GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Ukweli ni jambo muhimu ambalo litanusuru mambo mengi, kwa siku kadhaa nimekuwa nikimfuatilia dada fulani ambaye kanihakikishia kuwa yuko free, si hivyo tu pia kanihakikishia kuwa yuko tayari kuwa na mimi. Nimejipanga kadri ya uwezo wangu kupeleka barua ndo ananiambia kuwa samahani nimechumbiwa. Baada ya kuchunguza nimegundua ni kweli kachumbiwa na jamaa mmoja ambaye anaishi Dubai toka mwaka jana mwezi wa nne. Huu sio ustaarabu bora kuwa wawazi, ndani ya miezi minne niko na matumaini kumbe najivunia garasa. SI TABIA NZURI kuweni wazi, ona sasa wiki nzima sina raha nashindwa hata kufanya kazi zangu kwa ufanisi.