chamilo nicolous
JF-Expert Member
- Mar 10, 2016
- 1,991
- 1,364
Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete amepewa Tuzo leo kwa ajili ya nini na kazi ipi aliyofanya inayohusiana na bwawa la JNHPP?
Mradi wa JNHPP, SGR, Ikulu ya Chamwino n.k yote yalikuwa maono ya Mwalimu Nyerere. Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete amekaa Ikulu ya Dar es Salaam miaka 10, hakupoteza muda wake kuijenga Ikulu ya Chamwino, SGR hakuanzisha na wala hakuacha mkakati wowote wa kulijenga bwawa la JNHPP, sasa je leo kapewa Tuzo kwa kazi ipi aliyofanya kwenye mradi huu?
Miradi yote ya kimkakati iliyokuwa kwenye ndoto za baba wa Taifa letu imetekelezwa na hayati Dr. John Pombe Magufuli na hivyo Tuzo ya heshima (Exceptional Award) ilitakiwa iende kwa hayati Magufuli na siyo Kikwete.
Unajua mtabishana na sisi ila ukweli unabaki wazi kuwa Marais exceptional kwenye Taifa letu ni wawili nao ni Mwalimu Nyerere na John Magufuli. Simaanishi wengine hawakufanya kazi ila kazi yao haina maajabu kwa Taifa.
Hakuna kipindi ambacho Taifa letu liliingia katika mgawo wa umeme kama kipindi Mzee Kikwete akiwa Rais, Magufuli alipoingia madarakani mgawo ukaisha na akaanzisha ujenzi wa JNHPP. Maswali yangu ni je;
1. Rais Kikwete hakujua kuwa Watanzania wanateseka na adha ya umeme?
2. Je, alikuwa hajui kuwa kwenye makabrasha aliyoacha Mwalimu Nyerere ipo ndoto ya kujenga mradi mkubwa wa umeme wa JNHPP?
3. Swali la mwisho ni je, Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete amepewa Tuzo ya nini na kwa kazi ipi aliyofanya yenye mahusiano na mradi wa JNHPP?
Mradi wa JNHPP, SGR, Ikulu ya Chamwino n.k yote yalikuwa maono ya Mwalimu Nyerere. Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete amekaa Ikulu ya Dar es Salaam miaka 10, hakupoteza muda wake kuijenga Ikulu ya Chamwino, SGR hakuanzisha na wala hakuacha mkakati wowote wa kulijenga bwawa la JNHPP, sasa je leo kapewa Tuzo kwa kazi ipi aliyofanya kwenye mradi huu?
Miradi yote ya kimkakati iliyokuwa kwenye ndoto za baba wa Taifa letu imetekelezwa na hayati Dr. John Pombe Magufuli na hivyo Tuzo ya heshima (Exceptional Award) ilitakiwa iende kwa hayati Magufuli na siyo Kikwete.
Unajua mtabishana na sisi ila ukweli unabaki wazi kuwa Marais exceptional kwenye Taifa letu ni wawili nao ni Mwalimu Nyerere na John Magufuli. Simaanishi wengine hawakufanya kazi ila kazi yao haina maajabu kwa Taifa.
Hakuna kipindi ambacho Taifa letu liliingia katika mgawo wa umeme kama kipindi Mzee Kikwete akiwa Rais, Magufuli alipoingia madarakani mgawo ukaisha na akaanzisha ujenzi wa JNHPP. Maswali yangu ni je;
1. Rais Kikwete hakujua kuwa Watanzania wanateseka na adha ya umeme?
2. Je, alikuwa hajui kuwa kwenye makabrasha aliyoacha Mwalimu Nyerere ipo ndoto ya kujenga mradi mkubwa wa umeme wa JNHPP?
3. Swali la mwisho ni je, Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete amepewa Tuzo ya nini na kwa kazi ipi aliyofanya yenye mahusiano na mradi wa JNHPP?