Hili tangazo liko sawa kweli?

Hili tangazo liko sawa kweli?

Cardinal06

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2015
Posts
963
Reaction score
327
Kuna tangazo huwa linarushwa ITV kabla ya taarifa ya saa mbili usiku, tangazo hili linahusu Uzazi mpango, tatizo langu sio katika ujumbe wa tangazo hili bali ni wahusika waliotumika. Wametumika watoto wadogo ambao wana'act kama wapiga kampeni na wanataka kuwaambia wazazi watumie Uzazi wa mpango.

Wadau hii ni sawa? Mtoto- hasa wa umri kama uliotumika katika tangazo hili- amshauri mzazi kuhusu uzazi?
 
hata mimi nimeshangaa kwanini watoto watumike sababu wanaofanya uzazi wa mpango ni mama zao
 
Sijui ndo utandawazi... Ila kiukweli hilo tangazo mimi binafsi likionyweshwa huwa naona aibu pale mtoto anaposema uzazi wa mpango... BTW idea yao ni nzur
 
Sijui ndo utandawazi... Ila kiukweli hilo tangazo mimi binafsi likionyweshwa huwa naona aibu pale mtoto anaposema uzazi wa mpango... BTW idea yao ni nzur

Tatizo sio ujumbe bali huo ujumbe unafikishaje
 
Pale wamebugi, wale watoto hawana nafasi katika hilo tangazo,
mimi silielewi coz in reality wale watoto hawajui nini maana ya uzazi wa mpango.
 
wamechemka tangazo aibu hivi watu kwann sio creative jamani..yani kero sana
 
Kwani hao watoto wanakadiriwa kuwa na umri gani? Wengine hatuna access na hicho kituo kilichotajwa
 
Pale wamebugi, wale watoto hawana nafasi katika hilo tangazo,
mimi silielewi coz in reality wale watoto hawajui nini maana ya uzazi wa mpango.
Tangazo liko sawa tatizo ni nyinyi wenye tafsiri potofu. Mbona matangazo kama hayo yapo mengi tu mfano lile la watoto wachanga kuhamasishana kwenda kupima HIV. Au unadhani uzazi wa mpango ni kondomu tu? Tangazo linamhusu mtoto pia maana na yeye anahitaji afya bora, elimu bora, maisha bora, nk. Sasa bila mzazi kuzaa kwa mpango watoto watayapataje hayo?
 
Kumbe wengi tumeona! Mimi mwenyewe halinibariki kabisa, mini mtoto mdogo namna hiyo akashiriki mambo ya Uzazi wa mpango? Iwapo tu masuala ya Uzazi hufunfundishwa darasa LA saba na kidato cha Tatu nakuendelea. Kweli wamebugi na ningeomba wabadilishe wahusika.
 
Ni sawa linaonesha kiwango cha ubnafsi tulicho nacho kuwafanyisha kazi watoto zilizo juu ya uwezo wao
 
Back
Top Bottom