Hii tabia jamani kama unayo jitahidi kuiacha

Hii tabia jamani kama unayo jitahidi kuiacha

mkuu umenikumbusha mbali sana!
tukiwa wadogo na njaa ya shule basi unapakuwa kumkomoa mwingine!

basi mamangu akikwambia punguza ukagoma! anakuuliza mara tatu utamaliza ukimwambia ndiyo mara zote na akakubembeleza upunguze
ukakataa! ndugu hicho chakula utamaliza hata ikibid kwa viboko!

akikuona umeshiba na hujamaliza anakuita ukae karibu yake!
basi tulikuwa tunamaliza huku tunalia! coz umeshiba ila ndo lazima umalize


Hahaha mkuu tumekulia nyumba moja nin yaan kichapo utakachochezea utajutaaa
 
Kweli kabisa ndugu yangu huo ndio ulafi ambao ni moja ya dhambi kubwa
 
Kweli hii ni tabia mbaya. Unajua watu wengi wanaofanya hivi sikwamba wananjaa, ni tamaa na hamu zinawasumbua. Unakuta mtu kasikia harufu tu ya chips au wali, anaagiza na kudai ajaziwe jaziwe Halafu akipewa hata hamalizi chote.
 
mwingine anapakua kidogo tu nacho anabakiza yan ye ashajiwekea kubakiza hata iweje! najiuliza nakosa jhbu

Kuna makabila ukimaliza chakula kwenye sahani wanaamini hujashiba! Lazima ubakize kidogo ili kujulikana umeshiba.
 
Hata kama umepakuliwa omba ambunguze kabla haujaanza kula yaan mi naonaga uchungu kumwaga chakula alichoacha mtu wakati wengine . hata mlo mmoja na hawajui watapata wapi msosi

Ni kweli na ndivyo inavyotakiwa lakini watu wengine hawasemi sijui ni ujinga,unafiki au ushamba tu unakuta anaogopa au anaona aibu kusema kinachomfaa. Kwasasahivi hata kwenye sherehe inabidi watu tubadilike tuchukue vile tunavyoviweza,siyo lazima kuchukua bufee la kwanza mpaka la mwisho, unakuta mtu hata hali anaenda kulamba lamba na kuacha..
 
Back
Top Bottom