Hivi Dola inakuwa na rais?

Hivi Dola inakuwa na rais?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,624
Reaction score
164,682
Naomba wanasheria na wataalamu wengine mtusaidie katika hili na itakuwa vizuri mtupe mifano ya hizo state au dola zenye maraisi.

Mimi navyojua state(dola) inakuwa na governor au kiongozi mwingine lakini sio raisi.

Wanasheria na wataalamu tunaomba mtupe darasa juu ya hili.

Vile vile sio vibaya tukapata definition halisi na ya kitaalamu juu ya dola(state).

NB:Huu ni mjadala unaojitegema kabisa hivyo tuwe makini.
 
Naomba wanasheria na wataalamu wengine mtusaidie katika hili na itakuwa vizuri mtupe mifano ya hizo state au dola zenye maraisi. Mimi navyojua state(dola) inakuwa na governor au kiongozi mwingine lakini sio raisi. Wanasheria na wataalamu tunaomba mtupe darasa juu ya hili. o Vile vile sio vibaya tukapata definition halisi na ya kitaalamu juu ya dola(state). NB:Huu ni mjadala unaojitegema kabisa hivyo tuwe makini.
Na kuupanua zaidi mjadala, je Marekani zile 'states' zinazoiunda USA ni 'dola'? Na ni vipi UK?
 
Na kuupanua zaidi mjadala, je Marekani zile 'states' zinazoiunda USA ni 'dola'? Na ni vipi UK?
USA - United State of America na hapa ndipo alipochemkia Shivj kwani kule USA kuna Rais mmoja tu na hivyo kwa kauli ya Shivj Zanzibar haikutakiwa kuwe na Rais
 
USA - United State of America na hapa ndipo alipochemkia Shivj kwani kule USA kuna Rais mmoja tu na hivyo kwa kauli ya Shivj Zanzibar haikutakiwa kuwe na Rais
Mimi naomba mwenye kutetea kauli hiyo aje na mfano wa dola ya aina hiyo na si kupiga makelele tu.
 
faiza foxy na wengineo tunaomba mtupe mfano walau mmoja tu.
 
Last edited by a moderator:
kwa miaka ya leo ndani ya tanzania huwezi kutofautisha wasomi na waganga njaa a.k.a wachumia tumbo.
 
Prof ni Mzanzibari,nadhani ana lake jambo na Tanganyika.
Halafu kaniudhi sana kusema kuwa Tanzania hatuna magazeti ila vipeperushi.
Hii ni dharau kubwa na jeuri.
Anyways,wanasheria tunawasubiri elimu kama lilivyolengo la mleta hoja.Tunasubiri.
 
Pasco tunaomba ufafanuzi tafadhali...
 
Last edited by a moderator:
prof shivji nae anaweza tu kukosea,kwa kutoa mfano wa usa.kuna rais mmoja na kuongoza majimbo,hvyo basi zanzibar haipaswi kuwa na rais hata kidogo,muungano uliasisiwa kimizengwe na baba wa taifa,nyerere alikuwa anafanya mambo kimizengwe tu nae,
 
Tatizo la nchi zetu hizi ambazo propaganda, hata za uongo wa waziwazi, zimegeuka mhimili mojawapo muhimu wa dola inasikitisha kuona media zikieneza propaganda hizi kwa kutoa nafasi kwa upande mmoja bila upande mbadala kupata hata chembe ya airtime kutoa mawazo yao. This is unfair and unacceptable.

Kama Shiviji na kundi lake na hata wiki iliyopita akina Bashiru Ally na wenzake walikuwa studio hizo hizo wakitoa "maoni yao" yenye mwelekeo mmoja kwa nini nafasi isitolewe kwa wenye mawazo tofauti nao wakatoa maoni yao? Lakini cha kushangaza zaidi ni kwamba Tume ya Warioba iliundwa kwa Sheria ya Bunge la Jamhuri na ilitekeleza majukumu yake kisheria. La ajabu ni kwamba hawa (akina Shivji, Bashiru, et. al.) ambao hata sheria haiwatambui ndio wanaoonekana kuhodhi mchakato; ni ajabu sana.
 
prof shivji nae anaweza tu kukosea,kwa kutoa mfano wa usa.kuna rais mmoja na kuongoza majimbo,hvyo basi zanzibar haipaswi kuwa na rais hata kidogo,muungano uliasisiwa kimizengwe na baba wa taifa,nyerere alikuwa anafanya mambo kimizengwe tu nae,

Tatizo la kufanya mambo kisanii ndio hilo. Hata uwe na shahada na uzoefu wa aina gani, usiposimamia mambo kwa uhalisia, ukweli, na facts, na badala yake ukafanya kisanii ili kuridhisha baadhi ya makundi ni lazima utajichanganya - haiepukiki. Muungano wa USA kuufananisha na wa Tz wapi na wapi? USA ni nchi moja, Rais mmoja, majimbo mengi (53) under the same sovereign state.

Inachopendekeza Rasimu ya Warioba ni kuelekea muungano sawa na wa USA kwamba tuwe na nchi moja (Tanzania), chini ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu mmoja na majimbo mawili (Tanganyika na Zanzibar) kama yalivyo ya USA. Sijui kwanini wasomi wazima wanashindwa kuona hilo.
 
prof shivji nae anaweza tu kukosea,kwa kutoa mfano wa usa.kuna rais mmoja na kuongoza majimbo,hvyo basi zanzibar haipaswi kuwa na rais hata kidogo,muungano uliasisiwa kimizengwe na baba wa taifa,nyerere alikuwa anafanya mambo kimizengwe tu nae,

Amekuwa prof.kilaza kabisa kwa kudanganya umma!
 
Tatizo la kufanya mambo kisanii ndio hilo. Hata uwe na shahada na uzoefu wa aina gani, usiposimamia mambo kwa uhalisia, ukweli, na facts, na badala yake ukafanya kisanii ili kuridhisha baadhi ya makundi ni lazima utajichanganya - haiepukiki. Muungano wa USA kuufananisha na wa Tz wapi na wapi? USA ni nchi moja, Rais mmoja, majimbo mengi (53) under the same sovereign state.

Inachopendekeza Rasimu ya Warioba ni kuelekea muungano sawa na wa USA kwamba tuwe na nchi moja (Tanzania), chini ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu mmoja na majimbo mawili (Tanganyika na Zanzibar) kama yalivyo ya USA. Sijui kwanini wasomi wazima wanashindwa kuona hilo.

Mkuu hongera sana kwa ufafanuzi uliokwenda shule. Ulichosema ndicho tume ya Warioba walicholenga hasaaaa,
Ukisoma rasimu hii ndiyo sentensi ya kwanza 1.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi na Shirikisholenye mamlaka kamili ambalo limetokana na Muungano wa nchi mbiliza Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ambazokabla ya Hati ya Makubaliano ya Muungano ya mwaka 1964, zilikuwanchi huru.

Hivi sielewi, hivi kwa sentensi kama hiyo hapo juu kwenye rasimu shids iko wapi? Kiukweli kuanzia leo Shifji ni wa kumchukulia kwa tahadhari sana
 
Ahsante sana Prof. Shivji leo umeweka wazi kila kitu, umefungua akili za walio wengi, hata hapa jukwaani sentensi ni ngumu kuandika kwa maana hiyo wameelewa.
 
Kwanza tungepata maana ya hayo maneno ili tuelewe vizuri kabla..
State
Dola
Governor
Nchi
Jimbo
 
Back
Top Bottom