Hii UNICEF Promotion imekaaje?

Hii UNICEF Promotion imekaaje?

Hao ni matapeli wamedukua Account ya rafiki yako, nashangaa kwanini Facebook imekua rahisi hivi kudukuliwa, mpaka imebidi nitoe picha zangu zote kwani ukiwa na picha ndio wanatumia kusambazia.
 
vitu vingine unajiongeza tu mwenyewe.
ajira,kazi na madili watu wanapepeana kwa kujuana tena kimyakimya,iweje ghafla mibulungutu ya hela mtu asambaze kwenye mitandao!.
 
Nimempigia simu huyu rafiki yangu ameniambia sio yeye kabisa ameniambia wamedukua account yake kuna siku aliwatukana wao wakampigia simu kabisa ya video wakawa wanaongea wakawa wanaongea kiswahili cha Kenya wanamuambia wewe mzee unafikiri sisi tutaishi vipi acha kuharibia watu.Akawaambia sawa tafuteni maisha lakini sio kwa njia hii ya kudanganya watu.Wakamuambia tulikuwa Tanzani juzi kwa sasa tuko Kenya na account yako tunaitumia.
Wakageuka kuwa kama watani wakamuuliza wewe unaonekana DON sana una gari akawajibu issue ya mimi kuwa na gari haiwahusu.
Sasa wakamuambia rafiki kwa taarifa yako tumekusanya millioni2 sasa hivi wanaongea kama matani tu.
Nimetoa haya TCRA na wananchi wengine tuwe aware sana imagine mtu anakuuliza account number yako for what?.
Hivi kama kuna kupeana hela kuna haja gani ya kufanya kazi
 
Ni matapeli ukifungua kupitia Facebook wanakutumia namba ya msimbo kupitia simu yako, ukiingiza wao ndio wanakuwa na access ya akaunti yako, hata hiyo Msg hajakutumia jamaa yako, wapi hapo Kenya River achana nao
😂Ndio yale mambo account za FB tunaona zinapost "pono" ?
 
Back
Top Bottom