Sizinga
Platinum Member
- Oct 30, 2007
- 9,101
- 6,025
Juzi jumapili nimeshuhudia kitu cha ajabu sana!! Huku maeneo ya Sombetini-Ngusero Juzi Jumapili kulikuwa busy sana na mambo ya Ndoa-Sherehe!! Mi nilikuwa town nimeenda zangu kuangalia Mpira, nikarudi kama mida ya saa 3 usiku hivi, sasa wakati tunarudi kwa daladala pale maeneo ya sombetini kuna pick-Up moja ilipakiza watu kama watano hivi nyuma na kulikuw na mandoo kadhaa, (walikuwa wakitoka kwa sherehe bila shaka),na nyuma kulikuwa na gari kama 3 hivi, sasa njia ilikuwa imejifunga na ile pick up ndio ikituletea kauzibe manake ilikuwa inataka kukona ili iende njia ya pembeni so ikawa imenasa katikati, so konda wa daladala kaanza kuzozana na mmoja wa watu wa ile pick-up ili asogeze gari pembeni si tupite....
Hee e bhana bila kutegemea jamaa wa ile pick up si kachomoa bomba(bastola) akaanza kumshurutisha dereva wa daladala arudi nyuma!! Ikabidi dreva awe mpole tukarudi nyuma mpaka kwenye ile gari ya tatu...aise nilishangaa sana!!
Sijajua tatio ni nini jiji la Arusha kutumia Bastola nje nje bila sababu za msingi.
Ona hii nayo https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/562721-risasi-zarindima-arusha.html
N.B: Umiliki wa Bomba uangaliwe upya Arusha!!
Hee e bhana bila kutegemea jamaa wa ile pick up si kachomoa bomba(bastola) akaanza kumshurutisha dereva wa daladala arudi nyuma!! Ikabidi dreva awe mpole tukarudi nyuma mpaka kwenye ile gari ya tatu...aise nilishangaa sana!!
Sijajua tatio ni nini jiji la Arusha kutumia Bastola nje nje bila sababu za msingi.
Ona hii nayo https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/562721-risasi-zarindima-arusha.html
N.B: Umiliki wa Bomba uangaliwe upya Arusha!!