Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,860
- 50,626
Mimi sina hata chembe ya ujuzi wa masuala ya kiuchumi, siyajui kabisa,lakini najua kuna sera ambazo huendesha mambo ya mabenki kwenye nchi zote duniani. Na sera hizo hutungwa au hupitishwa na wanasiasa.
Swali langu ni hili: Hapa Tanzania mtu akienda kukopa mkopo binafsi kwenye taasisi za kifedha hukatwa kiasi fulani cha fedha kama gharama za mkopo. Kwa mfano mtu anakopa milioni Ishirini (20,000,000) basi hukatwa hadi shilingi laki sita(600,000) kama gharama za Mkopo. Hivi hii ni sahihi kweli? Benki inaandika imemkopesha Ml. 20 wakati kiuhalisia mkopoji kaondoka na Ml. 19,400,000. Ni haki kutoza Riba kwa kusema unatoza riba kwenye Ml.20 ya mkopo wakati Mkopaji mwenyewe umempa Ml. 19,400,000?. Nataka kujua kama huu ni utaalam wa kibenki au ni sera za kibenki au ni mfumo uliopo kwa kufuata sera za BOT?
Swali langu ni hili: Hapa Tanzania mtu akienda kukopa mkopo binafsi kwenye taasisi za kifedha hukatwa kiasi fulani cha fedha kama gharama za mkopo. Kwa mfano mtu anakopa milioni Ishirini (20,000,000) basi hukatwa hadi shilingi laki sita(600,000) kama gharama za Mkopo. Hivi hii ni sahihi kweli? Benki inaandika imemkopesha Ml. 20 wakati kiuhalisia mkopoji kaondoka na Ml. 19,400,000. Ni haki kutoza Riba kwa kusema unatoza riba kwenye Ml.20 ya mkopo wakati Mkopaji mwenyewe umempa Ml. 19,400,000?. Nataka kujua kama huu ni utaalam wa kibenki au ni sera za kibenki au ni mfumo uliopo kwa kufuata sera za BOT?