Hivi huyu Macron anatutaka nini sisi Waafrika?

MakinikiA

JF-Expert Member
Jun 7, 2017
5,011
6,542
Macron akosoa 'unafiki' wa viongozi wa Afrika kuhusu vita vya Ukraine

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amekosoa vikali mwitikio wa viongozi wa Afrika kuhusu vita vya Ukraine wakati wa mkutano na waandishi wa habari mjini Yaoundé.

Bw Macron aligonga msumari na kuita ni"unafiki, haswa katika bara la Afrika" ambalo limekataa mzozo wa Ukraine kuwa ni vita.

Baadhi ya nchi za Kiafrika zimejizuia kukosoa vikali uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

Mwezi Machi, nchi 17 za Afrika zilipiga kura ya kutofungamana na upande wowote katika mzozo huo.

Pia alisema kuwa suluhu pekee la mzozo wa watu wanaoongea kiingereza nchini Cameroon ni uhamishaji wa mamlaka: "Ni kupitia mchakato huu wa kisiasa wa mazungumzo na mageuzi ndipo suluhu la kudumu linaweza kupatikana," Tovuti ya Journal du Cameroun ilimnukuu Macron akisema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom