Kumsaidia mumeo katika kipindi kigumu kama hicho ni jambo jema sana. Mambo ya kuzihgatia, pamoja na michango ya maana mingine iliyotolewa, ni
1. Angalia ni kwa kiasi gani tatizo la kazi limemshitua na kumchanganya, inawezekana bado haamini kuwa kazi imeondoka
2. Msaidie aweze kufanya shughuli anayoweza kufanya na kuifurahia. Usimlazimishe kufanya shughuli fulani kwa vile wewe ni mtoa pesa
3. Mtafutie washauri wazuri katika masuala ya biashara na ujasiliamali ili asichanganye mahusiano yenu ya ndoa katika biashara
4. Endelea kumuonyesha kuwa bado unamtegemea kama baba wa familia, usimsimange kwa kutafuta kwake misaada na kushindwa kwake.