Hivi mwanaume unaanzaje kumlilia mwanamke?

Hivi mwanaume unaanzaje kumlilia mwanamke?

BEHOLD

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
5,057
Reaction score
10,731
Nimekuta lidume lina mlilia mwanamke, tena ni hawala tu. Nimetafakari sana, Dume zima linatoka machozi na makamasi kedekede kisha kuambiwa "its over" du!
Hata huyo mwanamke atakudharau sana tu.

Kuna kitu kimepungua kwa wanaume siku hizi sio bure!
 
We ni ke au me halaf nikupe siri kwa nn wanalia
 
Kumlilia demu ni ulofa wa kiwango cha lami, unless kama ni mbinu ya kufanikisha malengo yako
 
Hakuna cha kufikwa huo ni uzezeta tu!
Huwa tunakuwa na principal na theory nyingi za kujitia ugumu na ungangari kuhusu mapenzi na kupenda lakini tunashindwa kutambua mapenzi ni hisia. Mm namuunga mkono huyo jamaa muache alilie penzi lake na wala sio uzezeta
 
Ukiona mtu mzima analia mbele za watu ujue kuna jambo. Wakati mwingine machozi huwa si kwa sababu ya kulilia penzi, tunalia kwa sababu ya gharama tulizoingia juu yao. Unadate na mwanamke unampangia nyumba nzima unamuwekea kila kitu ndani halafu anakupiga chini hivi kweli wewe utaacha kulia? Unaweza kujikaza kwa kuacha kulia tusiyaone machozi yako, lakini wewe mwenyewe moyoni ukabaki na kilio kikubwa. Haya mapenzi hayana mbabe, usiwacheke wanaolia maana ipo siku yako yaja!
 
Kuna sababu nyingi zinazoweza mfanya mtu alie hasa aliyeachwa.
1. Kulia kunapunguza hasira
2. Kulia kunapunguza uchungu hasa ukifikiri mambo uliyomfanyia na leo anakuona hufai
3. Kulia kunaleta nafuu moyoni, na kutakufanya usonge mbele
4. Kulia kutakufanya ukubali hali ya kuachwa na uendelee na maisha.
na mengine kibaaaaao. Wanaume lieni tu wala sio uzuzu...mnaepusha mengi ikiwa ni pamoja na kuvunja shingo ya mtu au kujiua
 
Huyo kapewa limbwata. Utamliliaje mwanamke wakati wanawake wamejaa kibao. Ahhaaa! Nimekumbuka! Atakuwa Mario anatunzwa kama Kibenteni!
 
Nimekuta lidume lina mlilia mwanamke, tena ni hawala tu. Nimetafakari sana, Dume zima linatoka machozi na makamasi kedekede kisha kuambiwa "its over" du!
Hata huyo mwanamke atakudharau sana tu.

Kuna kitu kimepungua kwa wanaume siku hizi sio bure!


Mambo haya mara nyingi wanayo wanaume wa Dar. Nakumbuka siku Ruge Mutahaba alivyoachwa na Zamaradi alilia huku mikamasi ya hajabu ikimtoka na kujikojolea hadharani mpaka kina Jo Kusaga wakawa wanamletea diapers avae maana alikuwa ananuka mkojo balaa. Watu wakimuuliza dogo vipi, anasema Zama Zama, Ohooooooo, nimekosa nini mie jamani...."
 
Niliwahi sema sitalia kisa mwanamke mwisho wa siku nikalia baada ya kufuta machozi nika move on baada ya mda akanitafuta na misamaha kama yote nikasema NOO
 
Sijisifii ila wakati wa uschana wangu,wanaume wawili kwa nyakati tofauti walishatoa machozi mbele yangu....mie nikisema tuachane wao wanataka tuendelee.

Enzi za Kasie Msomali....

Kweli wakati ukuta.

Kasie Mahaba Matata.
 
Mambo haya mara nyingi wanayo wanaume wa Dar. Nakumbuka siku Ruge Mutahaba alivyoachwa na Zamaradi alilia huku mikamasi ya hajabu ikimtoka na kujikojolea hadharani mpaka kina Jo Kusaga wakawa wanamletea diapers avae maana alikuwa ananuka mkojo balaa. Watu wakimuuliza dogo vipi, anasema Zama Zama, Ohooooooo, nimekosa nini mie jamani...."
😳😳😳
 
Back
Top Bottom