Hili la wageni kuuziwa ardhi unalichukuliaje?

Konda wa bodaboda

JF-Expert Member
Jul 18, 2014
7,981
4,169
Jana kuna mada iliwekwa hapa jf kuhusu Lukuvi kukataa hongo ya bilioni 5 kutoka kwa wawekezaji waliotaka kuiuzia serikali ardhi kwa shilingi milioni mia moja na zaidi kwa ekari ambazo waliuziwa na wananchi kwa shilingi milioni tano kwa ekari moja. Je huo ndio uwekezaji kweli? Kwanza hao wawekezaji waliouziwa ardhi hadi ekari 400 waliuzuwa kwa kazi gani?

Kuna mdau mmoja hapa jf aliwahi kusema kuna kijiji morogoro ambacho mwekezaji amekinunua chote! Mwekezaji kununua kijiji kizima kwa kazi uwekezaji gani?

Binafsi nina mashaka na nia za hawa tunaowaita wawekezaji, na matunda ya kuwauzia ardhi tutakuja kuyaona baadae/muda si mrefu.
 
Sera na sheria za umiliki wa ardhi zinatakiwa kufanyiwa marekebisho ili ardhi isiuzwe kwa wageni. Majirani zetu Rwanda, burundi, uganda na malawi wana ardhi ndogo, sasa tukizubaa tutashangaa raia wao wanahamia kwetu kwa sababu ya uhaba wa ardhi kwenye nchi zao, kwa sababu wanajua Tanzania ina ardhi kubwa na wageni wanaruhusiwa kununua.
 
Sheria ya ardhi hairuhusu mgeni kumiliki ardhi isipokua kwa lengo la kuwekeza tu, na kibali hupatikata TIC, isipokua kuna namna mianya hutumika kwa wageni kumiliki ardhi kupitia ubia na wenyeji (partnership/jointventure)hiyo inakua rahisi kwao. Yeye anakua mpangaji tu katika mojawapo ya hivi vipindi vi 3, miaka 33,66 au 99,
 
Kwa kweli hili la ardhi kuuzwa kwa wageni ni hatari. Viongozi wa vijiji walirubuniwa na kukubali kuuza maelfu ya eka kwa wawekezaji wababaishaji. matokeo yake yapo mapori mngi tu hayajaendelezwa huku wananchi hawana ardhi.
 
Kuna wasomali wananunua ardhi nabkujenga na kuuza. Ukiwauliza wanakudanganya wanatoka Bahi au Tabora. Wakati kiswahili hawajui kabisa. Tunakazi ya ziada nchi hii
 
Kuna wasomali wananunua ardhi nabkujenga na kuuza. Ukiwauliza wanakudanganya wanatoka Bahi au Tabora. Wakati kiswahili hawajui kabisa. Tunakazi ya ziada nchi hii
Kuna raia wa nchi jirani wanajitambulisha kama wenyeji wa mkoa wa kigoma na kagera nao hawa nina wasiwasi nao sana maana ni wengi sana.
 
Tanzania ndio nchi pekee mgeni haswa akiwa mwafrika rahisi kujichanganya na kujidai raia wa hapa.
Kuna wacongo wengi wamejinadi kama wamanyema na kuhodhi haki za raia wa tz ikiwemo passport etc

What does it take to clear this problem. Wajaluo,Wazambia,malawi,kenyans,waganda,indians etc

Kuna binti mmoja ni mzambia amrajiriwa precision air na huwa anajidai ni mtanzania sababu tu anajua sana kiswahili na kasoma chuo hapa.
 
Tanzania ndio nchi pekee mgeni haswa akiwa mwafrika rahisi kujichanganya na kujidai raia wa hapa.
Kuna wacongo wengi wamejinadi kama wamanyema na kuhodhi haki za raia wa tz ikiwemo passport etc

What does it take to clear this problem. Wajaluo,Wazambia,malawi,kenyans,waganda,indians etc

Kuna binti mmoja ni mzambia amrajiriwa precision air na huwa anajidai ni mtanzania sababu tu anajua sana kiswahili na kasoma chuo hapa.
Yaani unachosema ni kweli kabisa, yaani mtu akichanganya miaka mitatu tu anakuwa mtanzania.
 
Back
Top Bottom