Hili la kuchimba dawa Mwakyembe hajajipanga

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
images


WAZIRI wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, aliliambia Bunge kuwa kuanzia Septemba mosi mwaka huu, itakuwa ni marufuku kwa mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi kusimama vichakani ili abiria wao wajisaidie haja kubwa na ndogo maarufu kama ‘kuchimba dawa’. Mwakyembe alitoa agizo hilo mwezi uliopita wakati akihitimisha hotuba ya bajeti ya mapato na matumizi ya wizara yake na kueleza madhara yanayotokana na vitendo hivyo vya kuchimba dawa vichakani.

  1. Kwanza, Dk. Mwakyembe alisema ni kitendo cha udhalilishaji kisaikolojia, hasa kwa wanawake, kuvua nguo hadharani mbele za watu wakiwamo watoto wao ili kujisaidia.
  2. Pili, akafafanua kwamba mbali na kadhia hiyo, pia ni hatari kwa usalama wa abiria hao kwani huko wanakopelekwa kujisaidia si sehumu salama, wanaweza kukumbana na wanyama wakali wakiwamo nyoka hivyo kudhurika.
  3. Tatu na kubwa, Waziri Mwakyembe alisema vitendo hivyo vinaharibu mazingira, hivyo kuhatarisha usalama wa afya za wakazi wanaoishi jirani na maeneo husika, na kwamba serikali haiwezi kuvumilia kuendelea kukaa kimya.........


Tunadhani ipo haja ya wizara yake kushirikiana na wenye mabasi yaendayo mikoani, kuhakikisha vinajengwa vyoo vya umma katika maeneo mbalimbali kutegemeana na urefu wa njia ambavyo vitawekewa usimamizi wa kutosha ikiwa ni pamoja na kufanyiwa usafi. Vyoo hivi vinaweza kujengwa jirani na vituo vya kuuzia mafuta vilivyopo jirani na barabara au karibu na makazi ya watu halafu vikakabidhiwa kwenye usimamizi wa uongozi wa eneo hilo na wenye magari pamoja na serikali wakawa wanachangia gharama za matunzo na usafi. Baada ya hatua hizo kufanyika ni rahisi sana agizo la Waziri Mwakyembe kutekelezeka kwani kutakuwa na mbadala wa vichaka, abiria nao hawawezi kukubali tena kupelekwa huko wakati wanajua vipo vyoo mahala fulani..............


MWAKIEMBE AMEKURUPUKA BILA TATHMINI YA MAANDALIZI YA KUTOSHA

Kwa maoni yangu kauli ya Waziri Mwakiembe ni ya kukurupuka bila kujipanga, la sivyo angeleta upembuzi yakinifu namna gani serikali imejipanga kukabiliana na tatizo hilo kwa kushirikiana na umoja wa wenye mabasi nchini, au serikali yenyewe ingejipanga kivyake tu kama ilivyo kwa nchi nyingi.

Barabara kuu maeneo ya mwendo mrefu ambayo hayana restaurants kando yake, serikali inatakiwa kujenga vituo vya kupumzikia, si kwa wasafiri wa mabasi tu, ila kwa magari yote kuanzia usafiri binafsi, magari ya abiria na mizigo.

Maeneo hayo ambayo hujulikana kama REST AREA huwa na huduma muhimu ya vyoo, vitafunio na vinywaji kwa kununua, ingawa nchi nyingine vyoo kwa vile vimejengwa na pesa ya walipa kodi huwa havilipiwi ila vitafunio na vinywaji. Huwepo parking ya magari madogo na makubwa, ulinzi wa watu na mali zao na wahudumu.

Baada ya serikali kujiridhisha kwamba imeandaa maeneo hayo, hakungekuwa na pingamizi kuchukuliwa hatua za kisheria anayekiuka utaratibu wa kuchafua mazingira kwa kuwa sehemu za kupumzikia na restroom vimeandaliwa. Lakini kwa sasa vita hivyo si rahisi kushinda kutokana na maandalizi yasiyofanyika kwa kiwango na hasa kutegemea vituo vilivyopo vya watu binafsi bila kufikiria maeneo yenye umbali mrefu ambayo hayana huduma hizo.

 
Kuna mambo mengi mengi mazuri anayofanya Mwakiemba yananipa moyo, lakini hili la kuchimba dawa naungana na mleta mada anahitaji kulifanyia kazi zaidi, kwani si rahisi mtu kutoka daraja la mto Rufiji avumilie kutojisaidia hadi Kilwa kwa vile sheria inakataza. Watujengee vitua njiani vinginevyo tutembee na plastic bags.
 
...Nlikuwa nina mawazo kama yako kuhusu hili, lakini baada ya jana kutumia usafiri wa basi kati ya Dar na Mbeya na kuona mabasi yakiutumia utaratibu huo kwa uzuri kabisa, kwa safari nzima hiyo ya karibu km 800 hakukuwa na kuchimba dawa kwa mtindo ule wa zamani, nimeshuhudia vyoo vilivyojengwa huko polini kwa ajili ya abiria kujisaidia kwa kulipia Tsh 200, with time watu wengi zaidi wataanzia miradi hii ya vyoo barabarani...

...Baada ya practical case hiyo, sasa nimeamini na ninamuunga mkono Dr.Mwakyembe kuwa kumbe inawezekana sasa na sio kesho....
 
...Nlikuwa nina mawazo kama yako kuhusu hili, lakini baada ya jana kutumia usafiri wa basi kati ya Dar na Mbeya na kuona mabasi yakiutumia utaratibu huo kwa uzuri kabisa, kwa safari nzima hiyo ya karibu km 800 hakukuwa na kuchimba dawa kwa mtindo ule wa zamani, nimeshuhudia vyoo vilivyojengwa huko polini kwa ajili ya abiria kujisaidia kwa kulipia Tsh 200, with time watu wengi zaidi wataanzia miradi hii ya vyoo barabarani...

...Baada ya practical case hiyo, sasa nimeamini na ninamuunga mkono Dr.Mwakyembe kuwa kumbe inawezekana sasa na sio kesho....

Utaratibu huo sipingani nao, ila ni wa kiwango cha chini, ukitilia maanani kuwa itafika wakati wawekezaji hao wa vyoo bora wangepewa maeno wakafanya kitu cha kweli kuwa na kituo cha rest area na huduma ya kisima cha mafuta. Kujenga choo porini bila uwepo wa huduma nyingine ndugu yangu ipo siku utakuja na hoja kwamba kitu fulani kinakosekana.

Bora mwanzoni kuweka mipango kamili endelevu, kama yule wa pale Kitonga bondeni kafanya kweli, ingawa ni kubwa, tungehitaji wengine wajaribu kitu kama kile cha kiwango cha kati ambacho kitasaidia wasafiri wengi.
 
Anajua anachokifanya...tusubiri

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Anajua anachokifanya...tusubiri

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Mimi nasafriki kesho na nayaona matatizo chungu nzima tokana na tangazo hili, kusubiri anachofanya bila kuonyesha njia mbadala ya uhakika ya utatuzi wa tatizo hili nitafanyeje? Kuna njia ambazo ni mapori makubwa kama kuanzia Sikonge kwenda Chunya Mbeya. Toka Sikonge -Kitunda - Makongorosi - Chunya kazi kwelikweli.
 
Back
Top Bottom