Historia ya kesi inayomkabili Tundu Lissu

Historia ya kesi inayomkabili Tundu Lissu

Mjusi Sharobalo

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2025
Posts
8,264
Reaction score
14,502
Sehemu ya kwanza - Tundu Lissu alikamatwa Aprhli 9, 2024, Mimba na kupelekwa Dar es salaamu, siku iliyofuata, Aprili 10, 2024, alishitakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Lissu alipinga hatua hii akisema ni kinyume cha sheria, kwa sababu sheria inataka mashitaka yapelekwe kama hatua za kisheria za kukamata mtu na kesi iendelee katika mahakama yenye mamlaka halali.

Nyaraka za mwenendo wa kesi hazikukamilika kikamilifu, nyaraka zilizo tolewa zenye mapungufu ziliibua pingamizi la Lissu, kwa mfano, alipatiwa nyaraka za Agosti 18, 2025, ambazo ni page 116 badala ya page 103 za mchakato mzima, jambo ambalo alidai linaonesha mapungufu na makosa yanayoweza kumzuia haki na kutikisa haki za kisheria.

Lissu anaamini kuwa makosa hayo yanahusiana na mamlaka ya Mahakama ya Kisutu yanazuia hata Mahakama Kuu kuendelea na shauri bila kuangalia pingamizi lake. Inaendelea...
 
Sehemu ya Pili - Anakabiliwa na shitaka la uhaini kinyume na sheria kifungu cha 39(2)(d) cha sheria ya kanuni za Adhabu, kilichotokana na maneno aliyotamka yanayohusiana na mpango wa kuthibiti au kuzuia uchaguzi Mkuu wa 2025. Mashitaka haya yamevutia umakini mkubwa wa umma na vyombo vya habari, huku wananchi wengi wakisubili kwa hamu uamuzi wa Mahakama kuu: Kuachiwa huru au kuendelea kusota rumande, jambo linaloangaliwa kuwa na athari kubwa kisiansa na kisheria nchini Tanzania. Mwisho...
 
Back
Top Bottom