Hii yetu wanaume.

Hii yetu wanaume.

Ukiona mtu anasisitiza pesa kwenye love elewa huyo si mpenzi,bali 'mgegedaji mwendazake' UPENDO unajengwa na kuelewana/kupatana kiroho,kinafsi na kimwili (mtiririko huo wa kiroho,kinafsi na kimwili) usipinduliwe hivyo ni vipaumbele muhimu ili UPENDO udumu
 
Mtajisimbua bure lakini ukweli ni huu... " wanawake hawajui wanataka nini exactly..."
 
Mtu aliye single ana enjoy sana. Vitu vyota hivyo anahitaji mwanamke??
 
Ndo maana nasema hii tabia yakuendesha mapenzi kupitia majarida na tamthilia ambapo mtu anayetoa huo ushauri hajawahi kuwa na mwanamke zaidi ya mke wake afu anazungumzia utafiti wakimapenz kwa watu wote huko nikudanganyana kabisa na porojo ambazo KAMWE utekelezaji wake HAUPO chini ya jua hili,mtu anakuambia mwanamke anahitaji care nakupendwa hata kama akukosee...dah!!asee hii ni kwingine siyo dunian hakyanani,kwanza ww jaribu kuwa kama wanavyoshaur uone kama hujakonda hadi kichwa kwa mawazo..

Mkuu mie huwa nasoma then, naishia kucheka tu nikilinganisha na experience yangu...
 
hii misamiati yenu hii.......watoto wenyewe wanavyong'aa macho kama tanuri la gongo......we jitahidi tuu....
 
Ni kweli ulichoongelea Mkuu lakini the last ingredient in practicality ni pesa tu, unaweza fanya yote hayo ila bila pesa to support the other things haitasaidia lolote
 
Utafiti mdogo unaonyesha kuwa
kuna vitu vya kimsingi ambavyo
wanawake wanaangalia na kama
hivyo vitakosekana basi mambo
huenda yasiwe mazuri katika
uhusiano wenu.
Mwanamke anataka awe
APPRECIATED: Najua wengi
watashangaa kwa nini siyo LOVE
kwanza. Ukweli ni kuwa Wanaume
wengi wanaweza kumwambia
mwanamke I LOVE YOU lakini
hawam-APPRECIATE. Kuwa
appreciated ni sehemu muhimu sana
ya mahusiano ambayo mwanamke
anahitaji.
Mwanamke anahitaji “DEEP
EMOTIONAL BOND WITH A MAN”.
Wanawake wanataka spouse wao
waelewe feelings zao na wawe
concerned nazo. Na pia wanapenda
kujua Spouse wao wanaf hisia zipi na
wanapenda kushare hizo feelings na
emotions.
Mwanamke anataka Mwanaume
ambaye atafeel kuwa yuko
“FEMININE and SEXY”. Anataka
kuwa na uhakika kuwa yeye ni
mwanamke bora aliyekuvutia kuliko
wengine na kwa nini. So u must
make it clear to her very regular.
Vinginevyo anakuwa na wasiwasi. So
usisangae unaulizwa mara kwa mara
“hivi kwa nini unanipenda” they want
an assurance.
Mwanamke anataka mwanaume
ambaye ni ROMANTIC. Romance ni
ubunifu wa kimapenzi. Hili
halielezeki, ni namna ya kuwa katika
MAPENZI na FURAHA katika
mahusiano. Wanawake wanataka
wafanyiwe mambo mengi madogo
madogo ambayo yataendelea
kuwahakikishia kuwa kweli
wanapendwa na wanafurahiwa.
Wanawake wanataka Mwanaume
ambaye yuko CONFIDENT au
anayejiamini.
Wanawake Wanapenda kuwa na
uhakika kuwa wenzi wao ni
WAAMINIFU.
Mwanamke anataka Mwanaume
mwenye MIPANGO inayoeleweka
katika maisha na awe AMBITIOUS.
Mwanaume ambaye ni MBUNIFU.
Mwanamke anataka mwanaume
Mkarimu na Mtoaji na si mkono wa
birika. LOL.
Mwanamke anataka Mwanaume
ambaye hatakuwa Mwenzi wake tub
ali pia RAFIKI yake.
Mwanamke anapenda Kupendwa
hata kama amekuboa. Anataka
wakati wote atosheke Mentally;
Emotionally and spiritually.
Mwanamke anataka Mwanaume
ambaye atampatia SECURITY na
PROTECTION. That he will be there
when she needs him no matter what.
SOURCE: Dismas Lyassa

We mpe hela mpe hela nasema helaaa.....
 
Back
Top Bottom