Hakuna siku ipitayo bila mtu kuweka post ya ulalamishi humu jf kuhusu ya kina dada hivi mara kina dada vile, mbona wengi wenu nyiye kinababa mu walalamishi sana? Natambua kwamba hii ni tabia ya baadhi ya wanaume sio wote hivyo post yangu inawalenga wale wenye tabia hiyo. Kasoro za wanaume zipo lukuki mbona hamzisemi au hamzioni au wanaume mko perfect? Nitoe mifano michache; mtu anajijua miguu yake inanuka halafu anavua viatu kwenye daladala/basi au ndani ya nyumba na kukera watu wote ni sahihi? Mbona hamlalamikiwi au ni haki yenu kukera wengine? Boxer ndo zishatajwa humu, mtu habadilishi mwezi hadi inafubaa au kuota ukoko/ugaga au vyote, halafu unai display kwa kuvaa mlegezo? Makwapa ya baadhi wakaka na wababa yananuka kiasi kwamba akinusishwa mtu aliyezimia anaweza kuzinduka, kuna siku konda alinipitishia kwapa lake wakati anachukua nauli toka mtu wa nyuma yangu, nakumbuka ilikuwa asubuhi - looh! hapohapo nilisikia kizunguzungu na kichefuchefu kwa wakati mmoja. Baadhi ya wanaume muda mwingi wana midomo inayotoa harufu ya breweries au harufu nyinginezo, tena harufu zenyewe zinakuwa sio fresh kwasababu mtu hapigi mswaki vizuri, mdomo unachacha halafu unasemesha mtu huku umemsogelea karibu na pua au mdomo, unafikiri ana enjoy kunusa hiyo harufu? Halafu tabia ya ku generalise sio nzuri, kitu akifanya mtu mmoja sio useme kina dada wote - kama heading yako ilivyo hapo juu, hao wadada wawili uliowaona ndio walio expose nguo zao za ndani au unataka kutuambia wanawake wote unaowaonaga wewe nguo zao za ndani ziko nje? Maana yake hata za dada zako unazionaga?