Hii ndiyo Ubungo!

Hii ndiyo Ubungo!

wilson peter

Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
32
Reaction score
10
Nipo kwenye foleni maeneo ya Ubungo hapa, nimeshuhudia kijana wa watu tena mkakamavu tu akiwa na kibegi chake akikaribishwa mjini na hawa jamaa wa karata 3 au mda mwingine hutumia vipande vya biskuti kwa mtindo ule ule wa kutaka kujipatia mkwanja faster faster. Alikuwa analia ila wasamaria wanamfariji na kumwambia "wezi wale, na ukiwafata watakuchoma visu ".

Vipi ndugu zanguni, hakuna aliewahi kuingizwa mjini maeneo haya ya Ubungo kwa style yoyote ile? Tuwe wakweli tu.
 
dah nipo kwenye foleni maeneo ya ubungo apa, nimeshuhudia kijana wa watu tena mkakamavu tu akiwa na kibegi chake akikaribishwa mjini na hawa jamaa wa karata 3 au mda mwingine hutumia vipande vya biskuti kwa mtindo ule ule wa kutaka kujipatia mkwanja faster faster. Alikuwa analia ila wasamaria wanamfariji na kumwambia "wezi wale, na ukiwafata watakuchoma visu ".
vipi nduguzanguni, hakuna aliewahi kuingizwa mjini maeneo haya ya ubungo kwa style yoyote ile?? tuwe wakweli tu.


"Ukiweka kwenye keusi umepata, ukiweka kwenye kekundu umeliwa"
 
Mi nlitoka chuo napanda daladala mchana kweupe wamenichomolea nilicheka kwa huzuni huyo home cku kombe la dunia linaanza sisahau wale washikaji n noooma na ukismama wanakuletea cmu wanauza.
 
hao jamaa ni majambazi na wanakula sahani moja na polisi, ukishtaki unanyea debe wewe
 
Karata tatu, hao jamaa wanakuwa kitu kimoja ili kuwaingiza mkenge wapita njia na wanakuwa na wanawake katika kundi lao ili wawapate hadi wanawake kiurahisi
 
mjini akili kijijini shule...! chukua hatua.
 
Nipo kwenye foleni maeneo ya Ubungo hapa, nimeshuhudia kijana wa watu tena mkakamavu tu akiwa na kibegi chake akikaribishwa mjini na hawa jamaa wa karata 3 au mda mwingine hutumia vipande vya biskuti kwa mtindo ule ule wa kutaka kujipatia mkwanja faster faster. Alikuwa analia ila wasamaria wanamfariji na kumwambia "wezi wale, na ukiwafata watakuchoma visu ".

Vipi ndugu zanguni, hakuna aliewahi kuingizwa mjini maeneo haya ya Ubungo kwa style yoyote ile? Tuwe wakweli tu.

miaka ya 1999 walinila hela zangu za shule sana nikawa napiga deshi mda wa lunch
Nilivyokuja kustuka nikawapotezea hawakuniona tena.
Wale jamaa vimeo sana
 
Watu walikuwa wanamfariji kwa nini?? Hivi hadi leo kuna watu bado wakiona sehemu wanachezesha karata 3 nao wanacheza wakitegemea kushinda? Hata kama umetoka bush leo, huu wizi ulishagunduilka na kutadhalishwa sana toka miaka ya 80's kweusi huko!
 
miaka ya 1999 walinila hela zangu za shule sana nikawa napiga deshi mda wa lunch
Nilivyokuja kustuka nikawapotezea hawakuniona tena.
Wale jamaa vimeo sana

mkuu umenifurahisha sana.. inaelekea kila mda wa lunch ulikuwa unawakumbuka majamaa.
 
Watu walikuwa wanamfariji kwa nini?? Hivi hadi leo kuna watu bado wakiona sehemu wanachezesha karata 3 nao wanacheza wakitegemea kushinda? Hata kama umetoka bush leo, huu wizi ulishagunduilka na kutadhalishwa sana toka miaka ya 80's kweusi huko!
Kuna mmoja kasema alikuwa analiwa mwaka 1999!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom