Kuna moja ilirekodiwa mahali nikiiweka hapa watu watakufa kwa kucheka...
Sent using Jamii Forums mobile app
Pale nje ya Shule ya Sekondari Kambangwa karibu na mahakama ya Kinondoni, kuna kijiwe cha kahawa cha Msisiri. 2002 nilijichanganya kukalia benchi nitest viwango vyangu nikaona na wa upande wa pili naye kainuka, hataki kucheza na mimi. Wenzake (kisanii, maana najua wanaujua mchezo wao) wakamuuliza, vipi bingwa mbona unainuka, akawajibu maishani mwake hajawahi kucheza disco toto, yaani mimi sio size yake.
Basi wakamuita mtoto mdogo mpita njia eti ndio akae acheze na mimi. Njoo cheza na mwenzako, dah. Ile kamecheza tu kete ya kwanza, nikasikia wooote kwa pamoja wanasema "heko", nikicheza mimi utasikia "mmmh, bora ulivyosimama...ulikuwa na kesi ya mauaji. Yule dogo alinifunga asee, maana si kwa mbeleko zile
mchezo hautaki hasiraKabisa.....nlikuwa naanza kujawa upepo.... Nikakosa kufikiria.
Carina ndugu yangu iliniweka karantini ikaja na Corona ndo shida ikawa kubwa zaidi.
Hiyo jamaa anatukana sana mkuu, nisije kula bani asee.Iweke plz
Ukicheza vibaya, alafu mchezo unakaribia kuisha, wapembeni, wanamwambia jamaa, kamtumbulie mbali huko, hapa atanuka.Mkuu hakuna michezo yenye ku hitaji uvumilivu kama huo, na kupotezea watu, hasa kiringe kikiwa na Wazee wa swahili waweza jitafutia murder case.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaaaaaa,,daaUkicheza vibaya, alafu mchezo unakaribia kuisha, wapembeni, wanamwambia jamaa, kamtumbulie mbali huko, hapa atanuka.
Hahahaha mkuu kwenye mabewe lugha ya matusi ni kawaida sana na hua na enjoy sana kuangalia pambano ambalo magwiji wakicheza halafu wawe na maneno ya shombo
Kuna siku nilienda kijiweni nikakuta kadogo kanawafunga wazee halafu kanachezea draft mkono wa kushoto. Nilipofika tu nikakuta kuna mzee ndio anatolewa nje baada ya kufungwa na hicho kidogo.
Mzee wakati ananyanyuka dogo akamuambia mzee hizo goli nilizokupiga hutakiwi kukaa hapa kanawe kwanza ndio uje tena
Daah wakati nastaajabu kuona mtoto akimtolea maneno ya shombo mdingi, kuna mzee mwingine akaingia, yule mzee aliyetoka akawa anampa kete kwa kumpisha mzee mwenzake ili aendelee kucheza na yule dogo ambaye anawasumbua, yule mzee akamjibu mzee mwenzake kua weka kete chini usinipe mkononi usije ukaniambukiza gono ulilopewa na huyo mtoto
Mzee akaendelea kucheza, yule dogo akampiga force kingi mzee halafu dogo akamuambia yule mzee "hebu visha hiyo kingi kabisa maana maradhi ni mengi"
Kwa nini na wewe usifanye nao?maana si lazima kucheza draft