Unauliza babu zetu ambao hawakuwa wakristo au waislam kiama watakuwa wapi.Wakristo na Waislam hata sasa hawafiki thelusi ya watu wa dunia.Wachina , wahindu, wajapani, wayahudi na wengine wasio wakristo au waislam in zaidi ya nusu ya population ya dunia na Mungu anawapenda sana ndio maana wengi in matajiri.Dini zao zilikuwepo miaka mingi sana kabla ya ukristo na uislam.Wako wanao toa hoja kuwa MTU atahukumiwa kwa matendo yake na si dini, kila watu walipewa dini yao kama mwongozo ili waishi vizuri na kuwafikisha kwa mola hivyo mababu zetu watahukumiwa kwa kufuata miongozo au tuite dini walizopewa wakati huo.Wanasema hakuna adhabu ya milele kwasababu hatujaishi milele, Mungu sio katili yaani kama umeishi dunani miaka 70 na ulikuwa unafanya maovu kila sekunde utaadhibiwa kwa uzito wa madhambi yako kisha unaungana na wenzako kwa mola. Hatimae wote tutakuwa peponi baada ya kutumikia adhabu zetu jehanam