Historia ya wamakonde

Historia ya wamakonde

HISTORIA FUPI YA KABILA LA WAMAKONDE

Kama ulikua hujui chanzo Cha Wamakonde kuweka NDONYA na kuchanja CHALE wacha nikufahamishe;-

Wamakonde ni kabila linalo patikana katika wilaya zote za Mkoa wa Mtwara ila Masasi na Nanyumbu wapo kwa asilimia ndogo na kwani wenyeji wa Masasi Ni Wamakua na wenyeji wao Nanyumbu ni Wayao.

Kama ulikua hujui ;-Rais Benjamin William Mkapa sio mmakonde Ni Mmakua,

Wamakonde wamejipatia umaarufu mkubwa nchini Tanzania kutokana na kuwa na ukakamavu na shughuli za uchongaji wa vinyago. Tofauti kubwa kati ya Wamakonde wanaoishi Kusini mwa Mto Ruvuma (Msumbiji) na Kaskazini mwa Ruvuma (Tanzania) ni aina ya urembo wa ndonya. Wale wa Msumbiji wana ndonya ndogo juu ya midomo yao wakati wa Tanzania wana ndonya kubwa zaidi midomoni mwao.

Wamakonde huonekana kwa uzuri wao, wapo waliochanja sehemu za juu ya mdomo, masikio na uso. Inaaminika kuwa chanzo cha kuchanja, kutoboa midomo na kuweka ndonya ilikuwa kujilinda dhidi ya wafanyabiashara wa watumwa ambao walibeba watumwa kwenda kwenye mashamba huko Ulaya.

Ndonya na Chale ziliwakasirisha sana wafanyabiashara wa Kiarabu kwa kuona kuwa watu hao hawapendezi. Wamakonde wengine wa Msumbiji waliamua kuchonga meno yao, ili kujilinda, kwamba mtu ambaye angeingia katika himaya yao akiwa hajachanja, hana ndonya na hajachonga meno, walimuona ni adui yao na kama ni mweusi, ni mpelelezi wa Waarabu ili wavamie kuwachukua kwenda utumwani.

Tabia hizi zikawa ni desturi na mila zao na zikawa kama urembo ndani ya kabila la Wamakonde. Baada ya kukomeshwa kwa biashara ya watumwa, mila hizi zilianza kutoweka na wengi wameachana nazo.
Hicho unachokiona hapo Puani ndio inaitwa NDONYA Ni mti wa mpingo huchongwa na kuwekwa katika kuweka hutobolewa hadi fizi za juu yaani akicheka unauona umetokeza kwa ndani upande wa juu ya mdomo.
Makala hii imeletwa kwenu na Dhulkad Madara kutoka morogoro
Walijikosesha fursa ya kuwa black people in the New World.
 
Kwa lugha nyingine wamalaba ni wamakonde wa Pwani (Wilaya za Mtwara zinazopakana na Bahari ya Hindi)
Na wamawia ni wabara.
Hii si kweli. Ukweli ni kwamba Wamakonde walio na chale au walio na chanjo hizo ni kutoka Msumbiji na kwa Mtwara ni wahamiaji tu. Wengi wanatokea Wilaya ya Mueda kule Msumbiji jimbo la Capo Delgado. Wamakonde wa bara kwa upande wa Tanzania HAWANA chanjo na asilimia zaidi ya 99 ni Waislam[ Newala, Tandahimba na Nannyamba], hao ni tofauti na wale wenye chanjo ambao wanatokea Msumbiji na ni jamii chache[ wengi ni Wakristo, kiukweli hula kitimoto na samaki nchanga] na popote utakapowaona iwe Mtwara, Lindi, Ruvuma, basi hao wenye chanjo kiasili ni Wanamsumbiji na ni wahamiaji.
Kwa upande wa Mtwara mjini na Mrwara DC, ni ukanda wa pwani na kwa hiyo wamakonde wake ni Wamalaba[ ni kati ya Kiswahili na Kimakonde ambacho kwa ufupi ni Broken Swahili]. Hao utawapata Mtwara Municipal na Mtwara DC kama kule Dangote, kule inakojengwa bandari mpya ya Mgao, Msimbati, Madimba gas plant, Kilambo boarder, Mikindani, Naliendele, Msijute, Ziwani, Nalingu kutaja vijiji vichache.
 
Hii si kweli. Ukweli ni kwamba Wamakonde walio na chale au walio na chanjo hizo ni kutoka Msumbiji na kwa Mtwara ni wahamiaji tu. Wengi wanatokea Wilaya ya Mueda kule Msumbiji jimbo la Capo Delgado. Wamakonde wa bara kwa upande wa Tanzania HAWANA chanjo na asilimia zaidi ya 99 ni Waislam[ Newala, Tandahimba na Nannyamba], hao ni tofauti na wale wenye chanjo ambao wanatokea Msumbiji na ni jamii chache[ wengi ni Wakristo, kiukweli hula kitimoto na samaki nchanga] na popote utakapowaona iwe Mtwara, Lindi, Ruvuma, basi hao wenye chanjo kiasili ni Wanamsumbiji na ni wahamiaji.
Kwa upande wa Mtwara mjini na Mrwara DC, ni ukanda wa pwani na kwa hiyo wamakonde wake ni Wamalaba[ ni kati ya Kiswahili na Kimakonde ambacho kwa ufupi ni Broken Swahili]. Hao utawapata Mtwara Municipal na Mtwara DC kama kule Dangote, kule inakojengwa bandari mpya ya Mgao, Msimbati, Madimba gas plant, Kilambo boarder, Mikindani, Naliendele, Msijute, Ziwani, Nalingu kutaja vijiji vichache.
Asante sana mkuu.
Nashukuru kwa ufafanuzi mzuri.

Vipi kuhusu Wamakua?
 
Masasi Ni Wamakua na wenyeji wao Nanyumbu ni Wayao.

Masasi Mtwara

KANISA LENYE HISTORIA YA KUSISIMUA TANZANIA HILI HAPA MASASI MTWARA​


View: https://m.youtube.com/watch?v=rndEVqBzkEs
Edward Steere (1828–1882) alikuwa askofu mashuhuri wa Anglikana na mmisionari katika Misheni ya Vyuo Vikuu Afrika ya Kati (UMCA) ambaye alichukua jukumu muhimu katika kuanzisha vituo vya misheni katika bara la Tanzania, ikiwa ni pamoja na eneo la Masasi..

Maelezo muhimu kuhusu Askofu Steere na Masasi ni pamoja na:
  • Jukumu Lake Masasi: Ingawa Askofu Steere alikuwa na makao yake makuu Zanzibar, aliongoza misheni hadi bara. Kijiji cha watumwa walioachiliwa huru kilianzishwa Masasi mnamo Novemba 1876 chini ya usimamizi wa UMCA.
  • Kazi ya Umisionari: Askofu Steere alifanya kazi ya kuendeleza misheni ya Masasi kama kitovu cha watumwa walioachiliwa huru kuishi na kwa ajili ya maendeleo ya kilimo, akilenga jamii inayojitegemea.
  • Michango ya Lugha: Alikuwa mtaalamu wa lugha aliyesoma lugha za wenyeji, ikiwa ni pamoja na kiYao, jambo ambalo lilikuwa muhimu kwa mawasiliano na kazi ya utume katika eneo la Masasi.
  • Jitihada za Kupinga Utumwa: askofu Steere alifanya kazi kwa karibu na mvumbuzi David Livingstone na mamlaka ya Uingereza kukomesha biashara ya watumwa huko Zanzibar na kuanzisha misheni, kama vile Masasi, kama mahali salama pa kukimbilia wale walioachiliwa.
  • Kifo: Alifariki Zanzibar mwaka 1882, muda mfupi baada ya kuanzisha juhudi hizi za bara.
Kumbuka: Dayosisi ya Anglikana ya Masasi ilianzishwa rasmi baadaye, mwaka wa 1926, huku Askofu William Lucas akiwa askofu wake wa kwanza

Habari za ziada:

Steere, Edward​

1828-1882
Ushirika wa Anglikana
Malawi, Tanzania

Edward Steere alikuwa mmishonari na askofu wa Kianglikana barani Afrika. Alizaliwa London na kufundishwa awali kama wakili katika Chuo Kikuu cha London, Steere alijisomea theolojia kibinafsi kabla ya kuwekwa wakfu rasmi mwaka wa 1858. Alikuwa rafiki wa Askofu George Tozer na aliandamana naye hadi Malawi mwaka wa 1863; wakati Misheni ya Vyuo Vikuu Afrika ya Kati (UMCA) ilipoondoka Malawi mwaka uliofuata, aliandamana na Tozer hadi Zanzibar. Ingawa Steere alikuwa amekusudia kukaa kwa miaka michache tu, ugonjwa wa Tozer na kurudi kwake Uingereza vilimwacha akisimamia Zanzibar.

Alisimamia kurudi kwa misheni hiyo bara kabla ya kurudi Uingereza. Kisha akarudi Afrika na msafara wa utafutaji wa Livingstone mwaka wa 1872. Askofu aliyewekwa wakfu wa Afrika ya Kati mwaka wa 1874, alizungumza na kufanya kazi dhidi ya biashara ya watumwa na kusaidia kujenga Kanisa Kuu la Zanzibar mahali pa soko la watumwa la zamani.

Alikuwa mtaalamu mahiri wa lugha, akitoa kamusi, sarufi, na vitabu vya nyimbo katika lugha kadhaa za Kiafrika, ikiwa ni pamoja na Kiswahili na Yao, pamoja na kutafsiri Biblia nyingi kwa Kiswahili.

Kama wamisionari wengine kadhaa wa Anglikana waliotembelea Afrika, alifuata mtindo wa maisha wa upendeleo sana na alitofautisha waziwazi kati ya Ukristo na utamaduni wa Ulaya. Wakati mmoja alisema, "Hakuna mtu atakayewahi kuwa mmisionari mzuri ambaye hawezi kuwa na furaha miongoni mwa wenyeji." Alifariki Zanzibar.

T. Jack Thompson


Marejeleo​

Edward Steere, Akaunti ya Zanzibar (1870).

——-, Misheni ya Afrika ya Kati (1873).

——-, Matembezi katika Nchi ya Nyassa (1876).

——-, Matembezi katika Nchi ya Zaramo (1880).

Anne EM Anderson-Morshead, Historia ya Dhamira ya Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati, 1859-1896 (1897).

RM Heanley, Kumbukumbu ya Askofu Steere (1888).

GH Wilson, Historia ya Dhamira ya Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati (1936).


Makala haya yamenakiliwa, kwa ruhusa, kutoka kwa Kamusi ya Wasifu ya Misheni za Kikristo , hakimiliki © 1998, na Gerald H. Anderson, Kampuni ya Uchapishaji ya WB Eerdmans, Grand Rapids, Michigan. Haki zote zimehifadhiwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom