Hivi kurudia uchaguzi na kuandaa Katiba mpya, ni lipi lina maslahi mapana kwa Taifa letu?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Tumemsikia wenyewe siku ya jana kwenye kongamano la uchumi, lililofanyika chuo kikuu cha Dar, Rais Magufuli akieleza kuwa hawezi kutenga fungu la pesa kwa ajili ya kuwapa posho wajumbe kwa ajili ya kuandaa Katiba mpya!

Akaendelea kueleza Mheshimiwa Rais kuwa ni heri pesa hiyo aipeleke kujenga reli ya Standard gauge........

Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa kuhusu msimamo huo wa Rais. Je tunavyotumia mabilioni ya pesa katika kurudia uchaguzi, kwa wagombea wanaotoka upinzani, wakigombea kwa nafasi zile zile walizokuwa nazo awali, je hayo ndiyo matumizi mazuri ya pesa zetu??

Vile vile nimjulishe Mheshimiwa Rais kuwa kilio cha Katiba mpya ni cha mamilioni ya watanzania, na wanaoipinga hii Katiba mpya ya Tume ya Warioba ni watu wachache sana walioko kwenye ngazi ya utawala

Hivi ngoja nimuulize swali jingine Mheshimiwa Rais, hivi hii pesa ya kuandaa Katiba mpya inatoka mifukoni mwake??

Kwa kuwa kwa namna alivyoongelea kuwa yeye hawezi toa pesa za kuwalipa posho "bure" kwa wajumbe wa Bunge la Katiba, utadhani pesa hiyo inatoka mifukoni mwake!

Nimuulize swali jingine, hivi haoni jinsi Taifa linavyopoteza mabilioni ya shilingi katika kurudia chaguzi ndogo kutokana na CCM "kuwanunua" wabunge hao wa upinzani??

Hivi tukilinganisha matumizi ya kurudia chaguzi ndogo na Taifa kupata Katiba mpya, hivi ni matumizi gani ambayo kiuhalisia ni ya hovyo kabisa??

Kwa kuwa kwa namna alivyoongelea Jana, ni kama pesa hiyo anavyoionea uchungu kama inatoka mifukoni mwake na hazitoki kwenye hazina ya Taifa!

Nipende tu kumfahamisha Mheshimiwa Rais kuwa ametoa mawazo yake binafsi na ya wenzake wachache wa CCM, lakini atambue kuwa mamilioni ya watanzania bado wanaililia Katiba mpya, kwa kuwa wanajua kuwa Katiba iliyopo sasa ni kama ya mfumo wa chama kimoja cha CCM na imempa madaraka makubwa mno Rais, na ndicho wananchi wanachoona umuhimu wa kupata Katiba mpya

Kwa hiyo niwashauri wananchi, tusikatishwe tamaa na kauli ya Mheshimiwa Rais na tuendelee kuidai kwa nguvu zote ili nchi yetu iweze kupata Katiba mpya ambayo ndiyo itakayotupa dira nzuri na ustawi wa nchi yetu na ndiyo itafaa katika kipindi cha sasa cha mfumo wa vyama vingi

Mungu ibariki Tanzania
 
Mtu yoyote anayetaka Katiba mpya Tanzania yetu kwa sasa ni mvivu na hana kazi ya kufanya, vinginevyo angekuwa kazini, kamuulize Muhindi Dewji na familia yake kama hata wanajua chochote au hata kujali kuhusu hiyo mnayoiita Katiba mpya!
 
Mtu yoyote anayetaka Katiba mpya Tanzania yetu kwa sasa ni mvivu na hana kazi ya kufanya, vinginevyo angekuwa kazini, kamuulize Muhindi Dewji na familia yake kama hata wanajua chochote au hata kujali kuhusu hiyo mnayoiita Katiba mpya!
Wewe umepangwa humu JF ku-clash hata yale mawazo mazuri yanayotolewa kwa maslahi mapana ya Taifa hili.......

Badala yake umekuwa mtu wa kumsifu kwa kila jambo analofanya/ analosema Magufuli!

Siwezi kupoteza muda kujibishana nawe
 
Mtu yoyote anayetaka Katiba mpya Tanzania yetu kwa sasa ni mvivu na hana kazi ya kufanya, vinginevyo angekuwa kazini, kamuulize Muhindi Dewji na familia yake kama hata wanajua chochote au hata kujali kuhusu hiyo mnayoiita Katiba mpya!
Bado hujachambua vyema kivipi anayedai katiba hana kazi?bado hujathibiyisha hoja yako hebu ipe nyama
 
Mtu yoyote anayetaka Katiba mpya Tanzania yetu kwa sasa ni mvivu na hana kazi ya kufanya, vinginevyo angekuwa kazini, kamuulize Muhindi Dewji na familia yake kama hata wanajua chochote au hata kujali kuhusu hiyo mnayoiita Katiba mpya!
Kwa hiyo waliotunga katiba mwaka 1977 walikuwa wavivu?
 
Suala la kurudia uchaguzi lipo kikatiba/kisheria na si matakwa ya mtu. Katiba mpya ulikuwa mchezo wa watu kupiga hela.
 
Tumemsikia wenyewe siku ya jana kwenye kongamano la uchumi, lililofanyika chuo kikuu cha Dar, Rais Magufuli akieleza kuwa hawezi kutenga fungu la pesa kwa ajili ya kuwapa posho wajumbe kwa ajili ya kuandaa Katiba mpya!

Akaendelea kueleza Mheshimiwa Rais kuwa ni heri pesa hiyo aipeleke kujenga reli ya Standard gauge........

Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa kuhusu msimamo huo wa Rais. Je tunavyotumia mabilioni ya pesa katika kurudia uchaguzi, kwa wagombea wanaotoka upinzani, wakigombea kwa nafasi zile zile walizokuwa nazo awali, je hayo ndiyo matumizi mazuri ya pesa zetu??

Vile vile nimjulishe Mheshimiwa Rais kuwa kilio cha Katiba mpya ni cha mamilioni ya watanzania, na wanaoipinga hii Katiba mpya ya Tume ya Warioba ni watu wachache sana walioko kwenye ngazi ya utawala

Hivi ngoja nimuulize swali jingine Mheshimiwa Rais, hivi hii pesa ya kuandaa Katiba mpya inatoka mifukoni mwake??

Kwa kuwa kwa namna alivyoongelea kuwa yeye hawezi toa pesa za kuwalipa posho "bure" kwa wajumbe wa Bunge la Katiba, utadhani pesa hiyo inatoka mifukoni mwake!

Nimuulize swali jingine, hivi haoni jinsi Taifa linavyopoteza mabilioni ya shilingi katika kurudia chaguzi ndogo kutokana na CCM "kuwanunua" wabunge hao wa upinzani??

Hivi tukilinganisha matumizi ya kurudia chaguzi ndogo na Taifa kupata Katiba mpya, hivi ni matumizi gani ambayo kiuhalisia ni ya hovyo kabisa??

Kwa kuwa kwa namna alivyoongelea Jana, ni kama pesa hiyo anavyoionea uchungu kama inatoka mifukoni mwake na hazitoki kwenye hazina ya Taifa!

Nipende tu kumfahamisha Mheshimiwa Rais kuwa ametoa mawazo yake binafsi na ya wenzake wachache wa CCM, lakini atambue kuwa mamilioni ya watanzania bado wanaililia Katiba mpya, kwa kuwa wanajua kuwa Katiba iliyopo sasa ni kama ya mfumo wa chama kimoja cha CCM na imempa madaraka makubwa mno Rais, na ndicho wananchi wanachoona umuhimu wa kupata Katiba mpya

Kwa hiyo niwashauri wananchi, tusikatishwe tamaa na kauli ya Mheshimiwa Rais na tuendelee kuidai kwa nguvu zote ili nchi yetu iweze kupata Katiba mpya ambayo ndiyo itakayotupa dira nzuri na ustawi wa nchi yetu na ndiyo itafaa katika kipindi cha sasa cha mfumo wa vyama vingi

Mungu ibariki Tanzania
Kupanga ni kuchagua.
 
Mtu yoyote anayetaka Katiba mpya Tanzania yetu kwa sasa ni mvivu na hana kazi ya kufanya, vinginevyo angekuwa kazini, kamuulize Muhindi Dewji na familia yake kama hata wanajua chochote au hata kujali kuhusu hiyo mnayoiita Katiba mpya!
Duh!
 
Mtu yoyote anayetaka Katiba mpya Tanzania yetu kwa sasa ni mvivu na hana kazi ya kufanya, vinginevyo angekuwa kazini, kamuulize Muhindi Dewji na familia yake kama hata wanajua chochote au hata kujali kuhusu hiyo mnayoiita Katiba mpya!
Yuleyule aliyetekwa ukatoa hisia zako za kikaburu na unyanyapaa, au mwingine?
 
Back
Top Bottom