Hivi kweli Watanzania wamekubali maisha haya.

Molembe

JF-Expert Member
Dec 25, 2012
9,821
11,527
Ukienda huko vijijini watanzania wanaishi maisha ya tabu na shida sana, wengi wanaishi kwenye nyumba za tembe huku huduma za kijamii kama barabara, maji na hospitali hakuna, akina mama huko wanatumia masaa mengi sana kutafuta maji na hutembea umbali mrefu kupeleka watoto wao kliniki na hospitalini.

Shule za kata nyingi zimekuwa sehemu ya kukuzia watoto na sio kuwapatia elimu, shule nyingi zina uhaba wa walimu, miundombinu mibovu ikiwemo ukosefu wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia matokeo yake ni asilimia kubwa watoto hawa wanaosoma kwenye mazingira mabovu hufeli na hakuna juhudi zozote za kuwaendeleza.

Ukienda hospitalini dawa hakuna, yaani ukipeleka mgonjwa wako unaweza kufa kwa presha maana huduma ni mbovu watumishi wanafanya kazi kwa mazoea na kila dawa utaandikiwa ukanunue hata glovu za kuzalisha hakuna.

Ukosefu wa ajira ni janga kuu vijana wengi wamejazana mtaani bila kazi, wengi hushinda vijiweni wakibeti lakini serikali haifanyi juhudi zozote kukabiliana na suala hili, wao wanasema wajiajiri lakini hata mazingira ya kujiajiri sio rafiki ikiwemo ukosefu wa mitaji.

Watumishi ambao huwa ndio msaada mkubwa kwa ndugu zao wa vijijini wamebanwa wakabanika, hakuna nyongeza ya mishahara, hakuna kupanda madaraja wala uhamisho lakini vilevile wanahakikiwa kila siku tena wanaenda kwa gharama zao wenyewe na hakuna kurudishiwa. Vilevile kuna watumishi wa umma wamefukuzwa kazi bila kufuata taratibu hata wengine bila kusikilizwa na kuhojiwa na mamlaka za nidhamu zilizopo kwenye utumishi wao.

Uonevu kwa viongozi wa vyama vya kisiasa, ndani ya uongozi huu tumeshuhudia kamata kamata na uonevu wa wazi kabisa kwa viongozi vyama vya siasa na wengine kufungwa kwa hila za kisiasa.

Ukosefu wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ni janga lingine vijana wengi waliohitimu elimu zao wamenyimwa mikopo wapo mtaani wanazurura tu,
Nchi hii kwa sasa hakuna demokrasia, hakuna uhuru wa bunge (mtu mmoja anapanga bajeti) , ni mtu mmoja tu anaetakiwa kusikika, ni yeye tu anaetakiwa kuwa live na ni yeye tu anaepanga kila kitu ndani ya nchi hii.

Hivi kweli Watanzania wenzangu wameridhika na hali hii, tumekaa kimya kabisa haya yakifanyika, tutamlaumu nani huko mbeleni.
 
Umeongea kwa machungu sana mkuu! Yaani ni wengi tunaoumia sema tunayo hasira balaa,
 
Walioamua haya ni wale wanaoruhusu watu wale wale kututawala ndani ya miaka hamsini huku wakitajirika wao na familia zao na sie kuendelea kupauka tu,mi nadhani tumekubaliana na hali hii,maana hata alternative hatuna,wala hatuonekani tukipaza sauti zetu na kufanya jitihada za pamoja kujikwamua katika kifungo hichi
 
Tatizo kubwa kuna zile maiti zinazohisi hakuna maisha bila Lumumba na kijani yake.....tuko hapa tulipo kwa sababu ya misukule ya kijani.
 
Ukienda huko vijijini watanzania wanaishi maisha ya tabu na shida sana, wengi wanaishi kwenye nyumba za tembe huku huduma za kijamii kama barabara, maji na hospitali hakuna, akina mama huko wanatumia masaa mengi sana kutafuta maji na hutembea umbali mrefu kupeleka watoto wao kliniki na hospitalini.

Shule za kata nyingi zimekuwa sehemu ya kukuzia watoto na sio kuwapatia elimu, shule nyingi zina uhaba wa walimu, miundombinu mibovu ikiwemo ukosefu wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia matokeo yake ni asilimia kubwa watoto hawa wanaosoma kwenye mazingira mabovu hufeli na hakuna juhudi zozote za kuwaendeleza.

Ukienda hospitalini dawa hakuna, yaani ukipeleka mgonjwa wako unaweza kufa kwa presha maana huduma ni mbovu watumishi wanafanya kazi kwa mazoea na kila dawa utaandikiwa ukanunue hata glovu za kuzalisha hakuna.

Ukosefu wa ajira ni janga kuu vijana wengi wamejazana mtaani bila kazi, wengi hushinda vijiweni wakibeti lakini serikali haifanyi juhudi zozote kukabiliana na suala hili, wao wanasema wajiajiri lakini hata mazingira ya kujiajiri sio rafiki ikiwemo ukosefu wa mitaji.

Watumishi ambao huwa ndio msaada mkubwa kwa ndugu zao wa vijijini wamebanwa wakabanika, hakuna nyongeza ya mishahara, hakuna kupanda madaraja wala uhamisho lakini vilevile wanahakikiwa kila siku tena wanaenda kwa gharama zao wenyewe na hakuna kurudishiwa. Vilevile kuna watumishi wa umma wamefukuzwa kazi bila kufuata taratibu hata wengine bila kusikilizwa na kuhojiwa na mamlaka za nidhamu zilizopo kwenye utumishi wao.

Uonevu kwa viongozi wa vyama vya kisiasa, ndani ya uongozi huu tumeshuhudia kamata kamata na uonevu wa wazi kabisa kwa viongozi vyama vya siasa na wengine kufungwa kwa hila za kisiasa.

Ukosefu wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ni janga lingine vijana wengi waliohitimu elimu zao wamenyimwa mikopo wapo mtaani wanazurura tu,
Nchi hii kwa sasa hakuna demokrasia, hakuna uhuru wa bunge (mtu mmoja anapanga bajeti) , ni mtu mmoja tu anaetakiwa kusikika, ni yeye tu anaetakiwa kuwa live na ni yeye tu anaepanga kila kitu ndani ya nchi hii.

Hivi kweli Watanzania wenzangu wameridhika na hali hii, tumekaa kimya kabisa haya yakifanyika, tutamlaumu nani huko mbeleni.


Ulitaka tufanye nini sasa?
 
Kizazi kijacho kitalaumu sana kizazi hiki cha vijana wa. Com. Tumeshidwa kuibadilisha nchi kama vijana shenzi zetu tunapiga domo tu mitandaoni no action.
 
Hakuna njia mbadala ya kututoa tulipo!.Je unayo ili tutoke hapa? weka jamvini tusikie ushauri mubashara
 
Siasa za kutishana, "Mkifanya hivyo patakua kama Rwanda" "Si mnawaona Libya?" Zinawatisha wanaopiga kura.

Nimesema wanaopiga kura kwa sababu wapiga kura ni wengi ila wanaopiga ni wachache, mara ya mwisho utafiti ulionesha kua wazee hupiga kura kwa asilimia kubwa kushinda vijana, vijana wapo vizuri kwenye makelele siyo kwenda kupanga foleni na kupiga kura.

Hao wazee ni wale walioshuhudia utafutaji uhuru kipindi hiko umeme ni anasa mpaka leo yeye kwake kuna umeme, aikatae CCM? Hapana.
Anatishwa kutokipa kura chama fulani moto utakaowaka ni kiwango cha Libya na Rwanda, asiende kukipigia kile chama? Hapana.

Hapo ndiyo unahisi waTanzania wameridhika ila hakuna kitu kama hicho
 
Kizazi kijacho kitalaumu sana kizazi hiki cha vijana wa. Com. Tumeshidwa kuibadilisha nchi kama vijana shenzi zetu tunapiga domo tu mitandaoni no action.

TANU Youth League bado wanaendeleza kazi ya kuweka mazingira rafiki zaidi kwa ajili ya kudumisha matunda endelevu ya uhuru.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom