Historia, sababu na Hati za Muungano Tumeona moja nyingine ya Zanzibar iko wapi?

kibogo

JF-Expert Member
Apr 1, 2012
9,739
4,732
HISTORIA YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliundwa mnamo tarehe 26 Aprili,1964 kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (inayojumuishaVisiwa vya Pemba na Unguja). Tanganyika ilikuwa ni mwendelezo wakoloni la Ujerumani, utawala wa Waingereza kwa Mamlaka ya Umoja wa Mataifa, Himaya ya Umoja wa Mataifa chini ya utawala wa Uingereza na mwisho Taifa huru kuanzia mwaka 1961 ndani ya nchi za Jumuiya ya Madola Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ziliingia mkataba wa Muungano mnamo mwaka 1964 na kuanzishwa Dola ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mkataba huu wa Muungano ulitiwa saini na aliyekuwa Rais wa Tanganyika, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume tarehe 22 Aprili 1964 huko Zanzibar. Mkataba huo ulithibitishwa na Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi hapo tarehe 26 Aprili, 1964 na mnamo tarehe 27 Aprili, 1964, viongozi wa nchi zote mbili walikutana katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam na kubadilishana Hati za Muungano. Sheria za Muungano zilitoa tamko la Jamhuri ya Muungano katika Ibara ya 4 kwamba:"Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar zitalazimika,baada ya kuungana na siku zote baada ya kuungana, kuunganishwa kuwa Dola ya Jamhuri kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar' (Ibara ya 4 Sheria za Muungano)

swali langu linasimamia hapo nilipoweka Blue.

Kwa urefu unaweza kusoma hii attachment:


 

Attachments

  • Historia ya Muungano_2.pdf
    102.8 KB · Views: 120
Back
Top Bottom