Hivi kwanini Wabongo hawana amsha amsha?

Zee Korofi

JF-Expert Member
Oct 5, 2021
1,612
1,410
Yaani Wabongo amsha amsha kwenye issues za msingi hawana kabisa, kisiasa ni kondoo ambao wanapelekeshwa kwa kila kitu. Sioni Wabongo mfano wa miamba ya akina Aristotle na Plato, mifano ya akina Lincoln, mifano ya watu wagumu waliowahi kufanya makubwa duniani.

Wengi ni hodari kwenye upuuzi usio na tija, na ubishani wa kijinga. Kila kitu ubishi ubishi tu, huku muda unakwenda na kazi haifanyiki, maendeleo zero, vijana wamekalia kubishana mitandaoni tu, kutoa hoja nyiiingi kana kwamba zitatekelezeka in real life, mwisho zero.

Yaani mtu anajifia ndani au kwenye hospitali ndogo kulinganisha na magonjwa anayoumwa. Bila msaada wowote kutoka kwa ndugu na marafiki. Michango ya maana hamna, ila akifariki anazikwa kwa gharama, ndugu wazito mno wanakuja. Wengine kutoka hata nje ya Afrika, wenye pesa kede kede.

Watu watakula, watasaza, watazika. Ila ukiumwa utaambulia "pole" tu ya mdomo, wachache watakuuguza mpaka utakapokata roho, hawa Mara nyingi ni mama yako na baba yako. Ukifa mpaka mjomba wako wa SA atatuma ndege ikupeleke kijijini, na baba yako mdogo pale MOI atatoa milioni 10 kwa ajili ya chakula na kutengeneza ukumbi wa msiba.

Binamu yako wa USA atakuja na kutoa 20000000 kwa ajili ya rambi rambi kwa wazazi wako na kuwajengea pa kujisitiri

Mara baada ya kutafakari haya usiku mmoja huku machozi yakinilenga lenga, niliamua kwa dhati kutochangia TENA sherehe yoyote au ndoa. Niliapa kuchangia matibabu tu badala ya sherehe na harusi. Sijui kama nipo au sipo sahihi, ila ni miaka 8 sasa sitoi mchango wa harusi au sherehe yoyote, pia hata harusi yangu sitoomba mchango wa yeyote.

Kifupi tunapigiana chapuo na kuhimizana kwenye vitu vya kipuuzi au vyenye kuleta maumivu. Ni rahisi mtu kukushawishi uingie kwenye ndoa kisa yeye anaumia kwenye ndoa ila ana-fake ili na wewe uingie uteseke.

Ni hatari na upumbavu!
 
Umeeleza ukweli kabisa, na hayo ndiyo yaliyopo kwenye Jamii zetu.

Bado tuna Safari ndefu ya kuweza kutathimini juu ya priorities, about what matters the most
 
Yaani Wabongo amsha amsha kwenye issues za msingi hawana kabisa, kisiasa ni kondoo ambao wanapelekeshwa kwa kila kitu. Sioni Wabongo mfano wa miamba ya akina Aristotle na Plato, mifano ya akina Lincoln, mifano ya watu wagumu waliowahi kufanya makubwa duniani.

Wengi ni hodari kwenye upuuzi usio na tija, na ubishani wa kijinga. Kila kitu ubishi ubishi tu, huku muda unakwenda na kazi haifanyiki, maendeleo zero, vijana wamekalia kubishana mitandaoni tu, kutoa hoja nyiiingi kana kwamba zitatekelezeka in real life, mwisho zero.

Yaani mtu anajifia ndani au kwenye hospitali ndogo kulinganisha na magonjwa anayoumwa. Bila msaada wowote kutoka kwa ndugu na marafiki. Michango ya maana hamna, ila akifariki anazikwa kwa gharama, ndugu wazito mno wanakuja. Wengine kutoka hata nje ya Afrika, wenye pesa kede kede.

Watu watakula, watasaza, watazika. Ila ukiumwa utaambulia "pole" tu ya mdomo, wachache watakuuguza mpaka utakapokata roho, hawa Mara nyingi ni mama yako na baba yako. Ukifa mpaka mjomba wako wa SA atatuma ndege ikupeleke kijijini, na baba yako mdogo pale MOI atatoa milioni 10 kwa ajili ya chakula na kutengeneza ukumbi wa msiba.

Binamu yako wa USA atakuja na kutoa 20000000 kwa ajili ya rambi rambi kwa wazazi wako na kuwajengea pa kujisitiri

Mara baada ya kutafakari haya usiku mmoja huku machozi yakinilenga lenga, niliamua kwa dhati kutochangia TENA sherehe yoyote au ndoa. Niliapa kuchangia matibabu tu badala ya sherehe na harusi. Sijui kama nipo au sipo sahihi, ila ni miaka 8 sasa sitoi mchango wa harusi au sherehe yoyote, pia hata harusi yangu sitoomba mchango wa yeyote.

Kifupi tunapigiana chapuo na kuhimizana kwenye vitu vya kipuuzi au vyenye kuleta maumivu. Ni rahisi mtu kukushawishi uingie kwenye ndoa kisa yeye anaumia kwenye ndoa ila ana-fake ili na wewe uingie uteseke.

Ni hatari na upumbavu!
Mkuu tulikuwa tunaitwa WADANGANYIKA kabla hatujawa WATANZWA-NIA .
Watu wa giza walituwahi mapema walipogundua hili taifa lina resource za kufa mtu na limebarikiwa kichwa kiitwacho NYERERE, Wakamdanganya kwa matambiko ya kutosha alipokuwa akiongoza harakati za kutafuta uhuru, waliliinamisha taifa lote mpaka ikulu ya magogoni imekuwa ya " wazee wa Dar es Salaam" miaka yote.
Mizimu imekamata akili zote kwa maagano ya siri aliyofanyishwa baba wa taifa bila mwenyewe kutambua wakati ule.
Imekuwa ni desturi sasa siasa zote za nchi hii ni uchawi, viongozi wote wanapogombea wanatafuta uganga na uchawi, ili kuinamisha akili za Watanzania ili wawachague, sasa niambie hizi akili zetu Watz zimeinamishwa kiasi gani mpaka sasa!
JPM alipojaribu kuwakataa wazee wa Dar jumba jeupe halikukalika , mpaka akalihama, akajaribu kuvunja giza kwa kujiunganisha yy na taifa kwa kuwahusisha viongozi wa dini badala ya wazee wa giza, ila tunajua wote yaliyofuata!
Sasa usishangae jamaa wakionesha umiliki wao tena kwa uchifu!
 
Mkuu tulikuwa tunaitwa WADANGANYIKA kabla hatujawa WATANZWA-NIA .
Watu wa giza walituwahi mapema walipogundua hili taifa lina resource za kufa mtu na limebarikiwa kichwa kiitwacho NYERERE, Wakamdanganya kwa matambiko ya kutosha alipokuwa akiongoza harakati za kutafuta uhuru, waliliinamisha taifa lote mpaka ikulu ya magogoni imekuwa ya " wazee wa Dar es Salaam" miaka yote.
Mizimu imekamata akili zote kwa maagano ya siri aliyofanyishwa baba wa taifa bila mwenyewe kutambua wakati ule.
Imekuwa ni desturi sasa siasa zote za nchi hii ni uchawi, viongozi wote wanapogombea wanatafuta uganga na uchawi, ili kuinamisha akili za Watanzania ili wawachague, sasa niambie hizi akili zetu Watz zimeinamishwa kiasi gani mpaka sasa!
JPM alipojaribu kuwakataa wazee wa Dar jumba jeupe halikukalika , mpaka akalihama, akajaribu kuvunja giza kwa kujiunganisha yy na taifa kwa kuwahusisha viongozi wa dini badala ya wazee wa giza, ila tunajua wote yaliyofuata!
Sasa usishangae jamaa wakionesha umiliki wao tena kwa uchifu!
Maneno ni mazito sana, nini maana yake? Kwa hiyo tumefungwa akili kimkakati? JPM alikuwa na uthubutu mno!

Sent from my A50s using JamiiForums mobile app
 
Mkuu tulikuwa tunaitwa WADANGANYIKA kabla hatujawa WATANZWA-NIA .
Watu wa giza walituwahi mapema walipogundua hili taifa lina resource za kufa mtu na limebarikiwa kichwa kiitwacho NYERERE, Wakamdanganya kwa matambiko ya kutosha alipokuwa akiongoza harakati za kutafuta uhuru, waliliinamisha taifa lote mpaka ikulu ya magogoni imekuwa ya " wazee wa Dar es Salaam" miaka yote.
Mizimu imekamata akili zote kwa maagano ya siri aliyofanyishwa baba wa taifa bila mwenyewe kutambua wakati ule.
Imekuwa ni desturi sasa siasa zote za nchi hii ni uchawi, viongozi wote wanapogombea wanatafuta uganga na uchawi, ili kuinamisha akili za Watanzania ili wawachague, sasa niambie hizi akili zetu Watz zimeinamishwa kiasi gani mpaka sasa!
JPM alipojaribu kuwakataa wazee wa Dar jumba jeupe halikukalika , mpaka akalihama, akajaribu kuvunja giza kwa kujiunganisha yy na taifa kwa kuwahusisha viongozi wa dini badala ya wazee wa giza, ila tunajua wote yaliyofuata!
Sasa usishangae jamaa wakionesha umiliki wao tena kwa uchifu!
Hii maneno ni kama inaflow hv
 
Maisha yenyewe ya Bongo changamoto, unaaanzisha harakati za kuamsha amsha unaishia korokoroni peke yako, siasa sio favourable kibongobongo tuseme ukweli..

Kuhusu ishu za michango ya harusi, elimu na matibabu well inadepend na mtazamo wako binafsi ambao hatukuzuii unaweza kuwa sawa upande mwingine na upande mwingine hauko sawa..maana unakochangia ni kwenye jamii hiyohiyo ambayo inakuzunguka ambapo leo au kesho utawahitaji kwa namna moja au nyingine

Sent from my SM-J720F using JamiiForums mobile app
 
647.jpg
 
Vijana wa kibongo wakiunga mkono tozo huku wakijadili vile tozo zitaipeleka nchi kuwa Taifa la ulimwengu wa kwanza👇😁😁😁
1637308571637308570.jpg
1637306176_1637306175-picsay.png
 
Halafu alitamka hayo kwa vijana wa UDSM, unaweza kuona alikuwa na nia njema kwa taifa kiasi gani,
Sio haya majizi yetu yaliyoiba hati miliki za taifa ikulu yakazipeleka kwenye ikulu zao!
We mtu anajenga kasiri copyright na ikulu halafu mtu mwenyewe katoka madarakani na anasifa kama hizo, hawajamsimikia huko baharini atutawale na ukoo wake nchi hii milele kweli,
Maana huko mnarani ndio V8 zilikuwa hazikauki wakati wa uchaguzi,
 
Mkuu uliza tu kwanini Wabongo hatuna Critical Thinkers mfano enzi za Kina Nyerere, Nkurumah Sankara n.k.; Unapoongelea kina Aristotle na Plato swali lako lingekuwa kwamba kwanini Dunia ya sasa hakuna Amsha Amsha....

Dunia ya leo ni watu wa easy things hawataki kusumbua akili zao..., watu wa kumeza na sio kuchunguza
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom