Yenga08
JF-Expert Member
- Jul 7, 2019
- 458
- 894
Habari zenu wana janvi..,
Nilimaliza chuo mwaka 2009 na kuanza kutafuta kazi.., ilinichukua mda mrefu sana bila kupata kazi mpaka ikafikia hatua yakukata tamaa juu ya kuajiliwa. Maana nilipoteza mda mwingi sana kutafuta ajira kitu ambacho huwa najilaum sana mpaka leo.
Huwa nakumbuka Interview moja hivi ilikuwa kwa ajili ya kazi za uhamiaji., daaah nikikumbuka huwa nacheka sana. Nadhani wengi mnaikumbuka hiyo mambo ilivyokuwa., hiyo ngoma tuliifanyia uwanja wa taifa written na ilikuwa na raia nyomi. Nakumbuka selection ilitoka watu kwenda Oral, na hatimaye kuitwa kazini. Lakini baadae ilikuja kuonekana mchakato haukufuata taratibu na ajira hizo au waajiliwa hao walifutwa na mchakato kusemekana utaanza upya ila sijuwi kama ulianza au laah.
Na mara ya mwisho kuacha kutuma maombi ya kazi ilikuwa kazi za TRA, hiyo ngoma ilikuwa na nafasi nyiingi sana na raia walikuwa wengi sana maana kulikuwa na vituo vya kupigia paper Dar na mikoani. Wanaokumbuka yalikuwepo mpaka maswali yanayohusu mapendekezo ya kamati ya makinikia, pamoja na swali linalouliza kuhusu AGoA yaani daaah ni sheeda.
Nakumbuka mi nilipata maksi 65 na waliochukuliwa kwenda kwenye Oral ilianzia maksi 67 yaani niliumia kinouma, kuanzia hapo nikaamua kuacha kupambana na kazi za kuajiliwa yaani nikaacha kabisa kuwa naomba kazi.
Mnamo mwaka 2017 mwishoni nilikopeshwa kiasi flani cha pesa nikaanza biashara, ila kwa bahati mbaya sana biashara haikufana na mtaji ukawa umekata na kuambulia madeni., ila hapa tatizo lilikuwa ni yule mwenyeji wangu juu ya hiyo biashara "Usimuamini mtu"
Nilikaa nikawaza sana nin cha kufanya, maana kazi ya kuajiliwa bilabila, biashara nayo imebuma., ila mwisho wa siku nikaamua kuwa mkulima. Kutokana na maelezo ya watu tofautitofauti niliamua kulima vitunguu na Mungu alibariki nikapata gunia za kutosha tu, changamoto ikawa ni soko yaani wapi pa kuuzia huo mzigo.
Kwa bahati mbaya sana kwa msimu ule mwaka 2018 kitunguu ilikuwa nyingi sana,
Mpaka kufikia hatua ya kitunguu kinunuliwa kwa shilinhi 25000 kwa gunia ikiwa shambani. Na ukijiuliza usafirishe unakosa pakuipeleka na mwisho wa siku nikaamua kuiuzia shambani na kupata kiasi kidogo cha pesa. Kwa wanaopafahamu Igunga mkoa wa Tabora kijiji cha Bukama ndiko nilipokuwa nimelimia.
Baada ya hapo nilikodisha shamba la kulima mpunga kwa msimu wa mwaka huo huo 2018 mkoa wa Simiyu. Kulima nilifanikiwa nikalima ekali tatu, ila kwa bahati mbaya nvua hazikutosha na matokeo yake sikuweza kuvuna hata debe ndani ya hizo ekali tatu. Kwa mda wote huo nimekuwa kama mwana kijiji na vyeti kuamua kufukia kabisa na hakuna tena kuviwaza maana niliamua kupambana Plan B baada ya kuona Plana A kusoma na kuajiliwa imefeli.
Mwaka 2019 niliunganishwa kwa jamaa flani hivi huko Wilaya ya Kahama, jamaa nimfanya biashara wa nafaka nikawa kama moja ya vijana wake wa kwenda porini, yeye anawagawia pesa mnaenda vijijini kukusanya mazao mnakuja kumuuzia yeye kwa bei itakayokuwepo au akulipe 2000 kwa gunia kama ujira wako.., maana jamaa huwa ni agent wa wafanyabiashara wakubwa.
Kiukweli jamaa alikuwa yupo pouwa sana na ananetwork kubwa juu ya nafaka, tulianza mwezi wa pili Choroko, mwezi wa tatu Karanga na Alizeti, mwezi wa nne Mpunga, Alizeti na Karanga na mwezi wa sita na kuendelea mpaka mwezi wa kumi ni Dengu na mbaazi.
Mwaka huo huo wa 2019 nililima tena mpunga ekali tatu, na Mungu alibariki nvua zilikuwa nyingi nikafanikiwa kupata gunia 60 za mpunga na hapo ndio nikaanza kupata mwanga na mwelekeo Mzuri wa maisha.
Inaendelea..,
Nilimaliza chuo mwaka 2009 na kuanza kutafuta kazi.., ilinichukua mda mrefu sana bila kupata kazi mpaka ikafikia hatua yakukata tamaa juu ya kuajiliwa. Maana nilipoteza mda mwingi sana kutafuta ajira kitu ambacho huwa najilaum sana mpaka leo.
Huwa nakumbuka Interview moja hivi ilikuwa kwa ajili ya kazi za uhamiaji., daaah nikikumbuka huwa nacheka sana. Nadhani wengi mnaikumbuka hiyo mambo ilivyokuwa., hiyo ngoma tuliifanyia uwanja wa taifa written na ilikuwa na raia nyomi. Nakumbuka selection ilitoka watu kwenda Oral, na hatimaye kuitwa kazini. Lakini baadae ilikuja kuonekana mchakato haukufuata taratibu na ajira hizo au waajiliwa hao walifutwa na mchakato kusemekana utaanza upya ila sijuwi kama ulianza au laah.
Na mara ya mwisho kuacha kutuma maombi ya kazi ilikuwa kazi za TRA, hiyo ngoma ilikuwa na nafasi nyiingi sana na raia walikuwa wengi sana maana kulikuwa na vituo vya kupigia paper Dar na mikoani. Wanaokumbuka yalikuwepo mpaka maswali yanayohusu mapendekezo ya kamati ya makinikia, pamoja na swali linalouliza kuhusu AGoA yaani daaah ni sheeda.
Nakumbuka mi nilipata maksi 65 na waliochukuliwa kwenda kwenye Oral ilianzia maksi 67 yaani niliumia kinouma, kuanzia hapo nikaamua kuacha kupambana na kazi za kuajiliwa yaani nikaacha kabisa kuwa naomba kazi.
Mnamo mwaka 2017 mwishoni nilikopeshwa kiasi flani cha pesa nikaanza biashara, ila kwa bahati mbaya sana biashara haikufana na mtaji ukawa umekata na kuambulia madeni., ila hapa tatizo lilikuwa ni yule mwenyeji wangu juu ya hiyo biashara "Usimuamini mtu"
Nilikaa nikawaza sana nin cha kufanya, maana kazi ya kuajiliwa bilabila, biashara nayo imebuma., ila mwisho wa siku nikaamua kuwa mkulima. Kutokana na maelezo ya watu tofautitofauti niliamua kulima vitunguu na Mungu alibariki nikapata gunia za kutosha tu, changamoto ikawa ni soko yaani wapi pa kuuzia huo mzigo.
Kwa bahati mbaya sana kwa msimu ule mwaka 2018 kitunguu ilikuwa nyingi sana,
Mpaka kufikia hatua ya kitunguu kinunuliwa kwa shilinhi 25000 kwa gunia ikiwa shambani. Na ukijiuliza usafirishe unakosa pakuipeleka na mwisho wa siku nikaamua kuiuzia shambani na kupata kiasi kidogo cha pesa. Kwa wanaopafahamu Igunga mkoa wa Tabora kijiji cha Bukama ndiko nilipokuwa nimelimia.
Baada ya hapo nilikodisha shamba la kulima mpunga kwa msimu wa mwaka huo huo 2018 mkoa wa Simiyu. Kulima nilifanikiwa nikalima ekali tatu, ila kwa bahati mbaya nvua hazikutosha na matokeo yake sikuweza kuvuna hata debe ndani ya hizo ekali tatu. Kwa mda wote huo nimekuwa kama mwana kijiji na vyeti kuamua kufukia kabisa na hakuna tena kuviwaza maana niliamua kupambana Plan B baada ya kuona Plana A kusoma na kuajiliwa imefeli.
Mwaka 2019 niliunganishwa kwa jamaa flani hivi huko Wilaya ya Kahama, jamaa nimfanya biashara wa nafaka nikawa kama moja ya vijana wake wa kwenda porini, yeye anawagawia pesa mnaenda vijijini kukusanya mazao mnakuja kumuuzia yeye kwa bei itakayokuwepo au akulipe 2000 kwa gunia kama ujira wako.., maana jamaa huwa ni agent wa wafanyabiashara wakubwa.
Kiukweli jamaa alikuwa yupo pouwa sana na ananetwork kubwa juu ya nafaka, tulianza mwezi wa pili Choroko, mwezi wa tatu Karanga na Alizeti, mwezi wa nne Mpunga, Alizeti na Karanga na mwezi wa sita na kuendelea mpaka mwezi wa kumi ni Dengu na mbaazi.
Mwaka huo huo wa 2019 nililima tena mpunga ekali tatu, na Mungu alibariki nvua zilikuwa nyingi nikafanikiwa kupata gunia 60 za mpunga na hapo ndio nikaanza kupata mwanga na mwelekeo Mzuri wa maisha.
Inaendelea..,