Hivi inawezekana kuteua Makamu kutoka Upinzani?

TANMO

JF-Expert Member
Apr 12, 2008
11,513
11,276
Hili swali limenijia ghafla wakati tunaendelea kuomboleza Kifo cha Rais Magufuli.

Kutokana na ukweli kuwa Uchaguzi uliofanyika mwaka Jana umeacha majonzi makubwa Kwa Viongozi na wafuasi Wa Vyama vya Upinzani. Pamoja na kuibuka manung'uniko miongoni mwa watanzania kuwa Vyombo vya Dola vilivyohusika kwenye Kampeni na hatimaye Uchaguzi vilipendelea Chama Tawala hata katika maeneo kilipoonekana kushindwa ama kuzidiwa na Upinzani.

Tuliona hali ya majonzi na hata manung'uniko kule Zanzibar lakini baada tu ya Rais Mwinyi kumwapisha Maalim Seif kuwa makamu Wa kwanza Wa Rais, ghafla hali ikabadilika na wananchi wengi hata wapinzani wakaonesha imani na mapenzi Kwa Serikali ya Rais Mwinyi.

Je, katika wakati huu tuliogubikwa na chuki na mpasuko Wa Kiitikadi za kisiasa, Mama Samia Suluhu anaweza kuteua Makamu wake kutoka Chama kikuu cha Upinzani nchini ili kutuliza hali?
 
Katiba inasema makamu rais akishachukua nafasi ya urais, atashauriana na chama chake ili kupata jina la makamu wa rais..na jina hilo itabidi lipitishwe na bunge.

Sasa labda rais mpya anaweza akashauriana na chama chake na wakaamua kuchagua mpinzani kuwa makamu wa rais. Ila haya ni maneno ya kuongea tu lakini practically haiwezi kuja kutokea.
 
Katiba inasema makamu rais akishachukua nafasi ya urais..atashauriana na chama chake ili kupata jina la makamu wa rais..na jina hilo itabidi lipitishwe na bunge. Sasa labda rais mpya anaweza akashauriana na chama chake na wakaamua kuchagua mpinzani kuwa makamu wa rais. Ila haya ni maneno ya kuongea tu lakini practically haiwezi kuja kutokea
Kumbe anaweza akapendekeza lakini Bunge Kwa vile limejaa CCM wakalikataa Jina?
 
Mmekuwa mafisi kutegemea mkono udondoke. Hivi kwa akili yako ndogo unaona nani pale kwa vilaza anaweza kuwa hata waziri ndani ya serkali
 
Katiba inasema makamu rais akishachukua nafasi ya urais..atashauriana na chama chake ili kupata jina la makamu wa rais..na jina hilo itabidi lipitishwe na bunge.

Sasa labda rais mpya anaweza akashauriana na chama chake na wakaamua kuchagua mpinzani kuwa makamu wa rais. Ila haya ni maneno ya kuongea tu lakini practically haiwezi kuja kutokea.
Kwanini isiwezekane Kitila Mkumbo,Anna Mwigira waliwezaje kufika uko ccm na madaraka kupewa
 
Wanaopendekeza jina ni Kamati za CCM, na anapigiwa kura na bunge lenye CCM mps wengi!

Mpinzani hawezi kupita
 
Walitegemea uchaguzi mpya. Mambo yamewabadilikia
Mmekuwa mafisi kutegemea mkono udondoke. Hivi kwa akili yako ndogo unaona nani pale kwa vilaza anaweza kuwa hata waziri ndani ya serkali
 
Kwanini isiwezekane Kitila Mkumbo,Anna Mwigira waliwezaje kufika uko ccm na madaraka kupewa
Hao waliteuliwa moja kwa moja na Rais, hakukuwa na suala la Bunge kuidhinisha, japo kwa ukali wa Magufuli bado Bunge lingefyata kuidhinisha chaguo lake
 
Back
Top Bottom