Wanajamii hii mitandao mingine ya kijamii yakuangalia matumizi yke kwani kuna dada poa wanajiuza,wengine ni mawasiliano ya kawaida.Bsi kuna binti mmoja nilijaribu nione je inawezekana ukafanikiwa kumpata mpenzi kwa njia ya mtandao bsi nikaomba awe mpenzi wangu akakubali na mpaka sasa tunamawasiliano naye mazuri na nilimkaribisha afike kwetu amekubali na kunipa masharti ya kukaa na mm kwa wki moja halafu atarudi kwao na amenipa masharti nikitaka aje lazima nimrushie hela ya nauli na hela ya chakula njiani.Sasa naombeni ushauri je hawezi kuwa tapeli na je kweli inawezekana kukubali kiurahisi namna hyo kwani haujaisha hta mwezi mmoja toka tuwe na mawasiliano naye.kwa wenye uzoefu wa mapenzi ya mitandao je anaweza akanifaa ktk maisha,na nyongeza kwenye picha zake ameziba mdomo usionekane vzuri na nilipomwuliza alinijibu sio kzi yangu kujua na alikasirika sikuelewa ni kwa nn napata wasiwasi kdogo kwann apate hasira kwa jambo hilo.Naombeni ushauri kwani jumamosi hii ndio atafika kwangu na nilimwahidi kumtumia hela ya nauli na chakula njiani kesho ijumaa.