Hivi kweli huwa inatokea?

Hivi kweli huwa inatokea?

ABDUL JIRANI

Senior Member
Joined
Jul 20, 2013
Posts
176
Reaction score
52
Kama siku wiki imepita tangu rafiki yangu anitembelee nyumbani kwangu na mpenzi wake. Wakakaa siku mbili na kuondoka. katika pitapita zangu nikakutana naye mtaani yule msichana nikapiga nae stori za hapa na pale mwisho nikamuaga kuondoka kwa sababu nilikuwa na mtu namuwahi.

Lakini kabla sijaondoka akaniomba nimpatie namba ya simu nikampa kisha nikaondoka chaajabu mpaka hii leo ni siku ya pili ananipigia simu kutaka kuja kwangu isitoshe mimi naishi bachela.

Wadau nimruhusu aje au nimkaushie?
 
mmnh kama unaujali urafki wko na rafki yako mfoadie msg na umwambie amkanye demu wake
wanawake wako wengi ni mbaya kutembea na demu wa rafiki yako
 
mmnh kama unaujali urafki wko na rafki yako mfoadie msg na umwambie amkanye demu wake
wanawake wako wengi ni mbaya kutembea na demu wa rafiki yako

Ni kwel ila msumbufu hata ukimkatalia bado anakuwa kinganganiz
 
Ivi ni kweli yeye anakusumbua au ni wewe ndie unaemsumbua?
 
Usimpe nafasi ya kuelezea feelings zake kama unajali urafiki wenu.

Be a kinda cold.
 
Stuka wewe wamepanga dili lakukuangamiza na gonjwa hatari la ukimwi so take care!
 
Usimruhusu aje kwa afya ya urafiki wenu na ukizingatia ni demu wa rafiki yako.
 
Angekuwa rafiki yako kweli wala usingeanzisha thread hii
 
Hili nalo ni swali la kutuuliza watu wazima?
 
Mruhusu aje, kwani kuishi bachela ndo nni???
Usiwe na mawazo yako ya kishetani kumbe mwenzio hana hayo mawazo???
Nakwambia ni utahaibika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom