Hili nalo ni tatizo

MTU KAZI

Member
Joined
Mar 25, 2014
Posts
85
Reaction score
31
Kusema ukweli nawapenda sana wanawake na huwa ndio rafiki zangu wakubwa mno,hubadilishana nao hili na lile ili kufikia malengo ya maisha. Lakini kwa wanawake huwa sivutiwi kabisa na maswala au tabia hizi:

1 kuunganisha nywele za bandia,

2 kuvaa vinguo vidongo vidogo ama visiketi vifupi kiasi cha kuacha 3\4 ya mwili wao wazi,

3 kuvaa nguo za kiume ama suruali za kubana kiasi cha kuchora umbo lote.

Lakini yote kwa yote kilicho nifanya niweke uzi huu sio mambo hayo ila ni hili;

yaani binti aliyesoma kiasi fulani akajua Kiingeleza japo si kwa wote ila kiukweli wanakera sana kwenye mapenzi.

Achana na kejeli walizo nazo, hivi ni kweli hamna maneno ya mahaba katika lugha ya Kiswahili ambayo yanaleta hamasa na kujenga upendo mpaka tuchanganye na Kiingereza kilicho vunjika vunjika.Utasikia; Hi baby,honey,sweet...n.k.

Jambo la kujiuliza kama ni majina ya huba katika lugha yetu ya KISWAHILI mbona yapo tu, mfana mahabuba, laazizi,mpenzi,malkia n.k. Tukithamini kiswahili katika weledi huu.
 
Sio kwamba ninalangu ila najalibu kuangalie upande wa hili tatizo,ama kunasehem nimekosea?

hujakosea lakini hao rafiki zako wanafanya hayo kwa utashi wao mradi hawavunji sheria
 
Happy fathers day! Kwa design hii i officially lounch BRING BACK OUR FATHERS
 
Hahahaha, nna rafiki aliwai kuniambia sifa za mwanaume anaemtaka, kujua kingereza ni mojawapo.
 

"Shule" imewafanya wengi sana kuwa wapumb.vu .....!!
 
Mmmh! Utakuwa mwalimu wa kiswahili wewe!!!
 
Aisee...mbona hata wanaume wanatumia hayo maneno
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…