Hivi kweli tumefika huku.....!!!!

Papushikashi

JF-Expert Member
Feb 28, 2016
10,702
12,774
Habari zenu waungwana na bila shaka weekend imeenda mujarabu

Niende moja kwa moja kwenye mada
Juzi kuna rafiki yangu wa siku nyingi tulikuwa tumepoteana kitambo na hatukuwa na mawasiliano, sasa nimeangaika nikawa nimepata mawasiliano yake. Basi nikampigia simu tukawa tunapiga story za hapa na pale, za maisha (kaajiriwa) sasa tukaingia kwenye suala hili la pensheni la asilimia 25...sasa nikawa namtania kwamba hajitahidi kuweka akiba maana akisubiri pensheni huko mbeleni hii sheria itawakamua....
Ghafla nikaona mtu kanikatia simu na baadae kidogo akanitumia sms kwamba eti haya mambo tusiyaongee kwenye simu maana eti serikali inarekodi mazungumzo kwahiyo tutajiweka kwenye matatizo......aisee nilipigwa na butwaa nikasema kweli tumefikia hatua ya kuogopa kiasi hiki mpaka tunashindwa kuongea mambo yanayotuhusu.....
Kweli tumefikia hatua ya kuogopa kiasi hiki?

Karibu kwa mjadala
 
Swala ni lazima amuogope simba mana haijawahi kutokea swala akamla simba au hata kumfukuza.

Swala anatishwa na historia ya kuwa chakula cha Simba .
 
Hali inatisha sana kwakweli..ni ile bora punda afe mzigo ufike.
 
Hugo jamaa mfute kuwa rafiki kwa kuwa anakuwa boya na fara kwa kuwa serikali haijawahi kufanya anachosema na kama unatukana watu sawa Ila unazungumzia maswala ya mafao halafu anakuwa hivyo basi kada yake itakuwa ile inayorudisha maendeleo na kulalamiki kila siku badala ya kufanya kazi kwa bidii
 
Habari zenu waungwana na bila shaka weekend imeenda mujarabu

Niende moja kwa moja kwenye mada
Juzi kuna rafiki yangu wa siku nyingi tulikuwa tumepoteana kitambo na hatukuwa na mawasiliano, sasa nimeangaika nikawa nimepata mawasiliano yake. Basi nikampigia simu tukawa tunapiga story za hapa na pale, za maisha (kaajiriwa) sasa tukaingia kwenye suala hili la pensheni la asilimia 25...sasa nikawa namtania kwamba hajitahidi kuweka akiba maana akisubiri pensheni huko mbeleni hii sheria itawakamua....
Ghafla nikaona mtu kanikatia simu na baadae kidogo akanitumia sms kwamba eti haya mambo tusiyaongee kwenye simu maana eti serikali inarekodi mazungumzo kwahiyo tutajiweka kwenye matatizo......aisee nilipigwa na butwaa nikasema kweli tumefikia hatua ya kuogopa kiasi hiki mpaka tunashindwa kuongea mambo yanayotuhusu.....
Kweli tumefikia hatua ya kuogopa kiasi hiki?

Karibu kwa mjadala
Bila shaka alikua mwalimu,, tena kada wa CCM anaelala na kuota Siku moja atakua mmoja wa wateule,,, Mkuu hawa watu wanakuaga kama wamerukwa na akili
 
Hugo jamaa mfute kuwa rafiki kwa kuwa anakuwa boya na fara kwa kuwa serikali haijawahi kufanya anachosema na kama unatukana watu sawa Ila unazungumzia maswala ya mafao halafu anakuwa hivyo basi kada yake itakuwa ile inayorudisha maendeleo na kulalamiki kila siku badala ya kufanya kazi kwa bidii
Nimependa id yako....lakini kwanini tumefika huku?
 
Kawaida waajiriwa wengi serikalini ambao wana nafasi kubwa kubwa (managerial positions) simu zao haziko salama sana kwa sababu watu wa system uwa wanafuatilia kwa karibu mawasiliano yao. Hivyo si vizuri kwa wenye nafasi kama hizo kuongea kwa simu au kutumiana meseji zinazohusu mambo yanayoonekana kupingana na serikali.
 
Back
Top Bottom