Historia fupi ya waasisi wa mataifa ya Africa

NostradamusEstrademe

JF-Expert Member
Jul 1, 2017
3,032
4,028
Kuanzia leo nakuendelea nitakuwa nawaletea majina ya mataifa ya Afrika alphabetically na historia ya waasisi wa mataifa hayo.

1.ALGERIA.
Ahmed Ben Bella alizaliwa 25 Dec 1916 alimuoa Zohra Sellani
alikuwa mwana siasa,mjamaa, askari,mwanamapinduzi alikuwa ndio raisi wa kwanza wa Algeria mwaka 1963-1965.
Alizaliwa sehemu inaitwa Maghnia kipindi cha utawala wa kifaransa,mtoto wa mkulima.Alihuhudhuria shule Ufaransa huko ndiko akaja gundua ubaguzi mkubwa kwa waarabu toka kwa walimu wake wa kifaransa.Alianza kulalamika na kukandia hali hiyo ya ubeberu na ukoloni na alipinga utamaduni wa kigeni kwa taifa lake na mara moja akaanza kushiriki harakati za utaifa.
Alijitolea kwenye jeshi la Ufaransa mwaka 1936.Alipigana vita vya pili vya dunia upande wa mfaransa.
Hata hivyo watawala walimuona ni mwiba mchungu wakatuma muuaji kwenda kumuua kwenye shamba lake.Jaribio hilo liliposhindikana wakaamua kutaifisha shamba lake.
Aliunda chama cha (OS) Organizationale Speciale kwa madhumuni ya kuchukua silaha dhidi utawala dhalimu wa kifaransa.
Hii ilileta kuundwa kwa NLF National Liberation Front mwaka 1949.
Alivunja bank mji wa Oran ili apate fedha za kuendesha chama lakini alikamatwa na kupelekwa gereza la Bilda mwaka 1951 na kuhukumiwa miaka 8.Alifanikiwa kutoroka na kukimbilia Tunisia mwishowe akafika Cairo mwaka 1952.
Vita vya Algeria vilipoanza 1954 alikuwa makazi yake ni Cairo akiwa ni mmoja wa wanachama wa kamati ya umoja kitendo ambacho kilikuja kuzaa (FLN) Front de Liberation Nationale ambapo kilizaliwa November mwaka huo.
Nia ya kumuua bado mabeberu walikuwa nayo mwaka 1956 alipokea kifurushi kutoka kwa driver tax akiwa hotelini Cairo akakataa kukipokea dereva alipoondoka tu na kifurushi hicho bomu likalipuka na kumuua dereva.Baadae akiwa hapo hapo hotelini Cairo alikuja mtu na bunduki akafyetua risasi haikumuua ila ilimjeruhi kidogo lakini mshika bunduki huyo aliuwawa na walinzi akijaribu kutorokea mpaka wa Libya.
Alikuwa anaunga mkono harakati nyingi za kudai uhuru kwa mataifa mengine.Ikumbukwe Mandela alipitia hapa Tanzania akaacha viatu vyake Dar akaelekea Algeria kupata mafunzo ya kijeshi kupambana na Makaburu ndipo aliporudi akafungwa maisha.
Ben Bella pia alikutana na Fidel Castrol na Che Guevara Havana Cuba mwaka 1962.Pia alikuwa anaungwa mkono na Pakistani.
Alichaguliwa kuwa raisi wa kwanza wa Algeria mwaka 1963.
Alipinduliwa na mkuu wake wa jeshi Boumedienne mwaka 1965.
Alifariki 11 April 2012
Somo lijalo tutaangalia nchi ya BENIN
Itaendekea
Screenshot_2020-02-04-20-37-37-1.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
2.ANGOLA.
Anto'nio Agostinho Neto alizaliwa tarehe 17 September 1922.Alìkuwa daktari,mwanafasihi na mwanasiasa alikuwa ndio raisi wa kwanza wa Angola.Ndiye aliyekuwa kiongozi wa chama cha MPLA-Movimento Popular de Libertacao de Angola.Popular movement for liberation of Angola.Na ndiye aliyeongoza vita vya uhuru 1961-1974.
Mkewe anajulikana kama Maria Eugenia alimuoa mwaka 1957.
Alizaliwa Icolo Bengo jimbo Bengo na alisoma secondary ya juu mjini Luanda.
Wazazi wake walikuwa walimu na methodists baba yake alikuwa kasisi wa kanisa la Methodist.
Baada ya kumaliza shule alifanya kazi katika sekta ya afya katika utawala wa wareno kabla ya kwenda chuo kikuu
Aliondoka Angola kwenda Ureno kusoma udaktari chuo kikuu cha Coimbra na Lisbon.
Chuoni alichanganya masomo na siasa chini ya chama PIDE.
Alishikiliwa na waziri mkuu Salazar mwaka 1951kwa miezi mitatu kutokana na shughuli zake za kisiasa.
Alishikiliwa tena mwaka 1952 kwa kujiunga kwake na chama cha kidemokrasia cha vijana wa kireno.Akakamatwa tena mwaka 1955 akashikiliwa hadi 1957.
Alimaliza masomo yake na kumuoa mwanamke wa kireno Maria Eugenia da Silva siku hiyo hiyo anahitimu.
Alirudi Angola mwaka 1959 na kushikiliwa mwaka 1960 na kutoroka kwenda kukamata hatamu za kuongoza mapambano ya kijeshi.
Vyama vya PCA na PLUA viliungana na kutengeneza MPLA Neto akiwa kiongozi wake.
Alishikiliwa tarehe 8th June 1960.Wafuasi wake waliandamana kutoka Bengo hadi Catete kupinga lakini walizuiliwa na askari wa kireno kitendo ambacho waliuwawa watu 30 na wengine 200 kujeruhiwa tukio hili lilibatizwa jina la Mauaji ya Icolo e Bengo.
Baada ya hapo Neto alipelekwa kizuizini huko Cape Verde.Baadae alipelekwa jela Lisbon Ureno.Baada ya shinikizo la mataifa mbali mbali aliachiwa lakini kipindi hiki alipewa kifungò cha house arrest.Alifanikiwa kutoroka na kutorokea Morocco baadae akaenda Congo Leopodville.
Mwaka 1962 aliwasili Washington DC na kuuomba utawala wa raisi Kennedy kusaidia lakini alipigwa chini maana marekani walikuwa wanautamani utajiri wa mafuta wa Angola.
Neto alikutana na Che Guevara mwaka 1965 baada ya hapo akaanza kupata misaada kutoka Cuba.Alishakwenda Havana Cuba mara nyingi kwa sababu yeye na Castrol walikuwa wana Ideology moja.
Angola ilipata uhuru wake mwaka 1975 na yeye akawa raisi wa kwanza wa Angola huru.Alianzisha mfumo wa chama kimoja cha siasa serikali yake ilikuwa karibu na serikali ya Usoviet ya warusi na mataifa ya mrengo wa kimashariki kama Cuba.
Mwaka 1973 alipokuwa matembezi ya kawaida Bulgaria alikutana na Mwanamke mmoja aliyemzaliaga mtoto Mihaela Radkova Marinova aliyekuwa anatunzwa nyumba ya watoto yatima huko Bulgaria.Familia ya Neto haikupata kumtambua mpaka mwaka 2013 vipimo vya DNA vilipoonyesha ni mtoto wa Neto kwa 95%
Alifariki 10 September 1979 akiwa kwenye matibabu ya ugonjwa wa cancer na hepatitis huko urusi.
Legacy
1.Chuo kikuu cha serikali ya Angola kinaitwa Neto
2.Airport ya Cape Vede inaitwa Neto.
3 . hospitali kuu ya nchi ya Cape Verde inaitwa Neto iliitwa hivyo kutokana na msaada wa kitabibu aliotoa kwao.
4.Huko Belgrade Serbia kuna mtaa unaitwa Neto.
List ya maraisi wa Angola hadi sasa.
1.DR Anto'nio Agostinho Neto.
2.Jose Eduardo Dos Santos
3.Joao Lourenco



Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom