Hii picha yanikumbusha jinsi watu walivyo wazembe na kutokuwa na tahadhari.Wanapenda kusema "hakuna neno bwana, iko sawa."
Iko siku nilimpa kijana wa bodaboda mkungu wa ndizi anipelekee nyumbani.Akauweka kwenye pikipiki bila kufunga na mpira kama ilivyo kawaida. Nilipomwuliza akaniambia kwa mikogo mingi sana, "mama, hii kazi tunaijua, hakuna kitakachoharibika"
Mkungu ulidondoka ukasagikasagika leo hii namdai mkungu wangu.
Hapo kwenye mayai pia kuna tatizo ambalo halikuzingatiwa kwa sababu ya uzembe wa wahusika