GE2025 Hivi kama ndani ya CCM wanaweza kunyang'anyana haki, ndio iwe kwenye chaguzi nje ya chama?

GE2025 Hivi kama ndani ya CCM wanaweza kunyang'anyana haki, ndio iwe kwenye chaguzi nje ya chama?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,866
Reaction score
4,252
Fikiria Kigwangala anaporwa ushindi. Anaumia moyoni kisha anaunga mkono uporaji.

Fikiria Ummy anakwapuliwa nafasi yake halali. Anaugulia moyoni kisha anatoka hadharani kuunga mkono

Fikiria Gambo anapigwa kumbo laivu.. Yani haruhusiwi hata kugombea. Analialia kisha tunamsahau.

Mpina hatujamwacha. Anaporwa ndani na anaporwa nje. Anapigwa home and away na hana pa kusemea.

Hao ni wachache sana. Ikiwa kwao wanafanyiziana hivi na hakuna pa kwenda, itakuwaje kwa wapinzani?

Siasa nzuri na za hoja zilizama na JK - Kikwete. Huyu ambaye tunamlaumu leo. Tumpe maua yake.

Siasa chafu zilianzia kwa JPM, kisha ikaonekana kumbe inawezekana? Hata JK anajisemea, kumbe inawezekana?

Swali la kujiuliza, inakuwaje tumevikwa vazi la hofu kiasi hiki? Wanawezaje? Kama wanaweza kutumia hila hivi na wakafanikiwa. Kwa nini wasinvetumia akili na maarifa hayo kuteka mioyo na wananchi?

Shida yetu kuu ni hawa CCM wafuasi. Wanaoporwa haki na bado wakabaki kusifu. Laiti wangejitutumua kama Mpina leo hii haya maujinga yasingekuwepo.

Kwanza tuidai Tanzania ya Mwinyi. Ile ya Mkapa. Iliyokuwa ya Jakaya. Ile ya Magufuli pamoja na jitihada za kiuchumi alizofanya, hapana. Hii ya Samia, big NO!

Mihimili ya Dola ilikufa kipindi cha JPM. Katiba ilikufa kipindi hicho. Mabakama zilipata ubutu wakati huo. Ndipo tukasikia KAZI iendelee.

Hadi kenge atakapoona damu ndio atajua kuwa kaumia. Sasa tumwache autumie mkia wake kwa kuchapia
 
Mwenye masikio yanayosikia na asikie, na mwenye macho ya kuona na aone bandiko hili.
Akhsante kwao mpandisha uzi.
Chakula ya akili.
 
Mjinga na Mpumbavu pekee anayeweza kuendelea kumlaumu Magufuli mpaka leo ni sawa na wale wapumbavu wanaoendelea kumlaumu Nyerere mpaka leo kisa katiba nyie mmefanya nini? kubadilisha Ayo mabaya wananchi nyie nikulaumu mtu na kumwachia Mungu kasikilize wimbo wa Joh makini simwachii Mungu.
 
Ukweli lazima usemwe baz kaiza. Wala hakuna aliemwachia Mungu, ndio maana tunasema huku. Na wengine wanapambana huko.

Kuna mdau mmoja aliandika, kosa la Jpm aliharibu kwa mtandao akaharibu na wapinzani kisha akabaki mwenyewe. Nami naongeza hapo, aliwagawa pia wananchi.
 
Back
Top Bottom