine hawana malengo mazuri na wengine ni wasumbufu wasio na chembe ya ustaarabu. Ndio maana huwezi kutoa namba hovyo hovyo kwa mtu yoyote tu....
 
Last edited by a moderator:
Tatizo hapa linakuja ni ktk matumizi mabaya ya namba za simu baada ya kuwa nayo,wengine hutukana,hutishia n.k
 
upigiwe! simu au utumiwe text na watu usio wajua wakutishie maisha ndipo utakao elewa.

Jiulize ni vyema kila mtu ajue unapoishi??
 
Na vipi unapokuwa na namba ya simu ya mtu wakati yeye hajui kama unayo namba yake, siku unawasiliana naye kwa mara ya kwanza swali la kwanza ni; "nani kakupa namba yangu?". Silipendi kabisa hili swali.
 
upigiwe! simu au utumiwe text na watu usio wajua wakutishie maisha ndipo utakao elewa.

Jiulize ni vyema kila mtu ajue unapoishi??

Na wewe pata tatizo kama la mtoto kuumwa halafu omba namba ya doctor uambiwe namba yake hataki apewe mtu ndo utajua.
 
tatizo wengi ni wasumbufu.. Mfano mtu anakupigia unamuuliza wewe nani? Anaanza blah blah..
 
Jinsi ilivyo namba za simu ulizo nazo asilimia 98 ni wale watu unaoendana nao ktk hali yako kimaisha.
Mifano:
1.anaetumia jiko la umeme hawezi kua na namba ya muuza mkaa.
2.Mvuvi hawezi kua na namba ya mchimba madini.
Labda wawe wana undugu.
 
Mkuu Makamee , salama kwanza? umenyimwa namba nini mkuu?? hahaaa, natania tu ....

Sio kitu cha siri ila ni kitu BINAFSI......Tofautisha BINAFSI na SIRI. Ukiifanya namba yako ya simu iwe ya PUBLIC utajuta. watu wana tabia tofaut, wengine hawana malengo mazuri na wengine ni wasumbufu wasio na chembe ya ustaarabu. Ndio maana huwezi kutoa namba hovyo hovyo kwa mtu yoyote tu....

True dat mutombo
 
Last edited by a moderator:
Hebu km si siri weka number yako haapa

Nijibu maswali yafuatayo:
hapo mtaani kwako unapoishi
je una namba ya balozi wako? Ya jirani yako? Ya mchungaji/shehe wako? Doctor yoyote? Ya fundi yoyote?
NAMBA ya simu si kitu kinachotakiwa kiwe siri matumizi mabaya ndio tatizo.
 
Nijibu maswali yafuatayo:
hapo mtaani kwako unapoishi
je una namba ya balozi wako? Ya jirani yako? Ya mchungaji/shehe wako? Doctor yoyote? Ya fundi yoyote?
NAMBA ya simu si kitu kinachotakiwa kiwe siri matumizi mabaya ndio tatizo.

Hao uliowataja ni public figures mbona hujauliza kama ana namba ya changudoa wa sinza au mpiga debe wa ubungo?
 
Wengine wakishapata namba ya simu hawakawii kuanza kutuma msg tafadhali niongezee salio au kupiga wakati hana jambo lolote la maana
 
Back
Top Bottom