Chilojnr
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 308
- 1,354
Najua hili somo litakuwa refu sana na lisiweze kuisha hata mwaka huu. Nitajitahidi sana kuwaandikia kuhusu Wagiriki, walipoanzia mpaka sasa hivi, ni kwa namna gani waliwahi kuitawala dunia, moja ya tawala iliyokuwa na nguvu sana ukiachana na China, Warumi na hata Wamarekani ambao tunao sasa hivi.
Nitaandika mengi sana, yaani kwa kifupi ni kwamba tunaingia darasani. Kama wewe hukupenda historia tangu darasani, hapa tuache tu kwa kuwa tunazama ndani, tunachimba na kuchimbua, tukitoka hapa, utakuwa umewaelewa Wagiriki kwa undani sana, yaani ukisikia mtu anazungumzia Wagiriki, hautoshangaa, utakuwa umewajua, na utakuwa umeyajua mengi kuhusu wao kuliko hata mwanafunzi aliyeingia darasani kusoma.
Okay! Acha nianze kuwaelezea kwa undani kabisa kuhusu hawa watu. Kumbuka hili somo haliishi leo hata kesho, nyie tusomeni mpaka pale tutakapoona imetosha.
Abdera: Huu ni mji muhimu sana kule Ugiriki, upo Kaskazini mwa Pwani ya Aegean, karibu na mto wa Nestos. Abdera ilikuwa sehemu maarufu sana ya kufanyia biashara kipindi hicho cha zamani. Watu walikuwa wakitoka na meli zao sehemu mbalimbali duniani na kwenda huko kuhakikisha biashara zao zinafanyika vizuri. Yaani kwa miaka hiyo ya nyuma, sehemu hii ilikuwa ni kitovu kikubwa cha biashara.
Huu mji uligunduliwa na kabila la Herakles ambao walikuwa wakiongozwa na Abderos. Mji huu uligunduliwa mwaka 650 Kabla ya Kristo.
Mji ulidumu kwa miaka kadhaa kabla ya kuharibiwa na kabila la Thracians lakini baadaye wafanyabiashara wa watumwa hapo Ugiriki wakaujenga upya, hiyo ilikuwa ni mwaka 545 Kabla ya Kristo.
Wagiriki hao wafanyabiashara ambao waliamua kwenda kuujenga upya walitoka sehemu iitwayo Teos, mji uliokuwa Magharibi mwa Ugiriki, karibu na sehemu iitwayo Ionia.
Miongoni mwa watu waliamua kwenda kuishi mahali hapo alikuwemo dogo aliyeitwa Anacreon. Wakati huo mfalme wao aliitwa Cyrus wa Kwanza.
Kama ilivyokuwa kwa makoloni mwengine sehemu nyinginezo, Abdera ilikuwa ikifanywa biashara na watu mbalimbali ambao walikuwa wakipeleka mbao, almasi, dhahabu na hata watumwa waliokuwa wakipatikana vitani.
Baadaye mji huu ukakabidhiwa kwa Mfalme wa Persian aliyeitwa Xerxes na yeye akawa mfanyabiashara mkubwa mjini hapo ila baada ya Persian kupigwa mwaka 479 Kabla ya Kristo, mji huu ukawa mwanachama muhimu wa Athenian ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Delian League. Kwa maana hiyo Abdera ikaanza kulipa kodi kila mwaka kwa hao Dealian League.
Wagiriki wengine waliwaona hawa watu wa Abderan kuwa wajinga sana kwa sababu mji huo ulikuwa ukitoa watu wenye akili zaidi ya wawili kwa mwaka. Hii ilimaanisha nini? Kwamba kulikuwa na miji ilikuwa inajitawala yenyewe kupitia watu wenye akili, watu hawa walikuwa na uwezo wa kuziongoza serikali kimapato na kila kitu, hazikuweza kutawalika.
Sasa hawa Abderans walionekana wajinga kwa sababu hiyo tu. Walikuwa na watu wenye akili kama Protagoras na Demokritus lakini pamoja na kuwa na watu hao, bado walitawalika.
Mwaka 404 Kabla ya Kristo, Abdera ikatawaliwa na Spartans lakini baadaye walikuja kupigwa na Athens katika vita viitwavyo Peloponnesian. Hivyo baada ya hapo huu mji ukaanza kulipa ushuru na kodi zake kwa Athenian League ambao ulikuwa unaongozwa na Mfalme wa Macedonia aliyeitwa Philip wa Pili.
Abdera ikabaki kuwa chini ya utawala wa Macedonia kwa miaka 180. Katika karne ya nne, mji ukaanza kupanuka upande wa Kusini. Sasa hapo Abdera ikaanza kuwa bize kupitia bandari zake mbili, wakaingiza pesa nyingi lakini baadaye wakaja kupigwa na majeshi ya Kirumi mwaka 170 Kabla ya Kristo katika vita vya Tatu vya Macedonia. Sasa mji huo ukaanza kutawaliwa na Warumi, hivyo ushuru na kodi zote za bandari na vinginevyo vikaanza kwenda kwa hawa majamaa.
***
Akademia Ilikuwa sehemu nyingine ya kupata elimu zaidi iliyokuwa ikipatikana mbali kidogo na Mji wa Athens, sehemu hii ilikuwa inaongozwa na jamaa aliyeitwa Akademos. Katika karne ya sita, moja ya sehemu kubwa ya mazoezi huko Ugiriki ilipatikana mahali hapa.
Katika mwaka 387 Kabla ya Kristo, Plato alinunua ardhi mahali hapo na kujenga shule ya wanafilosofi ambapo baadaye ikaja kuwa chuocha kwanza kujengwa huko Magharibi. Lengo la Plato lilikuwa ni kuwafundisha viongozi wa baadaye. Hapa ndiyo tunarudi palepale nilipowaambia kipindi cha nyuma kwamba Ugiriki walipata elimu kabla ya Misri na Warumi, wao walikuwa na elimu zao, ustaarabu wao na ndiyo maana walitoa wasomi wengi waliotingisha dunia.
Wasomi hao kipindi hicho hawakulipia ada, walikuwa wakisoma bure kabisa, na walikuwa wakifundishwa kwa namna ambavyo Plato alihitaji wao wafundishwe. Walifundishwa Hisabati, mashairi na Platonic ambayo ilijulikana kama Dialectic.
Kipindi hicho ni wanafunzi wawili ndiyo walionekana kuwa na uwezo mkubwa, ambao walifaulu vizuri sana, wanafunzi hao walikuwa ni Mwanahisabati na Mwanaanga, Knidos na Mwanafilosofo Aristotle. Huyu Aristotle ndiye ambaye alionekana kuja kuwa mrithi wa Plato kama rais wa chuo hicho lakini baada ya Plato kufariki, viongozi wa chuo wakamchagua binamu yake Plato aliyeitwa Speusippus kuwa mrithi.
Baada ya kuona amezinguliwa, Aristotle akaamua kujenga chuo chake mwenyewe na kukiita Lyceum
Chini ya rais Speusippus na warithi wake, chuo chao kiliendelea kuwa na watalaamu wa Hisabati hadi Arcesilaus wa Pitane (rais kuanzia 265 mpaka 242 Kabla ya Kristo) kuanza kufundisha masomo ya Filosofa.
Baada ya Warumi kuivamia Ugiriki mwaka 146 Kabla ya Kristo), chuo hicho cha Academy kikawavutia Warumi wengi kwenda kupata elimu humo. Chuo hicho kilidumu kwa miaka 900 kabla ya Mtawala wa Christian Byzantine aliyeitwa Justinian kukifunga chuo hicho na vyuo vingine.
Itaendelea....
Nitaandika mengi sana, yaani kwa kifupi ni kwamba tunaingia darasani. Kama wewe hukupenda historia tangu darasani, hapa tuache tu kwa kuwa tunazama ndani, tunachimba na kuchimbua, tukitoka hapa, utakuwa umewaelewa Wagiriki kwa undani sana, yaani ukisikia mtu anazungumzia Wagiriki, hautoshangaa, utakuwa umewajua, na utakuwa umeyajua mengi kuhusu wao kuliko hata mwanafunzi aliyeingia darasani kusoma.
Okay! Acha nianze kuwaelezea kwa undani kabisa kuhusu hawa watu. Kumbuka hili somo haliishi leo hata kesho, nyie tusomeni mpaka pale tutakapoona imetosha.
Abdera: Huu ni mji muhimu sana kule Ugiriki, upo Kaskazini mwa Pwani ya Aegean, karibu na mto wa Nestos. Abdera ilikuwa sehemu maarufu sana ya kufanyia biashara kipindi hicho cha zamani. Watu walikuwa wakitoka na meli zao sehemu mbalimbali duniani na kwenda huko kuhakikisha biashara zao zinafanyika vizuri. Yaani kwa miaka hiyo ya nyuma, sehemu hii ilikuwa ni kitovu kikubwa cha biashara.
Huu mji uligunduliwa na kabila la Herakles ambao walikuwa wakiongozwa na Abderos. Mji huu uligunduliwa mwaka 650 Kabla ya Kristo.
Mji ulidumu kwa miaka kadhaa kabla ya kuharibiwa na kabila la Thracians lakini baadaye wafanyabiashara wa watumwa hapo Ugiriki wakaujenga upya, hiyo ilikuwa ni mwaka 545 Kabla ya Kristo.
Wagiriki hao wafanyabiashara ambao waliamua kwenda kuujenga upya walitoka sehemu iitwayo Teos, mji uliokuwa Magharibi mwa Ugiriki, karibu na sehemu iitwayo Ionia.
Miongoni mwa watu waliamua kwenda kuishi mahali hapo alikuwemo dogo aliyeitwa Anacreon. Wakati huo mfalme wao aliitwa Cyrus wa Kwanza.
Kama ilivyokuwa kwa makoloni mwengine sehemu nyinginezo, Abdera ilikuwa ikifanywa biashara na watu mbalimbali ambao walikuwa wakipeleka mbao, almasi, dhahabu na hata watumwa waliokuwa wakipatikana vitani.
Baadaye mji huu ukakabidhiwa kwa Mfalme wa Persian aliyeitwa Xerxes na yeye akawa mfanyabiashara mkubwa mjini hapo ila baada ya Persian kupigwa mwaka 479 Kabla ya Kristo, mji huu ukawa mwanachama muhimu wa Athenian ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Delian League. Kwa maana hiyo Abdera ikaanza kulipa kodi kila mwaka kwa hao Dealian League.
Wagiriki wengine waliwaona hawa watu wa Abderan kuwa wajinga sana kwa sababu mji huo ulikuwa ukitoa watu wenye akili zaidi ya wawili kwa mwaka. Hii ilimaanisha nini? Kwamba kulikuwa na miji ilikuwa inajitawala yenyewe kupitia watu wenye akili, watu hawa walikuwa na uwezo wa kuziongoza serikali kimapato na kila kitu, hazikuweza kutawalika.
Sasa hawa Abderans walionekana wajinga kwa sababu hiyo tu. Walikuwa na watu wenye akili kama Protagoras na Demokritus lakini pamoja na kuwa na watu hao, bado walitawalika.
Mwaka 404 Kabla ya Kristo, Abdera ikatawaliwa na Spartans lakini baadaye walikuja kupigwa na Athens katika vita viitwavyo Peloponnesian. Hivyo baada ya hapo huu mji ukaanza kulipa ushuru na kodi zake kwa Athenian League ambao ulikuwa unaongozwa na Mfalme wa Macedonia aliyeitwa Philip wa Pili.
Abdera ikabaki kuwa chini ya utawala wa Macedonia kwa miaka 180. Katika karne ya nne, mji ukaanza kupanuka upande wa Kusini. Sasa hapo Abdera ikaanza kuwa bize kupitia bandari zake mbili, wakaingiza pesa nyingi lakini baadaye wakaja kupigwa na majeshi ya Kirumi mwaka 170 Kabla ya Kristo katika vita vya Tatu vya Macedonia. Sasa mji huo ukaanza kutawaliwa na Warumi, hivyo ushuru na kodi zote za bandari na vinginevyo vikaanza kwenda kwa hawa majamaa.
***
Akademia Ilikuwa sehemu nyingine ya kupata elimu zaidi iliyokuwa ikipatikana mbali kidogo na Mji wa Athens, sehemu hii ilikuwa inaongozwa na jamaa aliyeitwa Akademos. Katika karne ya sita, moja ya sehemu kubwa ya mazoezi huko Ugiriki ilipatikana mahali hapa.
Katika mwaka 387 Kabla ya Kristo, Plato alinunua ardhi mahali hapo na kujenga shule ya wanafilosofi ambapo baadaye ikaja kuwa chuocha kwanza kujengwa huko Magharibi. Lengo la Plato lilikuwa ni kuwafundisha viongozi wa baadaye. Hapa ndiyo tunarudi palepale nilipowaambia kipindi cha nyuma kwamba Ugiriki walipata elimu kabla ya Misri na Warumi, wao walikuwa na elimu zao, ustaarabu wao na ndiyo maana walitoa wasomi wengi waliotingisha dunia.
Wasomi hao kipindi hicho hawakulipia ada, walikuwa wakisoma bure kabisa, na walikuwa wakifundishwa kwa namna ambavyo Plato alihitaji wao wafundishwe. Walifundishwa Hisabati, mashairi na Platonic ambayo ilijulikana kama Dialectic.
Kipindi hicho ni wanafunzi wawili ndiyo walionekana kuwa na uwezo mkubwa, ambao walifaulu vizuri sana, wanafunzi hao walikuwa ni Mwanahisabati na Mwanaanga, Knidos na Mwanafilosofo Aristotle. Huyu Aristotle ndiye ambaye alionekana kuja kuwa mrithi wa Plato kama rais wa chuo hicho lakini baada ya Plato kufariki, viongozi wa chuo wakamchagua binamu yake Plato aliyeitwa Speusippus kuwa mrithi.
Baada ya kuona amezinguliwa, Aristotle akaamua kujenga chuo chake mwenyewe na kukiita Lyceum
Chini ya rais Speusippus na warithi wake, chuo chao kiliendelea kuwa na watalaamu wa Hisabati hadi Arcesilaus wa Pitane (rais kuanzia 265 mpaka 242 Kabla ya Kristo) kuanza kufundisha masomo ya Filosofa.
Baada ya Warumi kuivamia Ugiriki mwaka 146 Kabla ya Kristo), chuo hicho cha Academy kikawavutia Warumi wengi kwenda kupata elimu humo. Chuo hicho kilidumu kwa miaka 900 kabla ya Mtawala wa Christian Byzantine aliyeitwa Justinian kukifunga chuo hicho na vyuo vingine.
Itaendelea....