Hebu mélèze huyu mtu maana akatoa kichefuchefu n'a maandishi yake y'a uchochezi.Dogo acha ujuaji.
CCM ni chama tawala na haijawahi kumkamua mtu damu.
CCM ni chama kinachotoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi na nchi jirani.
Wewe upo hapa nchini salama, ni moja ya matunda ya CCM na Serikali yake.
Swala la shida ya wananchi ni swala mtambuka na hata huko marekani kuna maskini na Ombaomba pia wapo.
Elimu bora kwa wananchi ni moja ya nyenzo ya kumkomboa mwananchi na hali ya umaskini, lakini sio kila mwananchi anauwezo wa kuipata elimu bora kwa wakati sahihi.
Kama huko Rwanda Serikali na wananchi wake wana maendeleo ya kiwango bora, basi ni swala la kujivunia na tutapenda kujifunza toka kwenu hayo mafanikio mliofikia.
Siasa za vyama vingi hapa nchini bado changa na bado zinakua.
Unaruhusiwa kujiunga au kushabikia chama cha upinzani lakini sio kwa ghalama ya kukikashifu chama tawala CCM ambacho kilikuwepo kabla ya Siasa ya vyama vingi hapa nchini.
Hao maraisi wenu mnaowasifia wamepata mafunzo ya aina moja au nyingine hapa nchini wakigharimiwa na serikari ya CCM na wanaiheshimu.
Ndugu zenu wakimbizi wana hifadhiwa hapa nchini na wengine kupewa uraia kamili kwa maridhio ya Sera ya serikali ya CCM.
Endelea kuchambua mada iliyopo hapa Jukwaani, lakini sio kwa ghalama ya kukiponda Chama Cha Mapinduzi.
Kama unavutiwa na nyanja ya siasa unaruhusiwa kujiunga na chama chochote na kugombea uongozi.
Ila ujue CCM ndio chama tawala na kimepewa ridhaa ya kuongoza nchi na Watanzania.
Kamwe CCM haijawahi kuwa na Sera ya kuwatesa raia wake walioipigia kura.