myhem
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 933
- 363
Wanafunzi ambao walianza darasa la kwanza mwaka 2002 ni wanafunzi ambao wana bahati sana,walipoanza shule tu ada ikafutwa,walipofika darasa la nne tu kurudia darasa kukafutwa na hatimaye kuibukia form one mwaka 2009 bahati ikazidi kuwaangukia coz kurudia form two kulifutwa.Kwa kudhibitisha bahati yao na matokeo yao ya mtihani wao wa form 4 yamefutwa baada ya kufeli sana,hivyo yanapangwa upya ili waweze kufaulu..Daah hawa vijana wana bahati sana nahisi dhambi zao pia zitakuwa zimefutwa!