Hivi MKUKUTA umeishia wapi?

Hivi MKUKUTA umeishia wapi?

Domenia

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
462
Reaction score
23
Haya mambo ya kupambana ma umasikini yameishia wapi...Naona wahusika karibia wote sasa wana onekana mafisadi... hii ime kaaje?
 
Haya mambo ya kupambana ma umasikini yameishia wapi...Naona wahusika karibia wote sasa wana onekana mafisadi... hii ime kaaje?


Mkuu, MKUKUTA kama ilivyokuwa kawaida ya nchi yetu hii kitu pamoja na kutumia mabilioni ya pesa imekuwa ni failure ya hali ya juu na ndiyo maana hata sasa hivi haitajwitajwi tena kama ilivyokuwa miaka ya karibuni. Sijui kama kuna lolote litakaloweza kufanyika ili MKUKUTA iwe na mafanikio ya aina yoyote ile.

Poverty Monitoring
 
Nilisikia MKUKUTA alimtemelea jamaa yake MKURABITA na wote kwa pamoja wakaenda vakesheni France na Spania, mpaka sasa hawajarudi.
 
Huyo MKUKUTA mara ya mwisho alionekana ameongozana na Gaddafi. Sasa sina uhakika kama watakuwa wameondoka wote au vipi.
 
huu ni mkakati wa kuondoa utajiri na kuongeza umaskin tanzania,bado unaendelea
 
Kama Rusia wanataka Putin arudi ikulu, basi hata sisi tunaweza kumrudisha mzee Mkapa ikulu ili aje azifufue hizi MKUKUTA na MKURABITA. Ni mawazo tu.
 
Mkukuta na Mkurabita,ulikuwa wimbo wa mzee wa ukweli na uwazi
 
Huyo MKUKUTA mara ya mwisho alionekana ameongozana na Gaddafi. Sasa sina uhakika kama watakuwa wameondoka wote au vipi.

na MKURABITA ALIONEKANA AMEONGOZANA NA NANI MWITA?
 
MKUKUTA + MKURABITA vyote kwa pamoja vimeishia kwenye makaratasi tu, hivi vitu vilikufa hata kabla havijaanza!!!
Kifupi vyote kwa pamoja ni JANGA LA KITAIFA
 
CCM @ work.

Kuna hii ya MKULAFILA -- hii ya mzee cameroon -- ha ha ha - kweli TZ ni pa kujifunzia kunyoa.
 
Dah!! Namkumbuka Mzee Fares Kabuye alipokuwa Mbunge wa TLP ya Mrema Jimbo la kule kwa Magufuli...... Huyu Mzee aliwaponda kishenzi wooote waliopigia debe utumbo huo wa Mkukukukukuta na Mkuraraarraabita na nini sijui.
 
Kwani wale jamaa wa king'oko wanaitwa something REPAO inausu poverty eradication program wapo Rejent estate karibu na kikwete vp havihusiani na mkurabita na mkukuta

1.Mkakati wa kuwanyanganya rasilimali wanyonge na kuwapa matajiri(mkurabita)
2.Mpango wa kuondoa utajiri na kuongeza umasikini tanzania(mkukuta)
3.Tanzania Sasa hAina Fedha(TASAF)
 
Back
Top Bottom